Lazima mnilipe deni langu

Washawasha

JF-Expert Member
Aug 7, 2006
16,652
13,077
Mambo zenu waungwana nafikiri mko safi,
Ni hivi kuna jamaa alikuwa Tajiri sana lakini alikuwa na marafiki zake watatu ambao ni choka mbaya,basi cku 1 wakamuomba jamaa awakopeshe msingi wa kuuza ubuyu kila mmoja aliomba laki tatu,jamaa akawapa lkn masharti ni kwamba lazima walipe hata iweje,jamaa wakakubali masharti hayo.
Jamaa wakachukua zile fedha na kuanza kupiga mzigo,lkn haikuchukua muda Tajiri akadead kabla wale jamaa hawajamlipa.
Cku ya mazishi jamaa wakaenda mpaka makaburini,lkn kabla ya kuzikwa wadaiwa wakaomba wamlipe deni tajiri,jamaa wa kwanza akatoa 300,000/= akaweka ktk kaburi la tajiri wapili nae akafanya hivyo hivyo,sasa watatu akawa hana hela CA$H,ikabidi achukue zile laki 6 na kumuandikia Cheque ya laki tisa na kuingiza kaburini,Tajiri akawa amelipwa pesa zake kama walivyokubaliana.
 
Back
Top Bottom