kwikwi ya nondozzzzz za CBE ( by Michuzi)

Kottler Masoko

Senior Member
May 28, 2010
193
28
Ankal pole na kazi za kuelimisha jamii. Tunaomba utuwekee katika glob yetu ya jamii ili maombi yetu yasikike kwa wahusika, maana tunajua haakosi kutupia jicho humu.

Sisi tulikuwa wanafunzi wa chuo cha elimu ya biashara CBE Dar es Salaam
tumemaliza mwaka 2006 wengine mwaka 2007 na tulifaulu katika masomo tuliochukuwa Ajabu mpaka leo huu mwaka wa nne hatujapata vyeti vyetu muda tuliosoma ni miaka mitatu ni ajabu muda wa kusubiri vyeti unazidi muda wa masomo na kila kukicha ni sababu tuu, mara printer hajapatikana, mara vinachapishwa nje ya nchi ili mradi siku zinakwenda ikiwa na ada tulishalipa tukamaliza tena kwa wakati.

Hii inatupa shida hata tunapoomba kazi wanakuwa na wasiwasi kama kweli tulisoma hapo maana tunatumia transcript ambazo wengine hawazikubali na hata iwapo unatakiwa upande cheo mwajiri anasema lete cheti chako kama huna unabaki palepale ulivoajiriwa na cheti cha awali.

Wadau wa enzi CBE
 
Back
Top Bottom