Lowassa vs MwanaHalisi

Sina uhakika kama umefanya analysis vizuri. Basically unachosema ni kwamba Mwanahalisi haliwezi kukaa mwezi mmoja mzima bila kuandika ccm! Ni gazeti gani jengine linaweza kukaa mwezi mzima bila kuandika ccm?. Nimetumia jina CCM badala ya majina ya Edward Lowassa na Rostam Aziz uliyoandikwa kwa sababu moja kuu. Wanachokifanya mwanahilisi ni kuuabarisha umma kuhusu ccm with a human face!

Hii ni hoja dhaifu kidogo kwa kuwa hakuna namna inauzika hapa,hakuna namna kuwa unapotaka kuiongelea ccm basi ni lazima uwataje Lowasa au Rostam, hii ni kwa ukeli kuwa mambo yeenyewe yanayotajwa kuhusu Lowasa ni yale yaliotokea miaka 3 iliopita na nikichekesho kuwa CCM haina mambo mapya kwa miaka yote mitatu......au ndio fitna zenyewe.
 
Mwanahalisi ni msemeno inakata pande zote
Hiki ni kichekesho kikubwa sana hata siku moja mwanahalisi halijawai kuwa linakata pande zote..................hata siku moja hatujapewa ukweli na wananchi wanaambiwa kuwa adui wao ni rostam na dowans huku hawaambiwi ukweli kuwa si aggreko,iptl wala songas ambayo inauza umeme bei rahisi kuliko dowans...........na sababu ya dowans kuuza umeme bei rahisi ni kurithi mkataba wa richmond ambao swala la bei kuwa ndogo liliivutia serikali iliokuwa chini ya Lowasa kuwapatia tenda................kwa ujinga wetu tumekaa gizani miaka 3 mpaka wamarekani wamekuja na kununua mitambo hio hio na wanatuuzia umeme....ama kweli akili yetu imejaa ukungu.
 
Makada wa Magamba utawajua tu! Pinga na ccm wenzako, sisi twafurah coz mwanahalisi imebeba sauti zetu wanyonge then waandishi wake ni wazalendo. Kubenea yupo India New Delhi bt anatupa mambo kama kawa. Polen sana wafuasi wa mafisadi, najua mwaumia sana!
Hawezi kuacha kuwapa mambo kwa kuwa mambo yenyewe anatunga kwa kiwango ambacho anaweza hata kutuambia nyumbani kwako mkeo anafanya nini nawe usiku............yuko india ni hizo habari anazifanyia uchunguzi kubaini ukweli muda gani...anaweza kugeuza kuliita gazeti lake Hekaya za Mwanahalisi.
 
Ufisadi in the true meaning of the term haumaanishi kuwa lowasa ndio kiiiivyo, hebu tuwe wakweli jamani inamaana ufisadi wa nchi hii unawakilishwa na lowasa? Mbona hata sumaye alifikia hatua ya watu kumuona kama kinyesi 2000-2005? Ufisadi wake umeenda wapi? Inamaana kagoda,iptl,ttcl,loliondo gate,mchuchuma,epa,deep green,trc,uuzwaji wa nbc,mikataba mibovu,atcl,nssf-pspf scandals,sugar scandle,mishahara feki..................................zote hizi ni lowasa tuuuuuuuuuu? Anyway,kwa kuwa siasa zetu na uchambuzi wetu ni fuata mkumbo,haiko mbaya,lakini hebu tufanye tafakuri upya,mbona lowasa tu ndo zaidi na si kikwete,mkapa na wengine??? Uraisi kazi kwelikweli-just thinking aloud.



" fiat justitia.luat caelum"-let justice be done though heavens fall,
 
mwana halisi ni kijigazeti ambacho lengo lake ni kuchafua wa2,yaani ni gazeti la udaku ambalo linatakiwa lijivue gamba.Tuna mambo mengi kwenye hii nchi ya lowasa na rostam tumeyachoka.sijui wa2 wanalipendea nini lile gazeti limejaa unafiki sana.
Umetumwa na NAPE,GAMBA JIPYA HILI,HAYA WASALIMU MASAKI
 
Si ninyi mliokuwa mnapakaza Kubenea kanunuliwa? Kwa sisi tunaomfahamu kamanda Kubenea, tulisema mapema kuwa hizo ni siasa za Nape na wenzake ambao waliamini kuwa Kubenea hawezi kuwachapa. Yeye akasema mambo ni kwenda mbele akaanika waanzilishi wa CCJ na mafisadi wake.

Leo mnaanza kulalamika! Tena wewe ulioweka mada unasema kuwa kama ungekuwa wewe ungeshafungwa jela kwa kumshughulikia mbaya wako, mbona tayari mko jela ya kisiasa? Hajamtosheka na tindikali mliyomwagia ambayo imemsababisha miaka yote hii mitatu mtoto wa watu kutibiwa nje?

HaMUMUWEZI Kube, atawachapa wote - magamba na mafisadi wake.
Jamani kubenea aliwatambua waliomwagia tindikali na kesi ilipopamba moto hakwenda kutoa ushahidi baada ya jamaa kutoa ushahidi kuwa mkewe alikuwa akiliwa na kamarade Kube.
 
mwana halisi ni kijigazeti ambacho lengo lake ni kuchafua wa2,yaani ni gazeti la udaku ambalo linatakiwa lijivue gamba.Tuna mambo mengi kwenye hii nchi ya lowasa na rostam tumeyachoka.sijui wa2 wanalipendea nini lile gazeti limejaa unafiki sana.

Tukazane kusoma uhuru na mzalendo ili magamba yawe mazito kung'oka, gamba la mwanadamu linauma sana.
 
mwana halisi ni kijigazeti ambacho lengo lake ni kuchafua wa2,yaani ni gazeti la udaku ambalo linatakiwa lijivue gamba.Tuna mambo mengi kwenye hii nchi ya lowasa na rostam tumeyachoka.sijui wa2 wanalipendea nini lile gazeti limejaa unafiki sana.

Mtu akiwa anakujulisha kila mara kuwa unaibiwa mkeo, (na kweli mkeo huwa analala huko huko bila taarifa), na mwizi wako anamtaja na mbinu anazotumia kumchukua, utasema umechoka na habari zake au utachukuwa hatua?
 
mwanaharisi ni km gazeti la udaku mana lenyewe linaangalia mastar wa siasa km lowasa wamevaa nn wanakula nn ili hali kuna ishu chungu mzima za kuzungumzia cyo cri mnaboaaaaaaaaaaaaaaa!mbona mazuri yake hamyasemi km kweli mna lengo zuri na huyu baba.

Mbwa akilinda nyumba vizuri miaka kadhaa utamtunza na kumsifia vyema, lakini siku moja akipata kichaa akamrarua kolomeo mwanao wa chekechea, hutaangalia alifukuza wezi mara ngapi-utamtwanga risasi mara moja bila huruma.

Ni kweli EL ni mtendaji mzuri sana kuliko "Punda" mara mia, enzi zake za U-PM serikali ilionekana inafanya kazi! Lakini alipogundulika kuwa anapiga deal huku anaziba za wenzake, hapo ndipo watanzania walipochoka naye. Hivyo kelele za ufisadi lazima ataendelea kupigiwa tu mpaka kieleweke!

Huyu wa sasa ni sawa na Punda anayecharazwa bakora na mafisadi huku akielekezwa njia ya kupita, hana ajualo wala la kusimamia kama PM mwenye mamlaka kama ya Sokoine.
 
Nimeangalia kwa makini sana gazeti la Mwanahalisi kwa zaidi ya miaka mitatu mfululizo bila kukosa na leo nasema kwamba Mwanahalisi ni gazeti maalumu lililoundwa kwa ajili ya kumshughulikia Edward Lowasa na Rostam Aziz.Siku ambayo hawa watu wawili hawatakuwepo basi na gazeti letu kipenzi litakuwa limekufa pia.Leo niko tayari kupinga na mtu yeyote kuwa “KAMA MWANAHALISI LIKIKAA MWEZI MMOJA TU HALIJAANDIKA HABARI YA LOWASA BASI NITATOA KWA NILIOPINGA NAE SHILINGI MILIONI MOJA” japo ni hela nyingi kwangu ila nina uhakika haziwezi kunitoka kw kuwa Mwanahalisi wanamuota mchana na usiku Edward Lowasa……….Kwa kweli Lowasa ni mvumilivu sana ningekuwa mie ningekuwa nimeshafungwa jela kwa kumshughulikia mtu mbaya kabisa ,siwezi kuchezewa namna hii.:angry:

........Peter selukamba anena!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
kubenea anastaili pongez,unashangaa nini hapo? Wao wataandikwa hadi watubu kwa wizi wakutuibia laslimali zetu watanzania.
 
Kama ni kweli unalisoma mwanahalisi kwa nini useme ya Lowasa tu?kuna mambo mengine mengi ambayo mwanahalisi imeyaandika kwa umakini kabisa.
Kubenea alistahili tuzo ya uandishi wa habari na uongozi wa gazeti makini kabisa,hata kama mifumo inayoendesha tuzo hizo haitamfikiria sisi wasomaji makini wa mwanahalisi tushamtunuku
 
Hivi ukiwa mwanaccm ni lazima uunge mkono uovu wa viongozi?Sasa MWANAHALISI hapa limefanya kosa gani?Kuujulisha uma kwamba wanaoifisadi nchi ni hawa na wanaiba kwa njia hii na kutoa ushahidi uliojaa mantiki ni kosa?Kama gazeti linalotetea maslah ya nchi ni lazima liandike majina ya majambazi wa nchi na ndo hao wanaotajwa.Kibaya kipi wanafanya?Angalau ungewashauri hao majizi,walifungulie mashtaka gazeti kwamba linawachafua na kuwasingizia.Mbona hawafanyi hivyo?
Nadhani uko nyuma ya wakati au ulumbukeni wa kutokua na taarifa za wakati,kwa taarifa yako Rostam alishashinda kei dhidi ya mwanahalisi na wakaamuliwa kumlipa shilingi billioni tatu....mwanahalisi wakakata rufaa na sasa inangojewa mahakama ya rufaa.sasa unataka wafungue mara ngapi?
 
Nchimbi sikubaliani na mtazamo wako kwamba gazeti limeanzishwa kuzungumzia Mtu au watu kwani kifo cha gazeti la aina hiyo kingeshatokea katika kipindi kisichozidi mwaka (kifo cha gazeti ni pale linapokosa wasomaji). Gazeti la mwanahalisi limeweza kuweka katika maandishi matendo maovu ya watawala na washirika wao wakati ambapo hakuna aliyeamini kwamba tungeweza kuyasoma mambo hayo katika gazeti. Uwepo wa habari hizi kila wiki zikiwahusisha ulio wataja ni ishara kwamba wamejihusisha kwenye "madili" mengi yanayoendelea kuibuliwa. Kwa hali ilivyo lisipo sema mwanahalisi yapo yatakayo sema na kwa jinsi hali ilivyo bado uliowataja watakuwemo kwenye habari kwani kinachowafanya wawe habari ni mavitus waliyoyafanya kwa nia ya kujipatia mali.
Si kweli kuwa kuna mambo mengi ambayo yanaibuliwa kama ambavyo unataka kuonyesha hapa.....zaidi ya kuongelea upupu wa richmond na epa ambayo yameteeokea miaka 4 iliopita kuna nini jingine la ziada zaidi ya majungu.
 
hello r u from magamba family?
Jenga hoja zako na sio umbeya hapa.....mi mi nasema kuwa uwekezaji uliofanywa na Rostam ndani ya tanzania ni muhimu kuliko hata haya majungu mnayoleta hapa.....mna laana nyinyi watu.
1.Kaleta dowans ambayo iliwapa offer ya umeme wa chini kuliko kampuni yeyote binafsi inayozalisha umeme kusini mwa jangwa la sahara.
2.Kaleta gazeti la mwananchi ambalo ndio gazeti bora tanzania katika ujenzi wa demokrrasia.
3.Anadhamini ligi ya vodacom
4.anadhamini miss tanzania
5,Analipa kodi zaidi ya bilioni 40 kwa mwaka
6.Katoa ajira kwa zaidi ya watanzania elfu tatu
7.Kajenga madarasa na kugawa madawati kwa zaidi ya shule mia tano nchini
Labda ajala chakula na walemavu tu
 
Mwanahalisi ndugu yangu ni viwango vingine jombaaaaaaaaaaaaa, Kubenea ni kamanda ile mbaya,bisha uone, funika afunue, uliza umjue, bandika akubandue. Think 1000 times b4 writing magambalism. Mwana halisi ni Mvua za mafuriko nyie magamba mnaoishi mabondeni mtakoma.Kubeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee tuko pamoja kamanda
Hapa siwezi kujibu kwa kuwa hii ni mipasho ya taarabu ambayo sio fani yangu.
 
Back
Top Bottom