Maadui wa CCM wanatengenezwa na wanaCCM wenyewe

Feedback

JF-Expert Member
Mar 14, 2011
7,988
4,507
Propaganda zinazosambazwa na vijana wa chama cha Mapinduzi CCM na baadhi ya viongozi wake zinakiongezea chama maadui bila sababu za msingi.

Imekuwa ni kawaida kwa vijana wa chama cha Mapinduzi kumuona kila mtu adui yeyote anayekosoa viongozi wake, chama au serikali, binafsi naona kama "ujinga mpya" umeingia ndani ya CCM ya sasa.

Hapo mwanzo vyama vya upinzani vilionekana kama adui wao mkuu, lakini siku za karibuni chama kimetengeneza maadui wengi kuliko marafiki zake. Yaani kwa sasa CCM na serikali yake hawamjui adui yao ni nani na rafiki yao ni nani, yeyote anayetoa mawazo mbadala kwao ni adui.

Mtu akisema kuwafukuza Acacia bila kurekebisha sheria za madini ni kazi bure anaitwa kibaraka wa mabepari. Akitokea mwingine akasema kuwanyima mikopo wanafunzi waliosoma shule binafsi ni ubaguzi, anatukanwa eti hataki watoto wa maskini wapate mikopo au anataka kukwamisha juhudi za rais Magufuli.

Leo hii makanisa yameongezwa kwenye orodha ya maadui wa CCM, akitokea Askofu akashauri jambo lisilowapendeza basi atashambuliwa na pengine kuchunguzwa uraia wake. Mchungaji Kakobe alisumbuliwa na TRA kwa kushauri viongozi 'watubu' akiwemo rais pengine kwa nia njema tu. Leo hii kanisa la KKKT limekuwa adui wa CCM kwa ukuitaka serikali ikomeshe uhalifu, Baraza la maaskofu katoliki (TEC) nalo liko kwenye orodha ya maadui wa CCM.

Wazazi na vijana wao wanaodai haki ya kupata mkopo wa elimu ya juu ni maadui wa CCM wamewekewa kigezo cha leseni ya biashara. Vyombo vya habari na Bloggers wote wanaodai uhuru wa vyombo vyao wamekuwa maadui wa CCM na serikali yake, leo kusajili blog lazima ulipe mamilioni ya pesa.

Mashekhe wa Uamsho tayari wao ni maadui wa CCM, Taasisi za Kiraia kama LHRC, TLS ni maadui wa CCM, Mtandao wa wanafunzi wa chuo vikuu TSNP nao ni maadui wa chama na serikali yake kwa vile tu wanadai haki yao.

Katika orodha ya maadui, CCM pia imewaunganisha hadi mataifa ya magharibi, Marekani na nchi za Umoja wa Ulaya EU wanaonekana ni maadui wa chama na serikali kwa hisia tu kuwa nchi hizo zinashirikiana na baadhi ya watu kuihujumu serikali ya Magufuli.

Kitu ambacho CCM hawakijui labda kwa ignorance ni kwamba kwa kadri wanavyotengeneza maadui wengi ndivyo wanavyopunguza marafiki, makundi haya (maadui zao) yakiungana pamoja dhidi ya serikali sijui kama CCM itaweza kuhimili nguvu yake.
 
Mimi nadhani CCM kutengeneza maadui ni furaha kwa wapinzani wa CCM!

Kinachoshangaza zaidi wapinzani ndio wanaishauri CCM isitengeneze maadui kwa sababu itashindwa kwenye Uchaguzi!

Yaani adui wa CCM inaipa CCM silaha ili CCM aitumie kumwangamiza huyo huyo aliyetoa silaha! This is fun to say the least!

Kweli za kuambiwa lazima uchanganye na zako!

Kama huzijui siasa za Tanzania lazima utaingia "mkenge"

Hao hao unaodai maadui wa CCM ndio hao hao wataiweka CCM madarakani kwa kuipa ushauri wakati wa Uchaguzi Mkuu.
 
Mimi nadhani CCM kutengeneza maadui ni furaha kwa wapinzani wa CCM!

Kinachoshangaza zaidi wapinzani ndio wanaishauri CCM isitengeneze maadui kwa sababu itashindwa kwenye Uchaguzi!

Yaani adui wa CCM inaipa CCM silaha ili CCM aitumie kumwangamiza huyo huyo aliyetoa silaha! This is fun to say the least!

Kweli za kuambiwa lazima uchanganye na zako!

Kama huzijui siasa za Tanzania lazima utaingia "mkenge"

Hao hao unaodai maadui wa CCM ndio hao hao wataiweka CCM madarakani kwa kuipa ushauri wakati wa Uchaguzi Mkuu.
Sikushangai kwa vile unacho-urgue tayari nimekizingatia kwenye mada yangu, kuwa yeyote anayetoa ushauri kwenu ni mpinzani au hakitakii mema chama.
 
Propaganda zinazosambazwa na vijana wa chama cha Mapinduzi CCM na baadhi ya viongozi wake zinakiongezea chama maadui bila sababu za msingi.

Imekuwa ni kawaida kwa vijana wa chama cha Mapinduzi kumuona kila mtu adui yeyote anayekosoa viongozi wake, chama au serikali, binafsi naona kama "ujinga mpya" umeingia ndani ya CCM ya sasa.

Hapo mwanzo vyama vya upinzani vilionekana kama adui wao mkuu, lakini siku za karibuni chama kimetengeneza maadui wengi kuliko marafiki zake. Yaani kwa sasa CCM na serikali yake hawamjui adui yao ni nani na rafiki yao ni nani, yeyote anayetoa mawazo mbadala kwao ni adui.

Mtu akisema kuwafukuza Acacia bila kurekebisha sheria za madini ni kazi bure anaitwa kibaraka wa mabepari. Akitokea mwingine akasema kuwanyima mikopo wanafunzi waliosoma shule binafsi ni ubaguzi, anatukanwa eti hataki watoto wa maskini wapate mikopo au anataka kukwamisha juhudi za rais Magufuli.

Leo hii makanisa yameongezwa kwenye orodha ya maadui wa CCM, akitokea Askofu akashauri jambo lisilowapendeza basi atashambuliwa na pengine kuchunguzwa uraia wake. Mchungaji Kakobe alisumbuliwa na TRA kwa kushauri viongozi 'watubu' akiwemo rais pengine kwa nia njema tu. Leo hii kanisa la KKKT limekuwa adui wa CCM kwa ukuitaka serikali ikomeshe uhalifu, Baraza la maaskofu katoliki (TEC) nalo liko kwenye orodha ya maadui wa CCM.

Wazazi na vijana wao wanaodai haki ya kupata mkopo wa elimu ya juu ni maadui wa CCM wamewekewa kigezo cha leseni ya biashara. Vyombo vya habari na Bloggers wote wanaodai uhuru wa vyombo vyao wamekuwa maadui wa CCM na serikali yake, leo kusajili blog lazima ulipe mamilioni ya pesa.

Mashekhe wa Uamsho tayari wao ni maadui wa CCM, Taasisi za Kiraia kama LHRC, TLS ni maadui wa CCM, Mtandao wa wanafunzi wa chuo vikuu TSNP nao ni maadui wa chama na serikali yake kwa vile tu wanadai haki yao.

Katika orodha ya maadui, CCM pia imewaunganisha hadi mataifa ya magharibi, Marekani na nchi za Umoja wa Ulaya EU wanaonekana ni maadui wa chama na serikali kwa hisia tu kuwa nchi hizo zinashirikiana na baadhi ya watu kuihujumu serikali ya Magufuli.

Kitu ambacho CCM hawakijui labda kwa ignorance ni kwamba kwa kadri wanavyotengeneza maadui wengi ndivyo wanavyopunguza marafiki, makundi haya (maadui zao) yakiungana pamoja dhidi ya serikali sijui kama CCM itaweza kuhimili nguvu yake.
Wamewanunua kazi hakuna waliona kaa LA moto na utamu wake kwenye unyayo
 
Ila tambua maadui wengi wa ccm wapo mjini, kijijini palipo na wengi wasioelimika bado ni marafiki wakubwa wa ccm na ndio wanaokujaga kuwaweka madarakani!
 
Sikushangai kwa vile unacho-urgue tayari nimekizingatia kwenye mada yangu, kuwa yeyote anayetoa ushauri kwenu ni mpinzani au hakitakii mema chama.
Suala sio kutoa ushauri bali unatoa ushauri kwa malengo gani.

Ushauri wa kinafiki ni chakula kwa wajinga lakini ushauri wa dhati na usio na unafiki ni chakula kwa watu wenye upeo mkubwa wa uelewa, hekima na busara.

CCM haiwezi kukubali ushauri wa kinafiki kwa sababu kufanya hivyo ni kujichimbia kaburi la kisiasa.

Kwa kukusaidia zaidi watoa ushauri usio wa kinafiki huwa hawapayuki ili kila mmoja ajue kuwa umetoa ushauri.
 
Ila tambua maadui wengi wa ccm wapo mjini, kijijini palipo na wengi wasioelimika bado ni marafiki wakubwa wa ccm na ndio wanaokujaga kuwaweka madarakani!
Siku hizi habari zinasambaa kwa haraka sana hazina cha mjini wala kijijini, mfano wa Waraka wa kanisa ulisomwa siku moja kwenye makanisa yote Tanzania nzima.
 
Suala sio kutoa ushauri bali unatoa ushauri kwa malengo gani.

Ushauri wa kinafiki ni chakula kwa wajinga lakini ushauri wa dhati na usio na unafiki ni chakula kwa watu wenye upeo mkubwa wa uelewa, hekima na busara.

CCM haiwezi kukubali ushauri wa kinafiki kwa sababu kufanya hivyo ni kujichimbia kaburi la kisiasa.

Kwa kukusaidia zaidi watoa ushauri usio wa kinafiki huwa hawapayuki ili kila mmoja ajue kuwa umetoa ushauri.
Usiseme kiujumla hebu onyesha unafiki uko wapi kwenye mada ili twende pamoja.
 
Tanzania hatuna viongozi. Ila tuna watawala.
Kwa sababu kwa mtu mwenye sifa ya uongozi hawezi kufikiria kila siku kuongeza maadui.
 
Back
Top Bottom