Elections 2010 Lipumba: Nilidhani ni zamu yangu kuanguaka

Quinine

JF-Expert Member
Jul 26, 2010
21,271
47,271
MWENYEKITI wa Chama cha Wananchi (CUF), Ibrahim Lipumba, jana aliuacha hoi umati wa wanachama wake waliokuwa wamefurika katika mkutano wa kampeni wa chama hicho baada ya Mgombea Udiwani wa Vingunguti, Ally Omary, kutikisa jukwaa lake na kuliyumbisha.

Lipumba alipigwa na butwaa na kuuchekesha umati wa watu akidai kuwa alidhani naye zamu yake ya kuanguka imefika, hali ambayo iliwafanya wananchi waliokuwa wamefurika katika viwanja vya Buguruni Kisiwani kuangua vicheko.

“Enh, ndugu yangu umenishtua sana baada ya kunyanyuka na kupanda jukwaani kwani niliona linayumba nikapata hofu sana nikasema leo nadhani nami zamu yangu imefika,” alisema Lipumba.

Lipumba aliyasema hayo bila kutaja nani mwingine aliyeanguka wakati akiendelea na utambulisho wa wagombea wa nafasi ya Ubunge na Udiwani kwa tiketi ya chama hicho ambapo mkutano huo uliandaliwa na mgombea Ubunge Jimbo la Segerea, Ayoub Kimangale.
 
MWENYEKITI wa Chama cha Wananchi (CUF), Ibrahim Lipumba, jana aliuacha hoi umati wa wanachama wake waliokuwa wamefurika katika mkutano wa kampeni wa chama hicho baada ya Mgombea Udiwani wa Vingunguti, Ally Omary, kutikisa jukwaa lake na kuliyumbisha.

Lipumba alipigwa na butwaa na kuuchekesha umati wa watu akidai kuwa alidhani naye zamu yake ya kuanguka imefika, hali ambayo iliwafanya wananchi waliokuwa wamefurika katika viwanja vya Buguruni Kisiwani kuangua vicheko.

“Enh, ndugu yangu umenishtua sana baada ya kunyanyuka na kupanda jukwaani kwani niliona linayumba nikapata hofu sana nikasema leo nadhani nami zamu yangu imefika,” alisema Lipumba.

Lipumba aliyasema hayo bila kutaja nani mwingine aliyeanguka wakati akiendelea na utambulisho wa wagombea wa nafasi ya Ubunge na Udiwani kwa tiketi ya chama hicho ambapo mkutano huo uliandaliwa na mgombea Ubunge Jimbo la Segerea, Ayoub Kimangale.

.
Duh!! 90 + 15 +5 sawa sawa na asilimia ngapi ya nini?
 
Back
Top Bottom