Ngapi ngapi bosi
Huo mpira niliangalia dakika za mwisho mwisho, hiyo Taifa Stars ya Paulsen hamna lolote!!
Bora tungechukua under 17 na under 20 tuwaweke pamoja tunaongeza Nizzar na Samatta kwa maendeleo ya baadae.
Huyo Uhuru Selemani ameonesha uwezo mdogo saana kila mpira anapoteza au anapiga krosi fyongo!!! Hao mabeki sasa, yaani kuna beki wa kulia alipelekwa akarudishwa eti amekaa chini kama amesusa Mkongo akatia krosi! namkumbuka sana Maximo kipindi kile Stars ilikuwa inafungwa lakini inacheza pasi kama Arsenal!
Sisi kweli ni bichwa la mwendawazimu, wameshatunyoa sana sasa wataanza kututoa ngozi ya kipara!