BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,789
- 288,015
Mabweni UDSM yalanguliwa
na Mobini Sarya
Tanzania Daima~Sauti ya Watu
WIMBI la kuuza vyumba vya kulala wanafunzi katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) sehemu ya Mlimani, limeshika kasi hivyo kuwafanya wanafunzi wengi wanaotokea familia maskini kushindwa kumudu gharama ya kupanga.
Inadaiwa vyumba vilianza kuuzwa sh 100,000. Hivi sasa chumba kimoja kinauzwa hadi sh 300,000 kupitia kwa mawakala ambao ni wanafunzi wanaokula na wahusika.
Taarifa hizo zinadai biashara hiyo inayowahusisha wasimamizi wa vyumba na madalali, imeanza siku chache baada ya chuo hicho kufunguliwa Septemba 29, mwaka huu, hivyo kuwalazimu watoto wa maskini wanaoshindwa bei hiyo kuamua kupanga mitaani.
Akizungumza na Tanzania Daima kwa njia ya simu, mmoja wa wabunge katika serikali ya wanafunzi (Daruso), alisema hivi sasa biashara hiyo inafanyika bila kificho.
Unakuta tangazo kwenye ubao wa matangazo kwamba chumba kinauzwa shilingi kadhaa kwenye jengo fulani na ghorofa namba fulani, lakini mtu huyo hakamatwi, alisema mbunge huyo ambaye jina lake limehifadhiwa.
Inaelezwa kwa kawaida mwanafunzi anatakiwa kuomba chumba kupitia mtandao wa chuo na kupewa na kisha kulipia sh 50,000 kwa muhula mmoja na iwapo atashindwa chumba hurudishwa kwa kitengo kinachohusika ili apewe mtu mwingine.
na Mobini Sarya
Tanzania Daima~Sauti ya Watu
WIMBI la kuuza vyumba vya kulala wanafunzi katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) sehemu ya Mlimani, limeshika kasi hivyo kuwafanya wanafunzi wengi wanaotokea familia maskini kushindwa kumudu gharama ya kupanga.
Inadaiwa vyumba vilianza kuuzwa sh 100,000. Hivi sasa chumba kimoja kinauzwa hadi sh 300,000 kupitia kwa mawakala ambao ni wanafunzi wanaokula na wahusika.
Taarifa hizo zinadai biashara hiyo inayowahusisha wasimamizi wa vyumba na madalali, imeanza siku chache baada ya chuo hicho kufunguliwa Septemba 29, mwaka huu, hivyo kuwalazimu watoto wa maskini wanaoshindwa bei hiyo kuamua kupanga mitaani.
Akizungumza na Tanzania Daima kwa njia ya simu, mmoja wa wabunge katika serikali ya wanafunzi (Daruso), alisema hivi sasa biashara hiyo inafanyika bila kificho.
Unakuta tangazo kwenye ubao wa matangazo kwamba chumba kinauzwa shilingi kadhaa kwenye jengo fulani na ghorofa namba fulani, lakini mtu huyo hakamatwi, alisema mbunge huyo ambaye jina lake limehifadhiwa.
Inaelezwa kwa kawaida mwanafunzi anatakiwa kuomba chumba kupitia mtandao wa chuo na kupewa na kisha kulipia sh 50,000 kwa muhula mmoja na iwapo atashindwa chumba hurudishwa kwa kitengo kinachohusika ili apewe mtu mwingine.