Ludovick Mwijage: The Dark Side of Nyerere's Legacy

Mwalimu wangu proffessor Shazia Reuben Mnyuku aliwahi kunifundisha kuwa hakuna technolojia isiyokuwa na matatizo. (There is no rechnology with zero risk). Hivyo mi nadhani tusiangalie mapungufu bali tuchukue yaliyo ya faida na siyo mapungufu. Mapungufu tuyazingatie katika kuchukua tahadhari lakini yaliyo mema tuyaenzi. Japo kuwa Mwalimu alikuwa na mapungufu mengi, hapana shaka kazi aliyoifanyia hii nchi ni kubwa sana kulinganisha na haya mapungufu. Ndiyo maana nasema japo hatunaye bado yungali anaishi mioyoni mwa watanganyika na watanzania kwa ujumla. Nyerere ni alama ya Tanganyika na Tanzania.

Umeongea kwa moyo mnyoofu....... maana hukatai kuwa alikuwa na mapungufu..... halafu pia hukatai kuwa alikuwa na mazuri...... wewe ni mwenye hekima....halafu unatoa hitimisho kuwa mabaya tuyaache tugange na mazuri tu.... sasa kuna ndugu zetu wengine wanasema tugange na mabaya ambayo kimsingi hayana hata chembe ya msaada...
 
Kuna wakati mwingine unajiuliza ni kwanini ulijua jambo fulani limhusulo mtu uliyemheshimu sana kwa kusikia sifa zake, kwa maana kwa kujua huko ile sifa yake yote huenda ikageuka kituko pale unapolinganisha na matendo yake.
 
Huu ni uongo Kama Wa akina FaizaFoxy mchango Wa Nyerere ktk ukuaji Wa TZ ni mkubwa usioweza kubezwa na kunguru yeyote.....
 
Last edited by a moderator:
It is good story and well told, could make a good movie. Yet, we need to establish why he (Ludovic) became the target of State machinery in the first place?
 
Dah! nna uhakika lugha imekupiga chenga na haujasoma kilichobandikwa, mwambie mleta mada akusaidie.

Nimesoma habari yote pamoja na Ku download hiyo PDF ndo maana nikawa na uhakika Wa kusema kuwa ni uzushi....

Bila Nyerere TZ isingestawi.....
 
Mkuu ungetumia muda wako kusoma hiko kitabu kwanza, kama tatizo ni lugha basi tafuta hata mkalimani akusaidie ili ukiwa unakosoa ukosoe kwa hoja.

Ningewezaje kukosoa bila kusoma? Umejuaje tatizo ni lugha? Vipi ningeungana na mwandishi je ungesemaje?

Nimesoma kitabu chote tena na tena but shutuma nyingi ni uzushi tupu....
 
Nyerere alikuwa binadamu kama binadamu yeyote yule, alikuwa na mapungufu mengi na muda mwingine unaweza ukasema 'aaa hata hili nalo'. Ukimsikia kamara Kasupa, Kamaliza, Bibi Titi na wengineo wengi hasa waliokuwa wapigania uhuru na haki kupitia vyama vya wafanyakazi utaona dhahiri kuwa Nyerere alikuwa na mapungufu na kwa hakika kabisa aliyoyafanya kunyamazisha vyama vya kiraia yana athari katika uhuru binafsi wa mawazo na ushiriki wa wananchi mpaka leo hii. Kipi cha maana katika hayo mapungufu ya Nyerere? La maana ni kuwa misingi aliyoiacha Nyerere inaumiza na kuwanyima haki watu wengine mpaka leo hii aidha kwa kuendelezwa kwa baadhi ya udhalimu aliouacha ama kunyang'anywa haki kulikofanyika kwa watu hao. Sasa sisi yatupasa kutumia hayo kama darasa la kujifunza ili makosa yasije yakarudiwa. Tutajifunza vizuri zaidi kwa kusema ukweli wote, wote kabisa hata kama itaonekana sehemu fulani Nyerere alidanganya kwa kinachosemekana ni maslahi ya taifa kwa wakati huo, tuseme hapa Nyerere alisema uongo, tuutafute ukweli. Hatuwezi kujifunza kwa uongo kwa vile tu ulisemwa au ulisababishwa na Nyerere. Nyerere naye alikuwa binadamu kusema uongo ni sehemu ya ubanadamu huo!
 
ndugu yangu junius unakuwa mwepesi sana wa kujudge mambo ya upande mmoja, hiyo statment au maelezo ni ya upande mmoja tu, wewe unaamini vipi kwamba huo ndio ukweli halisi.

Pili huyu bwana na kikundi chake inaonekana ni kikundi cha ukabila (HAYA TRIBE) na kwa asilimia kubwa kina ushirikiano mkubwa na nchi ya jirani Uganda kutokana na maelezo ya huyo bwana.

TATU hakuna kiongozi au state yoyote inayoweza kusimama bila ya damu kumwagika na watu kupata mateso makuu, hata Muhamadi alipokuwa anasimamisha dini watu wengi walikufa kwa sababu tu ya kutomwamini/kutomkubali, sasa iweje unashangaa ya Nyerere, lakini hata tukimwacha Nyerere je waliomfuata walishakuwa na mambo kama hayo ya Nyerere, ndugu yangu Junius hebu angalia vifo vya utata vya KOLIMBA, KOMBE,MALIMA,BALALI , sasa hapa utamshirikisha Nyerere, wewe umecomment hii issue kwa chuki za dhairi kwa Nyerere,

kuna mambo mengi tu yanatokea na kuna watu wengi tu wanashindwa hata sasa kukanyaga Tanzania japo Nyerere keshakufa, ajali ya Mwakyembe mpaka leo ni utata mtupu, kifo cha Wangwe mpaka leo ni utata mtupu,

NNe, sio Tanzania tu ndio watu walikuwa wapo detained hiyo nni system ya dunia nzima, Moi aliua (R.Auko na wengineo), Iddi Amini alikua, Bush, Putin, na viongozi almost wote katika hii dunia

Mwisho kabisa, ni kwamba usijudge vitu kwa chuki binafsi hata kama ni kweli huyo bwana aliteswa lakini alikuwa anadeserve kwa sababu alikuwa kinyume na misingi iliyokuwa inasimamishwa wakati ule, na sio yeye tu hata Kambona alishindwa ile misingi na akaamua kutimkia UK

Kolimba malima na kombe walikufa nyerere yupo hai. Na kolimba alipingana na nyerere kumpigia tafu mkapa na ndio kimoja ....
Malima nae ni stori ndefu humu jf zimeshaandikwa...kwa ufupi kutoka mrema ccm na kuingia nccr na kuzoa kundi kubwa la raia na pale malima kipenzi cha waislam alipotika ccm na kuonesha nia ya kugombea urais ilikuwa wazi ccm itapoteza kwani bila ya waislam ccm imekwisha ...hivyo yaliyotekea ni historia .
Kuhusu hizo shutuma dhidi ya mwalimu waulize kina kassela bantu na mapalala nini kiliwapata.
Hata kifo cha sokoine kina utata pia hivyo hii paper ni changamoto kui discuss kwa mapana na huu si wakati wa kuficha dhambi za watawala ikiwa walo pita au wa leo ..kujua tulipotoka ndio itatupa nguvu na weledi wa kuhakikisha yalofanywa hayarejewi tena
 
Ningewezaje kukosoa bila kusoma? Umejuaje tatizo ni lugha? Vipi ningeungana na mwandishi je ungesemaje?

Nimesoma kitabu chote tena na tena but shutuma nyingi ni uzushi tupu....
Shutuma zipi ni za uzushi? toa hoja.
Tatizo ni unabisha tu bila hoja ndio maana nina wasi wasi kuwa hujasoma.

Shutuma zipi ni za uzushi katika hiko kitabu ulichokisoma?
 
Nimekuuliza swali, jibu kwanza halafu uulize lako. Au swali langu limekuwa gumu kujibu? unaanza kuhororoja badala ya kujibu swali.
Teh teh teh an empty stomach can't understaand philosophy....

Nimeelewa fika swali lako na mantiki yake itawiana sana na jibu la swali nililokupa.....

Kama kuwepo au kutokuwepo enzi ya Nyerere ni kigezo kikubwa kwako ktk kupata picha ya changizi au mawazo yangu ndio maana nami nikakutandika swali kama je ulikuwepo enzi ya Mtume Muhammad??? Naomba jibu lako ambalo automatically litajibu lako....
 
Back
Top Bottom