Shedafa
JF-Expert Member
- May 21, 2008
- 802
- 173
Nakubaliana nawe kuwa ulikuwa na matatizo, kwa mawazo yangu muungano wowote ni kitu chema iwe ulianza vizuri au vibaya. Cha kufanya ilikuwa kurekebisha matatizo ya kuuweka sawa, ila hawa jamaa ukiwaangalia sicho wanachotaka. Wanataka kwanza nchi yao halafu waamue waungane na nani, kitu ambacho si kibaya ila wanaitaka toka kwa nani ndio shwali. Kwanini wasijaribu kujiondoa wenyewe waone kama kuna mtu atawashika mkono?Muungano ulikuwa na matatizo toka siku ya kwanza ya kuundwa kwake.
Utavunjika tu siku ccm itatoka madarakani, kama ccm itaendelea kuwepo tusitegeemee mabadiliko yoyote yale.
Ila mimi nina wasiwasi kuwa hawa jamaa kuna janja ndani yao, taarifa ya habari ya Channel Ten Mzee Mwinyi akiwa na umati mkubwa wanawakebehi wanaotaka kuvunja muungano. Kwani hawajuani!, si mchezo unaochezwa hapa? ili waendelee kuonewa huruma kama wanaonewa kweli na maisha yawe ya kuvyonza tu.
Hata kama unamdai mtu kitu, hapa achukue message ipi, hamtaki au mnataka?. Kama hawataki kweli wachukue ushauri waliopewa.