Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 234
Katibu Mkuu wa CUF, Maalim seif Shariff Hamad ambaye pia ni makamu wa Kwanza wa Rais wa Serikali ya mapinduzi (inayoongozwa na sera na ilani ya CCM) jana alijkwenda kwenye mkutano wa chama chake huko Manzese Dar, akiwa kwenye msafara wa magari ya serikali kinyume cha matumizo ya magari hayo, limeandika Mwananchi toleo la leo.
Seif aliwasili kwenye mkutano huo akiwa kwenye msafara wa magari zaidi ya sita, yakiwemo ya serikali likiwamo alilokuwa amepanda.
Msafara wake uliongozwa na pikipiki na magari ya msafara wa viongozi wa Jeshi la polisi .
Habari zaidi katika Mwananchi.
MY TAKE:
Inaonekana Maalim Seif anatumia hela za walipa kodi (ambazo siyo zile za ruzuku CUF inapata) kujikweza kisiasa na kuwafinya mahasimu wake katika chama chake.
Mwenzake aliyemnyonga hapo hadharani, yaani HR, hana uwezo huo jee hii kweli ni HAKI SAWA KWA WOTE?