Kwanini Tanzania haijavunja Uhusiano na Gadaffi?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,476
39,995
Wakati wa Nyerere Tanzania haikuwa na utata katika masuala ya siasa za Kimataifa; tulitambua POLISARIO na PLO kama vyama vilivyokuwa vinawakilisha maslahi ya watu wa Western Sahara na Palestina. Hatukuona shida kutambua na kutoa ushirikiano kwa vyama vya ANC na vingine vya haarakati za ukombozi wa Kusini mwa Afrika. Tulitambua dhana ya utu wa mtu na kukataa kuhusiana na tawala dhalimu. Ndio sababu ya kuwa tayari kujitoa Commonwealth kama RSA ingeruhusiwa kuingizwa ndani.

Wakati huo Tanzania ilikuwa kiongozi katika masuala ya haki za watu na kukataa ukandamizaji wa watawala dhidi ya watu wao. Watanzania wenyewe walitembea kifua mbali kwani kuitwa Mtanzania ilikuwa inaendana kabisa na kuwa "mpigania haki za wanyonge". Ukisema "Tanzania" ulikuwa unazungumzia sauti ya Afrika katika masuala ya Kimataifa. Hakutukuwa na ukaribu sana na nchi za Kimagharibi kiasi cha kushindwa kuwambia ukweli. (kesho inshallah, nitawawekea barua ya Nyerere kwa JFK kuhusu Angola/Mozambique na RSA).

Leo hii Tanzania hii ya Mwalimu imekatwa mkia na haina tena uwezo wa kusimama na kunyoshea kidole mtu yeyote. Haiwezi kuwanyoshea kidole Wamarekani wala Waingereza (Nyerere alivunja hata uhusiano na Waingereza! huku akimtimua Padre mmoja kutoka nchini!). Tanzania hii ya sasa haina uwezo hata wa kujenga hoja ya kimaadili dhidi ya tawala dhalimu. Matokeo yake ni kuwa Tanzania ndugu zangu sasa inafuata. Ndugu zangu, Tanzania inafuata nchi za Senegal, Liberia, Qatar, n.k linapokuja suala la Libya.

Tanzania ambayo ilikuwa na sauti ya kukataa viongozi wake wamepewa misaada ya magari kiasi kwamba hawawezi tena kuzungumza na wanabakia kumung'unya maneno. Maskini Tanzania hii. Najiuliza mpaka nani atambue Baraza la Mpito la Waasi kule Libya ndio Tanzania ifuate? Kwanini nchi kama Liberia, Botswana na Senegal zimeweza kuvunja mahusiano na Gaddafi lakini nchi kongwe kama Tanzania imeshindwa hata kuonesha kuwatambua uwepo wao?

Yawezekana kweli viongozi wetu wamekuwa so compromised kiasi kwamba wema umekuwa uovu na uovu umekuwa wema? Ni kweli Taifa letu limenunuliwa hadi sauti yake - ukiondolewa kununuliwa kwa wanyama na raslimali zake? Kwanini sauti za Upinzani nchini zinashindwa kupiga kelele kutaka serikali ivunje uhusiano na serikali ya LIbya? Rais wa Senegal ambaye alikuwa ni mpinzani kwa muda mrefu alielewa hili na hakuonesha utata tena yeye alienda kutangazia msimamo wake ndani ya Libya yenyewe (kule Benghazi), kina Kikwete wanashindwa nini? Wanaogopa nini? Tanzania haina tena ile moral standing ya kukemea udhalimu?
 
Thubutu... Just a week ago The Libyan Ambassador visited The President @ the State House...

Tulichukua Pesa za Mikopo ya Kujenga Misikiti we need to pay them back first...
 
Huwezi kuukata mkono unaokulisha! U-matonya wetu kama taifa hauna mipaka wala miko. As a result we've sold our souls ili mradi ni muda wetu wa kula. tragedy!
 
Mi nafikiri wewe ndo wa kulaumiwa sio Tanzania, wewe mwenyewe umesema wale ni" waasi wa libya" na huo ndio ukweli, sasa ni vipi tz na heshima zake zote hizi ilizonazo iwatambue waasi? hilo haliwezekani ndugu yangu. Wale ni waasi wa libya, na nchi zote zilizowatambua ni nchi ambazo zimefuata karoti kujipendekeza kwa marekani na nchi za magharibi, hamna lolote zaidi ya hapo. Hatuwezi kuwatambua waasi, kwa kuwa kwa kufanya hivyo ni kukaribisha uasi nchini kwetu, ile ni njia haramu na ni vibaraka tu hawana lolote wale.
 
Kuna" faida" ambazo haziko wazi ambazoTanzania imefaidika kutoka kwa Gadafi, "faida" hizo ndizo zinatufanya tuone "aibu" kukata uhusiano na Gadafi ijapo Watanzania wengi wameshasahau jinsi gani Gadafi alikuwa adui wetu wa vita vya Kagerai.
Nafikiri viongozi wengi wa Afrika wanaamini kuwa Gadafi atashinda tu vita hivyo, na kwa sababu hiyo, mataifa mengi ya Afrika yanaogopa huenda endapo Gadafi atashinda basi Gadafi anaweza aka wasapoti waasi na kuweza kupindua serikalihusika na huenda serikali yetu ikawa ktk woga huo. Gadafi alikuwa ni tishio, ka sponser waasi wengi sana
 
Mi nafikiri wewe ndo wa kulaumiwa sio Tanzania, wewe mwenyewe umesema wale ni" waasi wa libya" na huo ndio ukweli, sasa ni vipi tz na heshima zake zote hizi ilizonazo iwatambue waasi? hilo haliwezekani ndugu yangu. Wale ni waasi wa libya, na nchi zote zilizowatambua ni nchi ambazo zimefuata karoti kujipendekeza kwa marekani na nchi za magharibi, hamna lolote zaidi ya hapo. Hatuwezi kuwatambua waasi, kwa kuwa kwa kufanya hivyo ni kukaribisha uasi nchini kwetu, ile ni njia haramu na ni vibaraka tu hawana lolote wale.

Hawa ndio wanaonufaika na ujenzi wa misikiti alioufanya Gaddafi hapa Tanzania badala ya kuwajengea shule na hospital. Kiwete ni rais mdini kwahiyo hawezi kumtosa mwislamu mwenzake Gaddafi. huu ndio ukweli wenyewe.
 
Mwalimu alisema, nchi ikiendeshwa kwa kutegemea misaada toka nchi za nje, itakosa pia uhuru wa kuamua mambo yake. Na mwishowe itakua inaamuliwa mambo yake na nchi za nje.

That's what is happening katika TZ yetu sasa. Tumekua matonya kiasa kwamba hadi wabunge walishawahi kusema (wakati wa ujio wa Kichaka Jr.) "kua maandamano ya kupinga ujio wake yataonyesha picha mbaya, ivyo wajerumani, waingereza n.k. wataogopa kutuletea misaada!!!" Haya ni mawazo ya wabunge!!! Yaani kupenda misaada kunawafanya wasiwe huru katika kutoa mawazo na maoni yao!!
 
Mi nafikiri wewe ndo wa kulaumiwa sio Tanzania, wewe mwenyewe umesema wale ni" waasi wa libya" na huo ndio ukweli, sasa ni vipi tz na heshima zake zote hizi ilizonazo iwatambue waasi? hilo haliwezekani ndugu yangu. Wale ni waasi wa libya, na nchi zote zilizowatambua ni nchi ambazo zimefuata karoti kujipendekeza kwa marekani na nchi za magharibi, hamna lolote zaidi ya hapo. Hatuwezi kuwatambua waasi, kwa kuwa kwa kufanya hivyo ni kukaribisha uasi nchini kwetu, ile ni njia haramu na ni vibaraka tu hawana lolote wale.

Kwanini tulitambua POlisario na ANC?
 
Sijui kama status imebadilika, ila Nelson Mandela alichukuwa kiti cha urais kama a' convicted criminal' na ANC was branded a terrorist organisation. Na kama status haijabilika basi Mzee Mandela atakuwa a 'retired-convicted crimanal? mental!
 
Kulikuwa na thread kama hii wiki iliyopita (https://www.jamiiforums.com/interna...ll-tanzania-soon-recognize-libyan-rebels.html) ambapo nilisema tatizo letu kubwa hatujui hata Tanzania's foreign policy ni ipi. Membe alipoulizwa juu ya hili anajichanganya sana. Hata kama tunayo foreign policy itakuwa inafuata upepo. That's why I am not surprised what Kikwete and his Co did in South Africa in his recent visit. Msikilize kwenye hii video kuanzia dakika ya 4.5 mpaka ya 8. Anaongelea sera ya defense of freedom, human rights, equality and democracy. Sasa compare na Kikwete kwenda South Africa juzi ku-abolish SADC's Tribunal for human rights. How come one hand you say that one of the pillars of our foreign policy ni protection of human rights, whilst on the hand you goes on to abolish a human rights tribunal? Kwa issue ya Libya sidhani kama tukp bold enough. If we were bold enough we should have expressed our position from the beginning badala ya kusubiri mpaka sasa.

 
Last edited by a moderator:
Mwanakijiji, kweli unachekesha sana unataka Tanzania wavunje uhusiano na Libra iwatambue waasi wa Libra Kwani Gaddaf kafanyaje mpaka uvunje uhusiano nae, yaani nchi yoyote Marekani akiichukia basi tuvunje uhusiano nao
 
Hawa ndio wanaonufaika na ujenzi wa misikiti alioufanya Gaddafi hapa Tanzania badala ya kuwajengea shule na hospital. Kiwete ni rais mdini kwahiyo hawezi kumtosa mwislamu mwenzake Gaddafi. huu ndio ukweli wenyewe.
Kumbe waasi wa Libya ni wakristo tulikuwa atufahamu
 
Duh, mkulima kule kiembeni hawezi kamwe kumfahamu mheshimiwa Waziri Membe, concensus, investors, disadvantage, handle at a time, accomodate n.k. kweli haya maneno hayana mukabala wake katika kiswahili? Jamani, huu utumwa wa kiakili utakwisha lini?
 
Sina la kusema zaidi!

gaddafi_pix.jpg


By DANIEL MSANGYA in DODOMAPosted Saturday, March 5 2011 at 15:28Embattled Libyan leader Muammar Gaddafi, may be a worldwide villain today, but his legacy looms large in Tanzania where he is getting backing from people whose lives he has touched in some way or the other.

Were the eccentric leader to be driven out of power by a popular public revolt currently sweeping his oil-rich country, he would not be without Tanzanian sympathisers, who hail his support for the needy as testimony of his good leadership.

The collapse of the regime in Tripoli would also likely raise apprehension over several projects, worth billions of shillings, that Gaddafi had promised to implement in several African countries including Tanzania.

The Libyan leader, for instance, had committed to establish an ultra-modern complex, Mosque and College in Dar es Salaam after a successful example in Dodoma. A foundation stone for the Dar es Salaam centre was laid last year by retired President Ali Hassan Mwinyi.

One of the believers in Gaddafi's leadership is the Chief Sheikh for Dodoma Region, Mustapha Rajab Shabaan, who also doubles as the manager of the $4,081,632.7 million Gaddafi Education Centre and Mosque located in the city.

The imposing 3,000 capacity facility, inaugurated last year by President Jakaya Kikwete, is a picturesque architecture; the only one of its kind in the country and only rivalling the one Col Gaddafi also built and opened in Uganda over a year ago.

The Dodoma mosque and centre is thus a constant reminder of the hitherto great efforts that went into anything that Libya, and Gaddafi in particular, undertook to roll out either in his endeavour to serve humanity or seek loyalty far and wide.

Tanzania's Citizen on Saturday sought to establish the fate of activities at the Dodoma centre and the proposed Dar es Salaam complex in case the rebels succeeded in bringing to an end his 42 years of uninterrupted reign.




Humanity
Africa Review - Gaddafi
 
Kama sijakosea wakati wa Mwalimu tulikuwa upande wa Arafat dhidi ya Israel!? Maajabu sana na pia tulisimamia vita vya Kabila mpaka akamuondoa Mubutu wakati wa Mkapa hivi Kabila hakuwa muhasi kwa mubutu?!

Anyway swala la qadhaffi ni la UN nashangaa sisi kama wanachama wa UN bado hatujamkana Qadhaffi adharani!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom