Debby the FEMINIST
Member
- May 4, 2020
- 32
- 37
Jeshi la Polisi Mkoa wa Lindi linamtafuta Saidi Haji Ngamila (30) mkazi wa Kijiji cha Barikiwa Wilaya ya Liwale kwa tuhuma za kumuua kwa kumkata na kitu chenye ncha kali na kutengenganisha kichwa na kiwiliwili na kisha kuchimba shimo na kumfukia Mwajuma Ally Lipala (49) Mkazi wa Kijiji cha Barikiwa.
Kwa mujibu wa maelezo ya mume wa marehemu Rashid Ally Mkumba (69) Aprili 14,2022 yeye pamoja na marehemu mkewe walienda kwenye shamba lao la mahindi na mihogo ambapo walikuwa na ujenzi wa kibanda kwa ajili ya kulinda wanyama waharibifu na wakati anaendelea na ujenzi ndipo marehemu aliaga kuwa anaenda kukata nyasi za kuezekea kibanda hicho lakini hakurudi tten, kisha akaenda kutoa taarifa kwa uongozi wa kijiji Ambapo juhudi za kumtafuta zilianza na ilipofika Aprili 16, 2022 mwili wake uligundulika ukiwa umefukiwa pembezoni mwa nyumba ya Saidi Haji Ngamila ambaye ni mtuhumiwa.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Lindi Mtatiro Kitinkwi amesema kuwa polisi kwa kushirikiana na ndugu wa marehemu walibaini Mundu ya kukatia nyasi aliyokuwa anaitumia marehemu siku aliyotoweka, viatu ambavyo wa mara ya mwisho alikuwa amevaa vilikuwa nyumbani kwa mtuhumiwa.
Aidha, Kamanda Kitinkwi ameongeza kuwa uchunguzi wa awali umebaini kuwa marehemu na mtuhumiwa walikuwa na mahusiano ya kimapenzi.
Kwa mujibu wa maelezo ya mume wa marehemu Rashid Ally Mkumba (69) Aprili 14,2022 yeye pamoja na marehemu mkewe walienda kwenye shamba lao la mahindi na mihogo ambapo walikuwa na ujenzi wa kibanda kwa ajili ya kulinda wanyama waharibifu na wakati anaendelea na ujenzi ndipo marehemu aliaga kuwa anaenda kukata nyasi za kuezekea kibanda hicho lakini hakurudi tten, kisha akaenda kutoa taarifa kwa uongozi wa kijiji Ambapo juhudi za kumtafuta zilianza na ilipofika Aprili 16, 2022 mwili wake uligundulika ukiwa umefukiwa pembezoni mwa nyumba ya Saidi Haji Ngamila ambaye ni mtuhumiwa.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Lindi Mtatiro Kitinkwi amesema kuwa polisi kwa kushirikiana na ndugu wa marehemu walibaini Mundu ya kukatia nyasi aliyokuwa anaitumia marehemu siku aliyotoweka, viatu ambavyo wa mara ya mwisho alikuwa amevaa vilikuwa nyumbani kwa mtuhumiwa.
Aidha, Kamanda Kitinkwi ameongeza kuwa uchunguzi wa awali umebaini kuwa marehemu na mtuhumiwa walikuwa na mahusiano ya kimapenzi.