Boflo
JF-Expert Member
- Jan 20, 2010
- 4,384
- 4,409
source: ladyjaydee.blogspot.comPosted by Jide at 5:52 AM 0 comments
KUNA KITU KILINIKWAZA SANA JUMAMOSI
Nilikuwa nimejiendea kwenye starehe zangu, wakati nimekaa counter akaja sijui nimuite mvulala au mwanaume. Akaaniita we mapanga shaa, nikamuuliza hilo ndio jina langu??
Akasema si nyie watu wa musoma wakurya ni wauaji.
Kwanza nilitamani nisiendelee kuongea nae tena ila baadae nilikata shauri nikaamua nizungumze nae tu nijue mwisho wake.
Nikamwambia ina maana wauaji wote duniani ni wakurya? Mbona hata Mbeya hakuna hao wakurya na watu walikuwa wanachunwa ngozi?.
Au wanaouua albino duniani wote ni wakurya, basi kama ni hivyo kutakuwa na wazungu, wachina, waarabu na wahindi wakurya pia... Maana hata huko kuna wauaji.
Maana mwaka jana tu kuna kesi ya wahindi walimkata kata mwenzao wakamfunga kwenye box.
Ni sawa na imani ya kuwa wahaya wote wanapenda ngono, wakati tukiangalia picha halisi nani asieshiriki hilo tendo. Au kwakuwa hatuwaoni?
Tabia ya mtu na roho kama ni mbaya mbaya tu haijalishi kabila gani.
Niwafahamishe tu pia kuwa mimi sio mkurya, na sio kila mtu anaetoka mkoa wa mara basi ni mkurya......Na wapo wakurya wastaarabu tu na wenye roho nzuri, sio kama wengi wanavyodhani.
Kuwa mkurya sio sababu ya kuitwa muuaji, tuheshimu makabila ya watu.
Wahukumiwe wale tu wabaya tena kwa matendo yao.
Mimi kabila langu ni Msizaki halina uhusiano kabisa na Wakurya, natokea wilaya ya Bunda mkoani Mara.
Wale mnaoniita mkurya nadhani mtakuwa mmepata jibu, na hata kama ningekuwa mkurya ningejivunia tu kwakuwa ndio lingekuwa kabila langu.
Na ndio maana huwa nakaa kimya hata nikiitwa mkurya, na watu wote wamekuwa wakifahamu hivyo kwa miaka nenda rudi, wala sioni kama ni tatizo...kwakuwa ndio kabila maarufu zaidi kwenye mkoa ninao toka.
Kwani kuwa mkurya ni dhambi jamani??
JayDee