Mkono Mmoja
JF-Expert Member
- Jan 26, 2019
- 1,932
- 4,086
Salam
Husikeni na kichwa cha habari hapo juu , Wakazi na watumiaji wa barabara kuu itokayo kimara kuelekea bonyokwa na vitongoji vya karibu kama Baa mpya,Mavurunza,Kwa Mringo na Golani wamekuwa wakisumbuka kwa muda mrefu sasa juu ya kero ya usafiri wa hii barabara.
Kiuhalisia urefu wa barabara kuu ya Kimara - Bonyokwa haizidi kilometa 7 na hivyo vitongoji vingine kuelekea kimara havizidi km 4 ila imekuwa ni kero sana hususani nyakati za usiku kutokana na madereva wa bajaji na gari ndogo aina ya Noah kutoza nauli kutoka 1000 mpaka 2000 kwa kila abiria.
Hii barabara imekuwa ikinadiwa kila leo kuwa ipo kwenye mpango wa serikali wa kuhakikisha kuwa inawekwa lami lakini zimekuwa ni ahadi hewa. Kupanda kwa gharama za usafiri nyakati za usiku na nyakati za mvua imekuwa ni mzigo kwa raia kwa wanaofanya kazi katikati ya jiji hulazimika kutumia zaidi ya shilingi 6000 kwa ajili ya usafiri kila siku.
Wito wangu kwa serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Mheshimiwa Rais Daktari Mama Samia Suluhu Hassani ifanikishe kuitengeneza hii barabara ili kutoa fursa kwa wamiliki wa daladala kuleta mabasi yao ili kuwapunguzia wananchi gharama kubwa za usafiri zinazochangiwa na ubovu wa hii barabara.
Hii ni barabara ya kimkakati inayorahisisha kupunguza msongamano wa magari ktk barabara ya morogoro kwa kutoa wepesi wa watukufika tabata segerea,kinyerezi,buguruni na ukonga pasi na kupitia ubungo.
Kipindi cha uchaguzi kinakaribia na kero kubwa ya wananchi wa kimara ni ubovu wa hii barabara.
Mbunge wa hili jimbo ndio hana habari kabisa kuhusu hii barabara, pia tunakutaka Waziri wa ujenzi kupitia TANROADS muhakikishe hii barabara inawekwa lami.
Husikeni na kichwa cha habari hapo juu , Wakazi na watumiaji wa barabara kuu itokayo kimara kuelekea bonyokwa na vitongoji vya karibu kama Baa mpya,Mavurunza,Kwa Mringo na Golani wamekuwa wakisumbuka kwa muda mrefu sasa juu ya kero ya usafiri wa hii barabara.
Kiuhalisia urefu wa barabara kuu ya Kimara - Bonyokwa haizidi kilometa 7 na hivyo vitongoji vingine kuelekea kimara havizidi km 4 ila imekuwa ni kero sana hususani nyakati za usiku kutokana na madereva wa bajaji na gari ndogo aina ya Noah kutoza nauli kutoka 1000 mpaka 2000 kwa kila abiria.
Hii barabara imekuwa ikinadiwa kila leo kuwa ipo kwenye mpango wa serikali wa kuhakikisha kuwa inawekwa lami lakini zimekuwa ni ahadi hewa. Kupanda kwa gharama za usafiri nyakati za usiku na nyakati za mvua imekuwa ni mzigo kwa raia kwa wanaofanya kazi katikati ya jiji hulazimika kutumia zaidi ya shilingi 6000 kwa ajili ya usafiri kila siku.
Wito wangu kwa serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Mheshimiwa Rais Daktari Mama Samia Suluhu Hassani ifanikishe kuitengeneza hii barabara ili kutoa fursa kwa wamiliki wa daladala kuleta mabasi yao ili kuwapunguzia wananchi gharama kubwa za usafiri zinazochangiwa na ubovu wa hii barabara.
Hii ni barabara ya kimkakati inayorahisisha kupunguza msongamano wa magari ktk barabara ya morogoro kwa kutoa wepesi wa watukufika tabata segerea,kinyerezi,buguruni na ukonga pasi na kupitia ubungo.
Kipindi cha uchaguzi kinakaribia na kero kubwa ya wananchi wa kimara ni ubovu wa hii barabara.
Mbunge wa hili jimbo ndio hana habari kabisa kuhusu hii barabara, pia tunakutaka Waziri wa ujenzi kupitia TANROADS muhakikishe hii barabara inawekwa lami.