leopard mahona - mgombea wa cuf mwenye ushawishi atakayeibuka kidedea jimbo la igunga; umri; miaka 29. elimu; stashada ya biashara na uongozi. uzoefu wa kazi; mratibu wa shirika la world vision igunga kwa miaka 2. kazi ya sasa; mratibu wa shirika moja la kidini(halikupatikana) dar es salaam. asili yake na taarifa za wazazi; 1. mzaliwa wa igunga na amesoma na kukulia igunga.2. wazazi wote ni walimu wa shule za msingi tarafa ya nsimbo igunga. wasifu wa kisiasa; 1. mgombea pekee wa upinzani jimbo la igunga mwaka 2010 aliyefanikiwa kushinda vishawishi vya pesa na kukataa kuondoa jina lake na kumwachia rostam kama walivyofanya wenzake 12.2. alipata zaidi ya kura 11,000 katika uchaguzi huo lakini alishindwa kutokana na uwezo mdogo wa kifedha aliokuwa nao. kukubalika; anakubalika sana na watu wa rika zote katika jimbo la igunga. uwezo; anajiamini sana na uwezo mkubwa wa kujenga hoja thabiti. Ana uwezo wa kusimamia maamuzi yake na ya majukumu aliyotumwa.kwa nini atashinda; 1. ndiye mgombea pekee kijana, katika siasa za sasa za upinzani kijana anauzika mapema kuliko wazee.2. washindani wake kutoka ccm na chadema ni wazee na wataenda kulala bungeni jambo ambalo limewachosha wananchi kwa sasa.3. watu wa igunga wanahitaji mwakilishi watakayemtuma huku na kule na asichoke, washindani wake hawawezi mbio hizo kutokana na umri.4. alifanya kampeni jimbo zima mwaka jana 2010.5. anafahamika kwa wananchi kuliko wagombea wenzake.6. cuf imejipanga vizuri kumnadi na kuhakikisha anashinda jimbo la igunga.7. cuf ina nguvu kubwa igunga kuliko chadema na ccm9 ccm ina mtandao dhaifu kwani rostam alijijenga yeye kama yeye).naomba kuwasilisha.