Mabalozi wa Umoja wa Ulaya (EU) wamlima barua Waziri Mkuu kuhusu Albino

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,329
33,139
mabalozi+px.png

Walemavu wa ngozi

Mabalozi wa nchi za Jumuiya ya Ulaya (EU) nchini Tanzania, wamelaani mauaji yaliyofanywa kwa mwanamke mmoja na watu wasiofahamika katika Wilaya ya Bariadi mkoani Simiyu, Mei 12, 2014 aliyekatwa baadhi ya viungo vya mwili wake akiwa nyumbani kwake na kuitaka Ofisi ya Waziri Mkuu kufanya uchunguzi wa kina ili kukomesha mauaji hayo ambayo yameibuka upya nchini mwaka huu.

Katika waraka ulioandaliwa na Mabalozi hao (FikraPevu tunayo nakala), Mei 20, 2014 wamesema pamoja tukio hilo kuwa la kwanzai hapa nchi kwa mwaka huu, kufuatia kifo cha mwanamke, Munghu Lugata (40), aliyeuwawa hivi karibuni katika mkoa huo, ambapo kifo hicho kimekuwa cha 73 kunzia mwaka 2000 huku wakijua kuwa watu wawili walioshikiliwa watatoa ushirikiano kwa Vyombo vinavyohusika ili kutokomeza mauaji hayo.

Aidha, wamesema pamoja na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, kuwa katika mstari wa mbele katika mapambano dhidi ya vitendo hivyo, wanahitaji kukutana kwa mara nyingine na Ofisi yake ili kujadili namna ya kuimarisha dhamira ya kutatua tatizo hilo nchini.

Wamebainisha kuwa Serikali inatakiwa kuchukua hatua muhimu ili kuzuia matukio hayo na kuhakikisha mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi Albino yanaisha hapa nchini pamoja na uchunguzi kufanyika ili kutokomeza dhana potofu iliyojengeka miongoni mwa jamii kuwa viungo vya walemavu wa ngozi Albino vikitumiwa na waganga wa jadi wanapata fedha nyingi.

Tukio la kuuwawa kwa mwanamke huyo ambalo liliwahi kuripotiwa na FikraPevu, tukio hilo lilitokea katika kitongoji cha Chalala kijiji cha Gasuma Kata ya Nkololo Wilayani Bariadi mkoani humo saa 12 jioni, kwa kukatwa mguu wake wa kushoto sehemu ya goti, vidole 2 mkono wa kushoto pamoja na ukucha wa kidole gumba, na wahusika kutoweka na viungo hivyo.

Hata hivyo, katika mahojiano ya FikraPevu na Jeshi la Polisi mkoani humo lilisema linawashikilia baadhi ya waganga wa jadi, ambao wamekuwa wakiwadanganya wananchi kuwa viungo vya mlemavu wa ngozi Albino vinaleta utajiri hali ambayo inawafanya baadhi ya wananchi kuamini hali hiyo na kuendeleza mauaji ya Albino katika maeneo mbalimbali nchini.

Kwa habari zaidi
:

Mabalozi wa Nchi za Jumuiya ya Ulaya walaani mauaji ya Albino Kanda ya Ziwa
 
Mauaji ya albino yana mkono wa wanasiasa na wafanyabiashara wakubwa. Wengi wanatafuta vyeo na utajiri kwa nguvu za giza. Na hili linajidhihirisha wakati wa uchaguzi jinsi wanavyoandamana kwenda kwa waganga wa kienyeji. Wanapofika huko mojawapo ya masharti wanayopewa ni kupeleka viungo vya albino. Hao mabalozi wa EU hilo hawana habari nalo? Heri wajinyamazie tu kwa kuwa mauaji ya albino kuisha Tanzania kwa sasa ni ndoto!
 
Mpaka wazungu waseme,ok nyie mabaloz semen bas na haya mahandak yaliyo katikat ya barabara ya uhuru had mnaz mmoja yafukiwe.Maana barabara hii n ya kihistoria
 
Mauaji ya albino yana mkono wa wanasiasa na wafanyabiashara wakubwa. Wengi wanatafuta vyeo na utajiri kwa nguvu za giza. Na hili linajidhihirisha wakati wa uchaguzi jinsi wanavyoandamana kwenda kwa waganga wa kienyeji. Wanapofika huko mojawapo ya masharti wanayopewa ni kupeleka viungo vya albino. Hao mabalozi wa EU hilo hawana habari nalo? Heri wajinyamazie tu kwa kuwa mauaji ya albino kuisha Tanzania kwa sasa ni ndoto!

Wafanyabiashara wanasingiziwa Tu, haya mauaji yana mkono wa wanasiasa peke yao, tena wa CCM. We hujiulizi kwa nini baada ya uchaguzi 2010 mauaji yalikoma?!! Ina maana BIASHARA ZILISIMAMA?? Wafanyabiashara wamegeuzwa "easy target" na wanasiasa. Mauaji yamerudi sasa wakati tunaelekea uchaguzi mkuu na ndio kwanza kazi imeanza. Halafu maskini ya Mungu wanaotakiwa kuwalinda Albino Ni hao hao wanasiasa akina Pinda.

Nilisimuliwa kisa kimoja kuwa kuna mgombea ubunge wa jimbo moja kule Bunda, Mara wakati wa uchaguzi 2010 ilikuwa kila mtu anayechukua hela kwa ajili ya kumpigia kura ilikuwa lazima aruke FUVU la albino kwa minajili kuwa akipiga kura tofauti atakufa. So ilikuwa unachukua elfu kumi yako a.k.a msimbazi, then unaruka Fuvu la albino kwa kutanguliza mguu wa kushoto then unasepa zako. We hujiulizi kwa nini kura ni za siri lakini watu wakipewa hela hawaendi kutenda kinyume wakati hakuna mtu anawaona??!!
 
Wafanyabiashara wanasingiziwa Tu, haya mauaji yana mkono wa wanasiasa peke yao, tena wa CCM. We hujiulizi kwa nini baada ya uchaguzi 2010 mauaji yalikoma?!! Ina maana BIASHARA ZILISIMAMA?? Wafanyabiashara wamegeuzwa "easy target" na wanasiasa. Mauaji yamerudi sasa wakati tunaelekea uchaguzi mkuu na ndio kwanza kazi imeanza. Halafu maskini ya Mungu wanaotakiwa kuwalinda Albino Ni hao hao wanasiasa akina Pinda.

Nilisimuliwa kisa kimoja kuwa kuna mgombea ubunge wa jimbo moja kule Bunda, Mara wakati wa uchaguzi 2010 ilikuwa kila mtu anayechukua hela kwa ajili ya kumpigia kura ilikuwa lazima aruke FUVU la albino kwa minajili kuwa akipiga kura tofauti atakufa. So ilikuwa unachukua elfu kumi yako a.k.a msimbazi, then unaruka Fuvu la albino kwa kutanguliza mguu wa kushoto then unasepa zako. We hujiulizi kwa nini kura ni za siri lakini watu wakipewa hela hawaendi kutenda kinyume wakati hakuna mtu anawaona??!!

Duh, hii nayo kali, ila haya yote ni kwa sababu watu wema wa nchi hii wamenyamaza kimya!!!
 
Waliohukumiwa wanyongwe hadharani ili iwe fundisho, pia waganga wa jadi wote tz warudishe leseni wanawapotosha watu.pole kwa waliopoteza ndugu zao wenye asili ya albino,
 
Hao mabalozi waje groundzero watawajua wahusika wanaongea na mtu wa kulialia analia leo siku. Ya pili albino anauwawa
 
Uchaguzi mkuu unakaribia, unafikiri hawa ccm na mafisadi wao watakubali kuachia tonge lao. Documentary iliyopita ilionyesha bayana jinsi viongozi wa serikali wakiongozwa na dhaifu wao kwamba ni wahusika wakuu na ndio wateja.
 
Mauaji ya albino yana mkono wa wanasiasa na wafanyabiashara wakubwa. Wengi wanatafuta vyeo na utajiri kwa nguvu za giza. Na hili linajidhihirisha wakati wa uchaguzi jinsi wanavyoandamana kwenda kwa waganga wa kienyeji. Wanapofika huko mojawapo ya masharti wanayopewa ni kupeleka viungo vya albino. Hao mabalozi wa EU hilo hawana habari nalo? Heri wajinyamazie tu kwa kuwa mauaji ya albino kuisha Tanzania kwa sasa ni ndoto!

Ni aibu, wazungu kuwa na "huruma na kujali utu", sisi hatujali na tunaishia kulaani tu! Hivi katika ulimwengu huu, tunatawaliwa na mambo ya kishetani kweli? Tutafika wapi ikiwa hata baadhi ya viongozi na wakubwa ni wafuasi wa mambo haya. Mwenyezi Mungu Amlaze Mahali Pema huyo mama. Na Awalaani na Kuwapa Adhabu Kali wote waliohusika, Hapa duniani na Ahera.
 
mabalozi+px.png

Walemavu wa ngozi

Mabalozi wa nchi za Jumuiya ya Ulaya (EU) nchini Tanzania, wamelaani mauaji yaliyofanywa kwa mwanamke mmoja na watu wasiofahamika katika Wilaya ya Bariadi mkoani Simiyu, Mei 12, 2014 aliyekatwa baadhi ya viungo vya mwili wake akiwa nyumbani kwake na kuitaka Ofisi ya Waziri Mkuu kufanya uchunguzi wa kina ili kukomesha mauaji hayo ambayo yameibuka upya nchini mwaka huu.

Katika waraka ulioandaliwa na Mabalozi hao (FikraPevu tunayo nakala), Mei 20, 2014 wamesema pamoja tukio hilo kuwa la kwanzai hapa nchi kwa mwaka huu, kufuatia kifo cha mwanamke, Munghu Lugata (40), aliyeuwawa hivi karibuni katika mkoa huo, ambapo kifo hicho kimekuwa cha 73 kunzia mwaka 2000 huku wakijua kuwa watu wawili walioshikiliwa watatoa ushirikiano kwa Vyombo vinavyohusika ili kutokomeza mauaji hayo.

Aidha, wamesema pamoja na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, kuwa katika mstari wa mbele katika mapambano dhidi ya vitendo hivyo, wanahitaji kukutana kwa mara nyingine na Ofisi yake ili kujadili namna ya kuimarisha dhamira ya kutatua tatizo hilo nchini.

Wamebainisha kuwa Serikali inatakiwa kuchukua hatua muhimu ili kuzuia matukio hayo na kuhakikisha mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi Albino yanaisha hapa nchini pamoja na uchunguzi kufanyika ili kutokomeza dhana potofu iliyojengeka miongoni mwa jamii kuwa viungo vya walemavu wa ngozi Albino vikitumiwa na waganga wa jadi wanapata fedha nyingi.

Tukio la kuuwawa kwa mwanamke huyo ambalo liliwahi kuripotiwa na FikraPevu, tukio hilo lilitokea katika kitongoji cha Chalala kijiji cha Gasuma Kata ya Nkololo Wilayani Bariadi mkoani humo saa 12 jioni, kwa kukatwa mguu wake wa kushoto sehemu ya goti, vidole 2 mkono wa kushoto pamoja na ukucha wa kidole gumba, na wahusika kutoweka na viungo hivyo.

Hata hivyo, katika mahojiano ya FikraPevu na Jeshi la Polisi mkoani humo lilisema linawashikilia baadhi ya waganga wa jadi, ambao wamekuwa wakiwadanganya wananchi kuwa viungo vya mlemavu wa ngozi Albino vinaleta utajiri hali ambayo inawafanya baadhi ya wananchi kuamini hali hiyo na kuendeleza mauaji ya Albino katika maeneo mbalimbali nchini.

Kwa habari zaidi
:

Mabalozi wa Nchi za Jumuiya ya Ulaya walaani mauaji ya Albino Kanda ya Ziwa

Kwa kweli inasikitisha sana,Mungu awalaze pema.La kufanya hapa ni kupiga marufuku waganga wote wa kienyeji,isipokuwa kwa wale wanaouza madawa ya miti shamba masokoni,kama viuzwavyo viavi na mahindi.

Lakini waganga wote hawa wanaojiita wanatoa utajiri,wanasafisha nyota,wanatoa majini nk,Hawa ni maadui namba moja wanaongamiza Maalbino na Wazee ambao ni tunu ya Taifa letu,Nawaomba waheshimiwa wabunge,wapitishe sheria mara moja ya kupiga marufuku.Huku ni kuingiza Taifa kwenye laana ya damu ya ndugu zetu wenyewe.Wahenga walisema "Shetani wa mtu ni mtu".
 
Back
Top Bottom