marejesho
JF-Expert Member
- Jan 6, 2011
- 6,635
- 3,655
Wanajamvi leo nimefuata ushauri wenu,nikapanda Hood kutoka Morogoro kwenda Arusha!
Safari ilikuwa haina shida mpaka kufika kati ya Hedaru na Same!!Tukasikia mlio wa ajabu,hapa sidhani kama dereva alisikia maana aliendelea kuendesha gari mpaka abiria tulipoanza kulalamika!Harufu ya mpira unaoungua ilikuwa imetawala ndani ya gari!Dereva akasimama,tukashuka!Konda na Dereva wake wakagongagonga tairi baada ya muda tukaondoka!
Hatua chache mbele,harufu tena ya Moshi!!Ikabidi tushuke tena,mara moto ukawa unatoka kwenye tairi!!Dereva na konda wake wamefanikiwa kuuzima na safari yetu ndio imeishia hapa!
Dereva amepiga simu ofisini,msaada wa karibu ni kusubiri gari lililofika Moshi lirudi kuchukua abiria hapa tulipo!!
Sala zenu wanajamvi zinahitajika!!!
Safari ilikuwa haina shida mpaka kufika kati ya Hedaru na Same!!Tukasikia mlio wa ajabu,hapa sidhani kama dereva alisikia maana aliendelea kuendesha gari mpaka abiria tulipoanza kulalamika!Harufu ya mpira unaoungua ilikuwa imetawala ndani ya gari!Dereva akasimama,tukashuka!Konda na Dereva wake wakagongagonga tairi baada ya muda tukaondoka!
Hatua chache mbele,harufu tena ya Moshi!!Ikabidi tushuke tena,mara moto ukawa unatoka kwenye tairi!!Dereva na konda wake wamefanikiwa kuuzima na safari yetu ndio imeishia hapa!
Dereva amepiga simu ofisini,msaada wa karibu ni kusubiri gari lililofika Moshi lirudi kuchukua abiria hapa tulipo!!
Sala zenu wanajamvi zinahitajika!!!