Sio kuzeeka mkuu,hapo inategemeana na makubaliano kati ya NACTE na chuo husika,kama NACTE watawaruhusu hapo sawa,lakini ni vizuri watu wakajifunza kufuata utaratibu,kama utaratibu hauruhusu ndugu zangu tuanze kufuata utaratibu,SIKU HUWA NAAMINI HIZI NJIA ZA MKATO TUNAZOZITAFUTA NDIO ZINAZOZALISHA MAFISADI!
Mkuu sifikiri kama chuo cha serikali kitakuwa kinapromote njia za mkato. Utaratibu ulivo duniani kote hasa ni level ya chini katika chuo ni certificate (1 year) diploma (2 yrs) bachelor(3/4yrs), na sijawahi kusikia katika nchi yoyote yenye utaratibu usemao kuwa baada ya diploma, mtu akae nje mwaka mzima!!! Huku ni kurudishana nyuma! Ingekua vile vyuo vya kihindi vya kila course miezi sita kweli, lakini chuo cha serikali, kilichoweka ngazi hizo kisha eti ukae nje mwaka mzima!! Mwaka mzima ufanye nini? Sasa kwa mfumo huo wakukaa nje mwaka mzima ndo utazalisha MIFISADI hasa ilobobea!! Tz hakuna elimu, ndo maana watu hukimbilia India na malaysia!