Antar bin Shaddad
JF-Expert Member
- Oct 11, 2010
- 202
- 101
nimesoma maoni ya wadau hapo juu ila hoja ya msingi ni kwamba EL sifa anazopewa na wapambe wake na na wale wanaomshabikia ni sifa ambazo hana kwa mfano kama ni mchapakazi amewahi kufanya nini katika muda wake wa utumishi?rekodi gani amewahi kuiweka inayoonekana,ukienda jimbo la Monduli ambalo amekuwa Mbunge wake kwa miaka 20 sasa bado linakabiliwa na matatizo chungu nzima,huduma duni za kijamii maji,zahanati,shule na mengineyo na mbaya zaidi kiwango cha umaskini kinatisha sasa hapo utajiuliza kipi tofauti alichofanya kusadia watu wake?jibu ni ziro! wengine wanasema anaweza kufanya maamuzi magumu lakini ukiangalia rekodi hakuna uamuzi wowote mgumu aliowahi kuufanya ndugu zangu tuwe wakweli Lowassa ni kiongozi mchovu tu kama walivyo wenzake wengi ndani ya CCM na kingine kibaya zaidi anautafuta Urais kwa mbinu zile zile za kimtandao zilizomwingiza madarakani JK ya ktumia magazeti,kuchafua wengine na na kutumiwa wapambe waliolipwa fedha mbinu zote hizo ni chafu na hazikubaliki katika demokrasia ya sasa.