navy boi
JF-Expert Member
- Mar 15, 2014
- 1,517
- 480
Wadau,
Nimetafakari sana na hakika nawahurumia sana baadhi ya watu. Wakati Lowasa akiwa CCM, walijipambanua kuwa chaguo lao ni Lowasa. Tena wakaunda mitandao mingi kama Friends of Lowasa, 4U Movement nk. Hawa piga ua walikuwa wanaamini kuwa mgombea Urais kwa tiketi ya CCM ni Lowasa hivyo wakawa wanatumia muda mwingi kumnadi.
Baada ya Lowasa kukatwa na CCM, watu hao walilia sana na kusaga meno. Hata hivyo, kilio chao kilitulia baada ya Lowasa kuhamia CHADEMA. Wengi wao ambao wapo kwenye mitandao ya kijamii wakaenda huko kama vile nyumbu. Huku wakitaraji kuwa Lowasa ndiye Rais ajaye
Kutokana na upepo kuvuma vibaya, huku Lowasa akikimbiwa na kundi kubwa la wapiga kura, watu hao ambao kwa sasa wanajipambanua kwa kundi la Ulipo Tupo watalia tena kwa mara nyingine. Tena kilio cha safari hii hakina wa kuwafuta machozi. Maana baada ya kipigo atakachopata Lowasa, kundi hilo watapoteana kabisa.
Siku zi nyingi ukweli huu utadhihiri
Magazeti ya tarehe 26 yote yatakuwa hivi
"Baada ya Lowasa kukatwa na ccm saiv akatwa na taifa zima"
Namuhurumia sana sumaye na kingunge