Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 234
Na Pamela Chilongola, Mwananchi
UONGOZI wa Mkoa wa Dar es Salaam juzi ulitengeneza barabara ya Kagera hadi Madoto iliyoko maeneo ya Mburahati usiku, kwa ajili ya ziara ya rais Jakaya Kikwete jana.
Rais Kikwete jana alitumia barabara hiyo kutembelea kisima cha maji cha jumuiya ya watumiaji Maji, (Mrosso) kilichopo maeneo ya Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Mburahati Wilaya ya Kinondoni.
Barabara hiyo, ilitengenezwa juzi usiku baada ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam William Lukuvi kuitembelea saa 10:00 jioni na kubaini kuwa isingefaa kutumika katika ziara hiyo ya mkuu wa nchi.
Baadhi ya wananchi walioshuhudia ujenzi huo walilieleza Mwananchi kuwa muda mfupi baada ya Lukuvi kupita eneo hilo, yalionekana malori yaliyokuwa yakimwaga vifusi vya mchanga kufukia mashimo kwenye barabara hiyo.
"Ujenzi huo, ulianza saa 12:00 jioni hivi na uliendelea hadi usiku.
"Ilipofika saa 3:00 usiku lilionekana tingatinga likichimba barabara na kusawazisha kifusi hicho jambo ambalo lilifanya wakazi wote wa eneo hilo wabaini kwamba kulikuwa na ugeni mkubwa wa kitaifa katika eneo hilo," alisema mkazi wa eneo hilo, Said Omary
Mwandishi wa habari hii jana aliikuta barabara hiyo ambayo siku zote ilionekana kuwa na mashimo, jana usiku ilikuwa ikisawazishwa kwa kuwekwa vifusi.
Hatua hiyo ya uongozi wa Mkoa wa Dar es Salaam umepokelewa kwa hisia tofauti baada ya baadhi ya watu kuiponda na wengine kusema imelenga kujikomba kwa rais Kikwete.
UONGOZI wa Mkoa wa Dar es Salaam juzi ulitengeneza barabara ya Kagera hadi Madoto iliyoko maeneo ya Mburahati usiku, kwa ajili ya ziara ya rais Jakaya Kikwete jana.
Rais Kikwete jana alitumia barabara hiyo kutembelea kisima cha maji cha jumuiya ya watumiaji Maji, (Mrosso) kilichopo maeneo ya Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Mburahati Wilaya ya Kinondoni.
Barabara hiyo, ilitengenezwa juzi usiku baada ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam William Lukuvi kuitembelea saa 10:00 jioni na kubaini kuwa isingefaa kutumika katika ziara hiyo ya mkuu wa nchi.
Baadhi ya wananchi walioshuhudia ujenzi huo walilieleza Mwananchi kuwa muda mfupi baada ya Lukuvi kupita eneo hilo, yalionekana malori yaliyokuwa yakimwaga vifusi vya mchanga kufukia mashimo kwenye barabara hiyo.
"Ujenzi huo, ulianza saa 12:00 jioni hivi na uliendelea hadi usiku.
"Ilipofika saa 3:00 usiku lilionekana tingatinga likichimba barabara na kusawazisha kifusi hicho jambo ambalo lilifanya wakazi wote wa eneo hilo wabaini kwamba kulikuwa na ugeni mkubwa wa kitaifa katika eneo hilo," alisema mkazi wa eneo hilo, Said Omary
Mwandishi wa habari hii jana aliikuta barabara hiyo ambayo siku zote ilionekana kuwa na mashimo, jana usiku ilikuwa ikisawazishwa kwa kuwekwa vifusi.
Hatua hiyo ya uongozi wa Mkoa wa Dar es Salaam umepokelewa kwa hisia tofauti baada ya baadhi ya watu kuiponda na wengine kusema imelenga kujikomba kwa rais Kikwete.