Machangudoa wa UK kiboko,tahadhari kwa wana JF

Cho! bhebhe nang'ho si, mamihayo ke ayo?? na chene ule makoye matale,pamoja homm buoy.


haha hommie nilikuchakachua gasineyo uliogukaya....mkuu kwetu kuacha hiyo kitu dhambi...kula then omba ushauri mambo ya Stess sijui Straus mbele ya mahakama.....ulimhola namhala? hahahahaha pot wamekushambulia ka wa kona...sasa ngoja niilinde Siredi yako usijali...ripoti atakaye kuletea hahahaha
 
Kwa kiasi fulani huu mtiririko umekosa mshiko............aidha mkuu mvua ya kiangazi unasema kweli lakini ni mzembe (tusi kama wewe ni mwanasheria) ama unachangamsha kijiwe tu! 1. Aliyekupokea umesema ni mhudumu wa hoteli tena unafika hoteli eti anasema mko wote?? Masuala yanaanza kunitanza, hivi hapo reception hawamjui mhudumu wao? 2. Umesema msichana ni miala 17-19? Well, in UK hotel reps wao wengi wanaopokea wageni ni kuanzia miaka 30, kwa sababu mimi nimeshawahi kuifanya hii kazi na kuipata kwake, mbali ya mambo mengine wanataka pia lazima uwe na uzoefu kwenye udereva (at least miaka 3 bila points kwenye leseniya udereva) na uwe walau kuanzia miaka 25 (kwa sababu ya bima) Huyo msichana leseni alipata akiwa na miaka mingapi? ama unataka kutwambia mulikodi gari? Kwa huduma ya mapokezi wakifanya hivo ni hasara. 3. Uliondoka London J3 siku ya kesi? inawezekana kama ulipanda domestic flight ila haijakaa vema kwamba unasafiri siku ya kesi yenyewe, ukizingatia usafiri na hata kama ulienda na ndege bado kuna morning traffic jam toka J. Lennon airpot kwenda City. wacha niishie hapa.
Mnaojua mitaa ya huko ughaibuni mnatutesa sana wengine maana jamaa hapo anaongea kirahisi kama vile anazungumzia kupanda daladala la ubungo-msasani ukashukia kwa mtogole ukapita kijitonyama kwa Alli Maua ukatokea Sayansi n.k
 
Yaani Faiza foxy, mii ningekuwa mod ningemban tuu humu ndani maana comment zake zingine utadhani kaumbwa na Mungu ili kupika majungu tuuuuu, no constructive criticism.
 
Wa Ndugu,Kama wiki moja hivi iliyopita nilikuwa Liverpool,UK kwa dhumuni la kumuwakilisha mteja wangu kwenye baraza(tribunal) moja la migogoro juu ya biashara ya pamba, nilipofika Heathrow Airport nilikutana na binti mmoja umri wake kama 17-19 akiwa na bango lenye jina langu la kunikaribisha,akajitambulisha kuwa anaitwa Cassie na ni mhudumu wa hotel niliyopanga kufikia:Kwa kuwa ilikuwa week end nilipanga kukaa London muda wote hadi jumatatu ambayo ilikuwa siku ya kesi, nikaongozana nae moja kwa moja hadi hotelini,tulipofika reception tukaulizwa mko pamoja?? akajibu "oooh, yes! akanisindikiza hadi chumbani kwangu na akaniomba aingie ili aweke mizigo yangu,kwa kuwa nilijua labda ndiyo British hospitality nikakubali.............kumbe ilikuwa janja ya nyani[ili ionekane kama tuko pamoja,yaani nimekuja nae] alipofikisha mizigo akaniaga na kuondoka.Baadae niliondoka mpaka Sussex kuonana na ndugu yangu mmoja na kula bata kiaina,niliporudi usiku reception wakaniambia funguo anazo mwenzangu.....nikaduwaa lakini sikutaka kuwashtua ili nijue nini kinaendelea in case mambo yakienda kombo niwa sue(niwashtaki kwa usumbufu ili wanilipe fidia)...basi ile kuingia chumbani,nikamkuta Cassie akiwa na night dress ameketi kwenye kijimeza,amewasha mishumaa huku akinywa mvinyo akanipokea kwa mahaba mazito kwa maneno ya ulaghai.......AT YOUR SERVICE P'SE,nikamuuliza what service?? akaanza kusaula,nikasema yaleyale ya STRAUSS KAHN!!!! nikachukua simu ili kupiga reception na polisi akanisihi nisifanye hivyo kwani yupo kazini,nilipomuuliza kwa nini hakusema akaniambia yeye sio HO, bali anatafuta pesa za kwenda mapumzikoni tu........nilipomsamehe aliniporomoshea matusi makubwa eti mi nyani tu................Hayo ndo yaliyonisibu,kwa hiyo mkuwe makini jamani wale mnaopenda kutembelea pande hizo........
hihiii...:D...POYEEEE
 
haha hommie nilikuchakachua gasineyo uliogukaya....mkuu kwetu kuacha hiyo kitu dhambi...kula then omba ushauri mambo ya Stess sijui Straus mbele ya mahakama.....ulimhola namhala? hahahahaha pot wamekushambulia ka wa kona...sasa ngoja niilinde Siredi yako usijali...ripoti atakaye kuletea hahahaha

Cho,mhola guke nyand'one,tole hamo nkoi................
 
Mnaojua mitaa ya huko ughaibuni mnatutesa sana wengine maana jamaa hapo anaongea kirahisi kama vile anazungumzia kupanda daladala la ubungo-msasani ukashukia kwa mtogole ukapita kijitonyama kwa Alli Maua ukatokea Sayansi n.k

Hahahaha! Watu mna vituko nyie! Au ni kama vile kutanua pale mahakama ya Kisutu, unakuja kutokea Diamond Jubilee, unakamata barabara ya Umoja wa Mataifa mpaka Salender Bridge; hilo lote ni zoezi la kukwepa foleni! Tehetehetehetehe!
 
Back
Top Bottom