Live ITV: Fahami Matsawili anazungumzia Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar na Utukufu Wake!

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,504
113,618
Wanabodi,

Leo ni kumbukumbu ya miaka 54 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar ya Mwaka 1964.

Katika Kipindi cha Kumepambuzuka ITV, mchambuzi wa mambo ya siasa, Fahami Matawili, anayazungumzia Mapinduzi hayo.

Fahami amesema utukufu wa Mapinduzi yale ni kuleta usawa kwa Wanzibari wote, kabla ya hapo, kulikuwa na matabaka, Wazungu, Waarabu, Wahindi, Washirazi na Wamatumbi, tabaka la Wamatumbi ambao ndio haswa na halisi wenye Zanzibar yao, ndio walikuwa dhalili, hawana Ardhi, hawana chochote, hawana lolote, wakati tabaka la Waarabu, ndio walikuwa na Ardhi yote, majumba, mashamba, na kila kitu. Kulikuwa na tabaka mbili kuu za mabwana na watwana. Mabwana walikuwa Waarabu, Wahindi, na Wazungu, watwana walikuwa Washirazi na tabaka la chini kabisa, la mwisho ni Wamatumbi. Hivyo utukufu wa Mapinduzi, yalileta usawa baina ya matabaka haya.

Fahami amezungumzia matunda ya Mapinduzi Matukufu ni muungano huu wetu adhimu, watwana wanamiliki Ardhi, watu wote wanapata huduma sawa za elimu, afya na fursa za maendeleo ni kwa wote, tukiwemo Watanzania bara kuwa huru kwenda Zanzibar na Wazanzibari na Wapemba wako huru kfanya shughuli zao popote ndani ya JMT.

NB. Fahami anaonekana ni Kijana mdogo, hivyo amekuja kuhadithia au kueleza kile alichoelezwa, kwa maoni yangu, media ya Tanzania, bado haijayatendea haki kabisa Mapinduzi ya Zanzibar kwa kutotoa fursa popote ya kujua nini kilitokea hiyo January 12, mwaka 1964. Karibu wote wanaozungungumzia Mapinduzi haya kwenye media, ni watu wa kuhadithiwa tuu!, kwa nini media zetu siku zote zinakumbatia watu wa kuhadithiwa tuu, wakati baadhi ya waasisi wa Mapinduzi haya Matukufu, wangalipo wapo?.

Kipindi Kimemalizika.
My Take
  1. Ushauri kwa Uongozi wa ITV, kwenye baadhi ya mada muhimu kama hii ya Mapinduzi ya Zanzibar, wawe wanatafuta watu ambao wako deep kwenye hizi issues na sio kutuletea wauza sura. Kila alichokisema Mchambuzi huyu, mtu yoyote angekisema, hivyo there is nothing new alichotuongezea Mchambuzi huyu.
  2. It is high time media zetu, tuwatafute waasisi wa Mapinduzi, tuzungumze nao kuhusu nini haswa kilitokeo Zanzibar ile Januari 12, 1964, maana stories ni nyingi na ziko tofauti tofauti, wakati wengine wakiyasifu Mapinduzi hadi kuyaita Matukufu, kuna wengine wanayalaani na kuyaita mauaji ya halaiki!, ukweli ni upi?.
  3. Media ziende ndani Zanzibar zikazungumze na Wazanzibari na kuonyesha matunda ya Mapinduzi, watu waonyeshwe jinsi Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, yalivyoleta utukufu kwa visiwa hivyo.
  4. Pamoja na utukufu wote wa Mapinduzi haya, pia yameacha baadhi ya makovu, its high time Zanzibar takes time to heal the wounded kwa kuunda peace and reconciliation commission, watu waponyeshe vidonda vyao na kuyafuta makovu ya Mapinduzi hayo.
  5. Mwisho, essence ya kitu chochote, inatokana na wakati husika, kwa mwaka ule 1964 kulikuwa na haja ya kufanyika mapinduzi yale, lakini leo miaka 54 baadae, jee sababu za mapinduzi yale bado zingalipo?, bado kuna sababu za serikali ya Zanzibar kuendelea kuitwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, au baada ya mapinduzi yale, sasa serikali ya Zanzibar ni serikali ya kidemokrasia iliyochaguliwa na watu na sio mapinduzi Daima.
Hitimisho.
Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, bado yamezingirwa na baadhi ya mazonge mazonge fulani ambayo, its high time mapinduzi haya yawe defined crystal clear.

Nawatakia mapunziko mema ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.
Paskali
 
Mkuu naona na wewe Magufuli amekukanyaga na kile kiatu alichochora Said Michael kisha akakuambia "Unawonaje viatu vyangu" na wewe ukamjibu "Viko safi sana tu"

Pascal Mayalla chaliiii chali kabisa. Umefungwa mdomo siku hizi umebaki kuleta tu updates za morning talks. Kweli Magu si wa mchezomchezo! Emb thubutu tena kuanzisha zile threads zako za eti Magufuli ni dikteta uone kama hujawekewa harsh tag ya kuhesabiwa siku.

Tutasoma [HASHTAG]#MayallaSiku49Sasa[/HASHTAG]....... teh teh teh Unawonaje viatu vyake!
 
nafikiei na Fahmi Mastawili,
niliwahi muona kariakoo,
kweli dunia haina hutuma, cjii kwanini CCM hawampi shavu kama wengine....
Ninhekuwa yeye ningesubiri procurement process nisepe zangu.....
 
Fahami amesema utukufu wa Mapinduzi yale ni kuleta usawa kwa Wanzibari wote, kabla ya hapo, kulikuwa na matabaka, Wazungu, Waarabu, Wahindi, Washirazi na Wamatumbi, tabaka la Wamatumbi ambao ndio haswa na halisi wenye Zanzibar yao, ndio walikuwa dhalili, hawana Ardhi, hawana chochote, hawana lolote, wakati tabaka la Waarabu, ndio walikuwa na Ardhi yote, majumba, mashamba, na kila kitu. Kulikuwa na tabaka mbili kuu za mabwana na watwana. Mabwana walikuwa Waarabu, Wahindi, na Wazungu, watwana walikuwa Washirazi na tabaka la chini kabisa, la mwisho ni Wamatumbi. Hivyo utukufu wa Mapinduzi, yalileta usawa baina ya matabaka haya.

P.
 
Wanabodi,

Leo ni kumbukumbu ya miaka 54 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar ya Mwaka 1964.

Katika Kipindi cha Kumepambuzuka ITV, mchambuzi wa mambo ya siasa, Fahami Matawili, anayazungumzia Mapinduzi hayo.

NB. Fahami anaonekana ni Kijana mdogo, hivyo amekuja kuhadithia au kueleza kile alichoelezwa, kwa maoni yangu, media ya Tanzania, bado haijayatendea haki kabisa Mapinduzi ya Zanzibar kwa kutotoa fursa popote ya kujua nini kilitokea hiyo January 12, mwaka 1964. Karibu wote wanaozungungumzia Mapinduzi haya kwenye media, ni watu wa kuhadithiwa tuu!, kwa nini media zetu siku zote zinakumbatia watu wa kuhadithiwa tuu, wakati baadhi ya waasisi wa Mapinduzi haya Matukufu, wangalipo wapo?.

Angalia ITV tunsikilize Fahami.

Paskali
Muhaya na mapinduzi ya Zanzibar wapi na wapi?!!.........tuwaache wazanzibar wajisemee wenyewe tafadhali!!
 
Fahami amezungumzia matunda ya Mapinduzi Matukufu ni muungano huu wetu adhimu, watwana wanamiliki Ardhi, watu wote wanapata huduma sawa za elimu, afya na fursa za maendeleo ni kwa wote, tukiwemo Watanzania bara kuwa huru kwenda Zanzibar na Wazanzibari na Wapemba wako huru kfanya shughuli zao popote ndani ya JMT.

P.
 
Fahami amezungumzia matunda ya Mapinduzi Matukufu ni muungano huu wetu adhimu, watwana wanamiliki Ardhi, watu wote wanapata huduma sawa za elimu, afya na fursa za maendeleo ni kwa wote, tukiwemo Watanzania bara kuwa huru kwenda Zanzibar na Wazanzibari na Wapemba wako huru kfanya shughuli zao popote ndani ya JMT.

P.
Mayalla hizo njaa zitakuua..
 
Sioni tatizo Fahami kuongelea mapinduz eti kisa hakuwepo.. Leo hii tunafundishwa mambo ya firt & second war na watu ambao hawakuyaona.. Ila wamesoma na wanafundisha watu wanawaelewa
 
Kipindi Kimemalizika.
My Take
  1. Ushauri kwa Uongozi wa ITV, kwenye baadhi ya mada muhimu kama hii ya Mapinduzi ya Zanzibar, wawe wanatafuta watu ambao wako deep kwenye hizi issues na sio kutuletea wauza sura. Kila alichokisema Mchambuzi huyu, mtu yoyote angekisema, hivyo there is nothing new alichotuongezea Mchambuzi huyu.
  2. It is high time media zetu, tuwatafute waasisi wa Mapinduzi, tuzungumze nao kuhusu nini haswa kilitokeo Zanzibar ile Januari 12, 1964, maana stories ni nyingi na ziko tofauti tofauti, wakati wengine wakiyasifu Mapinduzi hadi kuyaita Matukufu, kuna wengine wanayalaani na kuyaita mauaji ya halaiki!, ukweli ni upi?.
  3. Media ziende ndani Zanzibar zikazungumze na Wazanzibari na kuonyesha matunda ya Mapinduzi, watu waonyeshwe jinsi Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, yalivyoleta utukufu kwa visiwa hivyo.
  4. Pamoja na utukufu wote wa Mapinduzi haya, pia yameacha baadhi ya makovu, its high time Zanzibar takes time to heal the wounded kwa kuunda peace and reconciliation commission, watu waponyeshe vidonda vyao na kuyafuta makovu ya Mapinduzi hayo.
  5. Mwisho, essence ya kitu chochote, inatokana na wakati husika, kwa mwaka ule 1964 kulikuwa na haja ya kufanyika mapinduzi yale, lakini leo miaka 54 baadae, jee sababu za mapinduzi yale bado zingalipo?, bado kuna sababu za serikali ya Zanzibar kuendelea kuitwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, au baada ya mapinduzi yale, sasa serikali ya Zanzibar ni serikali ya kidemokrasia iliyochaguliwa na watu na sio mapinduzi Daima.
Hitimisho.
Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, bado yamezingirwa na baadhi ya mazonge mazonge fulani ambayo, its high time mapinduzi haya yawe defined crystal clear.

Nawatakia mapunziko mema ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.
Paskali
 
Wanabodi,

Leo ni kumbukumbu ya miaka 54 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar ya Mwaka 1964.

Katika Kipindi cha Kumepambuzuka ITV, mchambuzi wa mambo ya siasa, Fahami Matawili, anayazungumzia Mapinduzi hayo.

NB. Fahami anaonekana ni Kijana mdogo, hivyo amekuja kuhadithia au kueleza kile alichoelezwa, kwa maoni yangu, media ya Tanzania, bado haijayatendea haki kabisa Mapinduzi ya Zanzibar kwa kutotoa fursa popote ya kujua nini kilitokea hiyo January 12, mwaka 1964. Karibu wote wanaozungungumzia Mapinduzi haya kwenye media, ni watu wa kuhadithiwa tuu!, kwa nini media zetu siku zote zinakumbatia watu wa kuhadithiwa tuu, wakati baadhi ya waasisi wa Mapinduzi haya Matukufu, wangalipo wapo?.

Kipindi Kimemalizika.
My Take
  1. Ushauri kwa Uongozi wa ITV, kwenye baadhi ya mada muhimu kama hii ya Mapinduzi ya Zanzibar, wawe wanatafuta watu ambao wako deep kwenye hizi issues na sio kutuletea wauza sura. Kila alichokisema Mchambuzi huyu, mtu yoyote angekisema, hivyo there is nothing new alichotuongezea Mchambuzi huyu.
  2. It is high time media zetu, tuwatafute waasisi wa Mapinduzi, tuzungumze nao kuhusu nini haswa kilitokeo Zanzibar ile Januari 12, 1964, maana stories ni nyingi na ziko tofauti tofauti, wakati wengine wakiyasifu Mapinduzi hadi kuyaita Matukufu, kuna wengine wanayalaani na kuyaita mauaji ya halaiki!, ukweli ni upi?.
  3. Media ziende ndani Zanzibar zikazungumze na Wazanzibari na kuonyesha matunda ya Mapinduzi, watu waonyeshwe jinsi Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, yalivyoleta utukufu kwa visiwa hivyo.
  4. Pamoja na utukufu wote wa Mapinduzi haya, pia yameacha baadhi ya makovu, its high time Zanzibar takes time to heal the wounded kwa kuunda peace and reconciliation commission, watu waponyeshe vidonda vyao na kuyafuta makovu ya Mapinduzi hayo.
  5. Mwisho, essence ya kitu chochote, inatokana na wakati husika, kwa mwaka ule 1964 kulikuwa na haja ya kufanyika mapinduzi yale, lakini leo miaka 54 baadae, jee sababu za mapinduzi yale bado zingalipo?, bado kuna sababu za serikali ya Zanzibar kuendelea kuitwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, au baada ya mapinduzi yale, sasa serikali ya Zanzibar ni serikali ya kidemokrasia iliyochaguliwa na watu na sio mapinduzi Daima.
Hitimisho.
Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, bado yamezingirwa na baadhi ya mazonge mazonge fulani ambayo, its high time mapinduzi haya yawe defined crystal clear.

Nawatakia mapunziko mema ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.
Paskali
MapinduZi...ya zanzibar yanepotoshwa kwa...kuwaezi ambao hata hawakushiriki
Siku moja Mama Karume aliteleza akasema mapinduzi yanatokea mume wake alikua kajilalia wakamfuata kumtoroshea Mbweni dar ,yalivokamilika akaletwa akafanywa raia
 
Mapinduzi ya Zanzibar ni complicated subject kwa sababu historia yake imepotoshwa mno.

Siokupotoshwa tu bali kuna ukweli mchungu ambao kwa Mwafrika Mweusi unaweza kuuonea aibu kuusema wazi wazi labda kwa kuhofu ya kuonekana kibaraka.

Kwa mfano... Je, Mapinduzi yale ni halali au haramu? Jibu ni NDIYO na HAPANA... kwa upande mmoja ni halali na kwa upande mwingine ni haramu huku ikitegemea na perception yako.

Kwanini Mapinduzi ni HALALI? Ukweli usio shaka ni kwamba serikali ya ZNP & ZPPP ilikuwa ni serikali ya wachache, and possibly, kwa maslahi ya wachache!!!

Hivyo basi, ukiyachukulia mapinduzi katika sura ya uanaharakati huku akijikita kwenye masuala ya usawa, basi hapakuwa na budi zaidi ya utawala wa wachache kuondolewa madarakani!!!

Kwanini Mapinduzi yalikuwa HARAMU?

Huu ndio ukweli mchungu ambao wana-Historia ya Kiafrika hawataki kuusema kwa hofu ya kuonekana ni vibaraka wa Mwarabu! Ni ukweli ambao ukiusema mbele ya wanazi wa ASP huenda wakakutoa macho!!!

Kwa bahati mbaya sana Waarabu walishaonekana ni sehemu ya jamii ya Wazanzibari hasa ukizingatia Zanzibar yenyewe majority walikuwa ni wahamiaji na matokeo yake hapakuwa na mwenye uwezo wa kumwambia mwenzake "hapa wewe si kwako!"

Na kwa kuzingatia hayo, ndio maana chama cha Waarabu, ASP kilikuwa kinashiriki chaguzi kama vyama vingine hususani ASP haidhuru hata kama uchaguzi huo ulikuwa ni kwa matakwa ya Mkoloni Mwingereza!

Swali la kutafakari: Endapo kwenye uchaguzi wa 1963, ASP ingeshinda kwa viti vingi maradufu kiasi kwamba, hata kama ZNP na ZPPP wangeungana kama walivyokuwa wamefanya, bado wasingeweza kuipiku ASP... sasa je, baada ya ASP kuunda serikali ingefukuza Waarabu?

Now, endapo ASP ingewafukuza Waarabu, basi Mapinduzi ya Zanzibar ni HALALI kwa 100% with no this or that! Hiyo ingeonesha wazi kwamba wametimuwa watu ambao hawakuwa na haki ya kuwepo Zanzibar unless kama wangeendelea kuishi as foreigners.

Lakini endapo ASP wasingewafukuza Waarabu, basi ukweli mchungu ni kwamba, Mapinduzi ya Zanzibar ni HARAMU!!

Yangekuwa ni haramu kwa sababu kutowafukuza au kutowafanya waishi kama foreigners ina maana walishakubali kwamba Waarabu na wao wana haki ya uraia ndani ya Zanzibar.

Kwamba uchaguzi wa 1963 haukuwa huru na haki haiwezi kuwa hoja ya msingi ya kuhalalisha mapinduzi.

Haiwezi kuwa hoja ya msingi, kwa sababu, since then, vyama vya upinzani mara kwa mara vimekuwa vikilalamika kwamba chaguzi zinazoendelea tangu ujio wa vyama vingi ni chaguzi zisizo huru na haki!!

Hayo pia yalikuwa ndiyo malalamiko ya ASP... kwamba, palitokea magumashi kwenye uchaguzi uliofanya ZNP+ZPPP kuunda serikali!!

Sasa je, leo hii tunaweza kupindua serikali ya CCM kwa hoja kwamba uchaguzi haukuwa huru na haki na bado mapinduzi hayo yakaonekana ni HALALI?

Upotoshaji mwingine wa Mapinduzi ya Zanzibar ni kuhusu ushiriki. Kwa mfano, wafuasi wa ASP wanapewa credit nyingi kuliko wale wa Umma Part.

Hata hivyo, ukiisoma historia ya Zanzibar angalau 3 years kabla ya mapinduzi, utagundua ni Umma Part ndio walikuwa Wanamapinduzi wa kweli kuliko ASP.

Ushahidi wa haraka katika hili unaweza kuuona kwa Vijana wa Umma Part ambao walipelekwa Cuba na waliporudi hawakuwa na kingine vichwani mwao zaidi ya fikra za kimapinduzi.

Ni hawa Umma Part ndio waliwafanya US kupitia CIA kumshawishi Mwalimu Nyerere kwamba aungane na Zanzibar vinginevyo Zanzibar ingeisumbua sana Tanganyika huko mbeleni!!

USA sio kwamba walikuwa wanampenda sana Mwalimu au wallipenda sana Tanganyika bali walikuwa na hofu ya kuzaliwa kile kilichoitwa "Cuba ya Afrika".

Marekani iliwaona vijana machachari wa Umma Part wanaweza kuwa chachu ya kuanzishwa taifa (Zanzibar) la kikomunist ambalo lingekuwa gumu kulidhibiti kama ilivyokuwa ngumu kuidhibiti Cuba.

Na ndio maana, mara baada ya mapinduzi, Karume akawatoa Zanzibar wale wote aliowaona threat kama vile akina Abdulrahman Babu bila kumsahau Salim Ahmed Salimu!!

Kinyume chake, hakuna ushahidi kuonesha ASP au Vijana wa ASP waliwahi kupelekewa popote kuchukua mafunzo. Lakini ni hawa ASP, tena eti akina Karume ndio wanaonekana waliongoza mapinduzi!
 
Wanabodi,

Leo ni kumbukumbu ya miaka 54 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar ya Mwaka 1964.

Katika Kipindi cha Kumepambuzuka ITV, mchambuzi wa mambo ya siasa, Fahami Matawili, anayazungumzia Mapinduzi hayo.

NB. Fahami anaonekana ni Kijana mdogo, hivyo amekuja kuhadithia au kueleza kile alichoelezwa, kwa maoni yangu, media ya Tanzania, bado haijayatendea haki kabisa Mapinduzi ya Zanzibar kwa kutotoa fursa popote ya kujua nini kilitokea hiyo January 12, mwaka 1964. Karibu wote wanaozungungumzia Mapinduzi haya kwenye media, ni watu wa kuhadithiwa tuu!, kwa nini media zetu siku zote zinakumbatia watu wa kuhadithiwa tuu, wakati baadhi ya waasisi wa Mapinduzi haya Matukufu, wangalipo wapo?.

Kipindi Kimemalizika.
My Take
  1. Ushauri kwa Uongozi wa ITV, kwenye baadhi ya mada muhimu kama hii ya Mapinduzi ya Zanzibar, wawe wanatafuta watu ambao wako deep kwenye hizi issues na sio kutuletea wauza sura. Kila alichokisema Mchambuzi huyu, mtu yoyote angekisema, hivyo there is nothing new alichotuongezea Mchambuzi huyu.
  2. It is high time media zetu, tuwatafute waasisi wa Mapinduzi, tuzungumze nao kuhusu nini haswa kilitokeo Zanzibar ile Januari 12, 1964, maana stories ni nyingi na ziko tofauti tofauti, wakati wengine wakiyasifu Mapinduzi hadi kuyaita Matukufu, kuna wengine wanayalaani na kuyaita mauaji ya halaiki!, ukweli ni upi?.
  3. Media ziende ndani Zanzibar zikazungumze na Wazanzibari na kuonyesha matunda ya Mapinduzi, watu waonyeshwe jinsi Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, yalivyoleta utukufu kwa visiwa hivyo.
  4. Pamoja na utukufu wote wa Mapinduzi haya, pia yameacha baadhi ya makovu, its high time Zanzibar takes time to heal the wounded kwa kuunda peace and reconciliation commission, watu waponyeshe vidonda vyao na kuyafuta makovu ya Mapinduzi hayo.
  5. Mwisho, essence ya kitu chochote, inatokana na wakati husika, kwa mwaka ule 1964 kulikuwa na haja ya kufanyika mapinduzi yale, lakini leo miaka 54 baadae, jee sababu za mapinduzi yale bado zingalipo?, bado kuna sababu za serikali ya Zanzibar kuendelea kuitwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, au baada ya mapinduzi yale, sasa serikali ya Zanzibar ni serikali ya kidemokrasia iliyochaguliwa na watu na sio mapinduzi Daima.
Hitimisho.
Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, bado yamezingirwa na baadhi ya mazonge mazonge fulani ambayo, its high time mapinduzi haya yawe defined crystal clear.

Nawatakia mapunziko mema ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.
Paskali
Sio lazima awepo aliyekuwepo enzi hizo unaweza kuwa ni kijana ukafanya utafiti wa kina ukawa na vitu vingi kuliko aliyekuwepo enzi hizo kaka usiwapuuze watu ivo
 
Back
Top Bottom