Jemima Mrembo
JF-Expert Member
- Jul 19, 2021
- 2,791
- 8,008
TISS ilitakiwa kuwa mbali zaidi kabla hata mkataba haujasainiwa. Idara ya usalama ilitakiwa iwe na wasomi wabobezi wa sheria, wenye roho za uzalendo na wenye uwezo wa kumwambia rais hapana, hili haliwezekani kwa maslahi ya taifa.
Leo ili mtu awe afisa, haàngaliwi uwezo wake wa kiakili, ni mwendo wa vimemo tu kutoka kwa wakubwa wa chama na Serikali.
Idara imejawa na watu wenye pua zisizonusa, macho yasiyo ona wala masikio yasio sikia hatari yoyote kabla haitokea.
Hili suala la DP WORLD ni matokeo ya uajili mbovu wa watu wasio na sifa za kiwemo kwenye taasisi nyeti kama Tiss.
Leo idara inatumika kulinda maslahi ya watawala na sio maslahi ya taifa. Hili ni janga kubwa, nchi iko uchi.
Tunaomba rais aivunje idara hii isukwe upya, na sheria ile iliyosainiwa na Bwana Ben Mkapa ifanyiwe marekebisho makubwa, ili idara kisiwe chombo cha chama chochote na kisiingiliwe na yeyote.
Watanzania tunataka idara yenye meno kwa wote, watawala wakubwa, wa kati, wachini na sisi tusio na mbele wala miguu tupate same treatment kwa maslahi mapana ya taifa letu.
Haya mambo ya DP WORLD yasiweze kujirudia tena. Hii ni kashfa kubwa kwa taasisi nyeti na nchi nzima kwa ujumla wake
Leo ili mtu awe afisa, haàngaliwi uwezo wake wa kiakili, ni mwendo wa vimemo tu kutoka kwa wakubwa wa chama na Serikali.
Idara imejawa na watu wenye pua zisizonusa, macho yasiyo ona wala masikio yasio sikia hatari yoyote kabla haitokea.
Hili suala la DP WORLD ni matokeo ya uajili mbovu wa watu wasio na sifa za kiwemo kwenye taasisi nyeti kama Tiss.
Leo idara inatumika kulinda maslahi ya watawala na sio maslahi ya taifa. Hili ni janga kubwa, nchi iko uchi.
Tunaomba rais aivunje idara hii isukwe upya, na sheria ile iliyosainiwa na Bwana Ben Mkapa ifanyiwe marekebisho makubwa, ili idara kisiwe chombo cha chama chochote na kisiingiliwe na yeyote.
Watanzania tunataka idara yenye meno kwa wote, watawala wakubwa, wa kati, wachini na sisi tusio na mbele wala miguu tupate same treatment kwa maslahi mapana ya taifa letu.
Haya mambo ya DP WORLD yasiweze kujirudia tena. Hii ni kashfa kubwa kwa taasisi nyeti na nchi nzima kwa ujumla wake