Lugalo sasa ni Hospitali ya Rufaa!

Bornvilla

JF-Expert Member
Feb 17, 2011
924
271
Hospital ya jeshi ya Lugalo imepandishwa hadhi na kuwa ya rufaa.
Source:TBC1
 
si wamesema mgomo umekwisha!mbona wanajichanganya?bugando haina specialists tusidanganyane.
 
Maspecialisti watawapata wapi? Au ndo kutoka kwa ayatola Khamenei.
 
Labda upeo wangu unaweza kuwa mdogo,lakini nikiwa nimezaliwa na kuwa kwenye maeneo ya kijeshi ninavyojua ni kwamba hizo hospital zimejengwa kwenye kambi za jeshi ili kuhudumia wanajeshi na familia zao kwasababu zipo ndani ya vikosi vya jeshi ambapo kuna siri kubwa kwa raia wa kawaida haruhusiwi kuingia anavyotaka,Sasa kuiweka hiyo hospitali ya lugalo kuwa ya Rufaa inamaanisha nini kuwa Raia wote dwataruhusiwa kwenda hapo je siri na unyeti wa jeshi upo wapi?au hiyo Rufaa ni kwa jeshi tu?tunaangamiza ulinzi na usalama wa nchi hiyo ni taasii nyeti sana ila siasa zitatumaliza,hiyo sio njia ya kutatua tatizo!!!
 
Hospital ya jeshi ya Lugalo imepandishwa hadhi na kuwa ya rufaa.
Source:TBC1

Serikali yetu inafanya mambo kama mtoto mdogo, yani hapo wanawalingishia madaktari kuwa wamepata mbadala wa MUHIMBILI, hivi kwanini hii serikali inaleta mambo ya kitoto hivi jamani?
 
Ni wakati muafaka hospitali zote kubwa ziwe chini ya JWTZ na wanaotaka kuomba kazi kama hawa interns na madaktari bingwa wawe wana JWTZ baada ya kuhenya. Hospitali kama Bugando, Muhimbili, rufaa Mbeya etc ziwe katika utaratibu huo na iwe mara moja.
 
Kila jambo hawa wenzetu wa CCM ni lazima wakurupuke au wafakamie.

Standard ni kitu ambacho wenzetu hata hawajui ni nini.

Mtu anasoma Diploma Mzumbe kwa taabu sana. Ana bebwa na kila mwalimu anahonga apewe mitihani anafanyiwa home work na mitihani. Mara akihitimu tunamsikia anafanya Masters part Time baada ya miaka 2 ana PhD na anjiita Dr kwa nguvu zote na serikali ya CCM inamkubali.

Ukigushi kiwango cha elimu yako umefungua mlango wa kugushi kiwango cha kila kitu.



Hospitali haiwi ya rufaa kwa kupandishwa daraja na NEC ya CCM yenye kila uoza wa watu wala haipandishwi daraja na kwa matamko yenye utata na jazba.

Kuna mambo kadhaa yenye kufanya hospitali iwe ya rufaa.

Madaktari bingwa
Vitendea kazi
Naafasi ya Kulaza wagonjwa
nk

Serikali ya CCM ni bingwa wa kulinyamazia jambo na kuishia kinyemela.
Naamini kabisa wanajua hamna kitu, hamna lolote ila wamesema ili waonekane bado wana uwezo wa kufikiri.
 
Kama ni kuamka na kutamka basi hata dispensary yetu ya kimara nayo ni hospital ya rufaa.. Period
 
Is this among the Govt strategie to tackle health sector crisis or what?coz from what i can sense sooner Amana hospital,Temeke,Mwananyamala,Selian hospital and many more will also be referal ones.We failed to support the few referalhospitals we have,yet we are adding the number.THIS IS CCM baaaana!
 
Back
Top Bottom