Kwanini nimuamini Mtu aliyeishi miaka 600 Baada ya Kufa Kwa Yesu, Niache Kuwaamini Mathayo, Marko, Luka na Yohana walioishi nyakati ya Yesu Kristo?

Huyo Aliyeishi Miaka 600 baadae angalau ameongea Vinavoeleweka Kuhusu Yesu Akina Marko Na Luka Wamedanganya sana Hata Ukisoma Wamepishana masimulizi Yao Mfano Kuhusu vazi la Yesu Wakati Anashurutishwa Kuna Mmoja Anasema Alikuwa Kavaa Vazi la Zambarau Mwengine Kasema Rangi Nyingine Sasa Unajiuliza Hivi Ni Kweli walikuwepo Au Ni Matapeli Tu waliotuzidi Akili
Ni vyema ukaleta uthibitisho wa utofauti huo ili wanajukwaa wasidhani kuwa unabwabwaja pekee.

Leta utofauti huo ili tuujadiri.
 
Am not Muslimu Mkuu!
Japo Kwa kujibu..
Quran Imebadilisha sana na imepitia Mabadiliko mpaka kufikia kwa Msahafu wa Uthmani (The standard of quran)..
Hakuna muislam anakubaliana hili.kwa kutafiti ama kuambiwa kama hivi.
But all in all
Hakuna Mwandishi hata mmoja wa Biblia Ambaye ni Authentic sources au Trur sources Vivo hivyo Quran
hakuna mkristo mwenye mashaka ama anayebisha jambo hili,linajulikana kabisa,
Sababu hata paulo si ktk wanafunzi 12 wa Yesu.
Na ndiye mtu wa kwanza kukusanya wakristo.
 
Injili ni nini? Maana kitabu chenu kinaiongelea injili ambayo hatuijui wala hatujawahi kuiona? Kama Quran inajitegemea Hadith za nini?

Wewe umejuaje kwamba the furthest mosque ni msikiti wa El-aqsa bila msaada wa Hadith na tafsir? Quran 17:1 haina context mpaka ukimbilie kwenye Hadith na tafsir 😊😊,kitabu chenu kina mashimo kibao yanayoonyesha upungufu wake.
😄😄😄mkuu taratibu.

Ila usijali nadhani injili OG anayo atakupa.
 
Mohamed alimuona Yesu? Quran ina mix mafaili kwamba mama yake Yesu alikua dada wa Aron msaidizi wa Musa. Quran haisemi Yesu alizaliwa wapi,alitokea kabila gani la Israel. Kwenye Quran haijulikani Yesu alikua na wanafunzi wangapi,wala majina yao .
Ukiishi miaka 600 baada ya tukio ni ngumu kuweza kufahamu kilicho tokea.

na ndio maana kuna hizo contradictions.
 
Habari wana theolojia.

Mathayo, Marko, Luka na Yohana hawa walikuwa ni mashahidi wa macho waliopata kumuona na kumsikia Yesu Kristo, hata baadaye wakapata msukumo kupitia roho mtakatifu kuyaandika yale ambayo kristo alokuwa akiyasema....

Huwa sipatagi kuelewa kwanini kundi fulani la watu wamejikita kumuamini na kuyaamini mafundisho potofu kumhusu Yesu Kristo yaliyoasisiwa na mtu aliyekuja kuishi miaka 600 baada ya kufa Yesu Kristo.

Mathayo, Marko, Luka na Yohana wote wanadai kuwa Kristo Yesu alikuwa ni MUNGU, jamaa anakuja miaka 600 baadaye anasema haikuwa hivyo. Mbaya zaidi ili kuhalalisha kauli yake akasingizia kuwa ameambiwa na Mungu.

Na licha ya hayo yote watu wakapata kumuamini.

Dah! sijui ipo sababu ipi kwakweli?
Karibu saa tisa, Yesu akapaza sauti, akisema: “Eli, Eli, lama sabakthani?” yaani, “Mungu wangu, Mungu wangu, kwa nini umeniacha?”

Mathayo 27:46
 
Quran pia Muhammad alizaliwa wapi, alitokea ktk kijiji gn, Quran hatujui Muhammad alikuwa na wanafunzi wangapi, wala majina yao. Ni kweli kabisa kwa Quran haijataja hata majina ya wake na watoto wake.
Ni ngumu sana kwasababu hayo mambo kuweza kuandikwa na kutiwa ktk kumbukumbu ktk miaka hiyo ilihitaji Mungu aingilie kati na uweza wake kwa manufaa ya kizazi kijacho na cha baadaye.
 
Naam ni sahihi kabisa. Kwa Quran si kitabu cha historia, si kitabu cha kisayansi, si kitabu cha hesabati au fani yyt. Bali kimetoa tu muhtasari wa historia, hisabati, sayansi, biology nk kwa muhtasari au mwongozo. Ili wewe tunapokuja kufanya utafiti ukusaidie ili usije kukupotosha.
Hebu taja usayansi wowote katika !Qurani ambao kwako una-make sense.?
 
Yesu ajakabidhiwa kitabu. Hamuelewi ata historia ya bibilia. Mnadhani Mungu ni ndogo kama kitabu. Vitabu vipo vingi sana ila vilikosa authenticity. Sasa moody ndio akakwapua huko mastory ya uongo. Eti aje baadae karne 6 mbele eti kaja kusahihisha!? Inaingia akilini. Acheni ujuaji , dini yenu ni false.
Maalim tujadili kwa kuheshomu.

Ujumbe wa muda, ibrahim, yesu, adam ni mmoja.

Muhamad hakuja kutengua torati na vitabu vingine. Bali kukamikisha.

Jiulize kwann mtumie biblia ambayo ni mkusanyiko wa maneno ya waandishi.

Kwanini hamtumii injili.

Ukiitumia utaona iko sawa na quran.

Ninyi mnafata disimformation kutoka kwa hasa paulo.

Ukisoma bible mayahudi wakimpinga paulo wakisema anakufuru na kumtukana Mungu ninyi ni nani Hadi mumfate
 
Injili ni nini? Maana kitabu chenu kinaiongelea injili ambayo hatuijui wala hatujawahi kuiona? Kama Quran inajitegemea Hadith za nini?

Wewe umejuaje kwamba the furthest mosque ni msikiti wa El-aqsa bila msaada wa Hadith na tafsir? Quran 17:1 haina context mpaka ukimbilie kwenye Hadith na tafsir 😊😊,kitabu chenu kina mashimo kibao yanayoonyesha upungufu wake.
Naam hadithi zipo ambazo hazijachakachuliwa. Lkn kuna ayah Chungu mzima zinazojitosheleza kuhusu masjid aqsa.

Kuhusu injili na kwakuwa uko muwazi sana na unathitisha hujawaji kuiona injili.

Nikupe ushauri wa bure ndugu yangu

Endelea kuwa na moyo huo ulio huru.

kwani Quran ni injili ile ya yesu uliyokamilishwa.

Kumbuka manabii wote walikuja na sheria moja. Na hawakuja kupingana bali kukamilisha.

Sijui kama umenielewa
 
Google usiwe mchovu si ayah bali kuna sura nzima zinatoa guidance juu ya sayansi. Mfano sayansi ya anga, asili ya mvua nk.

Ktk surat Radd.

Try googling my friend
Umeona ni namna gani Msaafu ulivyokuwa sio wa kuaminika?

Wewe kama muislamu hukupaswa kuniambia niende google.

Ilipasa unipe kifungu kutoka msaafuni then mimi niusome.

Hongera!!
 

Attachments

  • Screenshot_20240329_121749_Biblia Takatifu.jpg
    Screenshot_20240329_121749_Biblia Takatifu.jpg
    531.9 KB · Views: 1
  • Screenshot_20240329_121926_Biblia Takatifu.jpg
    Screenshot_20240329_121926_Biblia Takatifu.jpg
    504.9 KB · Views: 1
  • Screenshot_20240329_122129_Biblia Takatifu.jpg
    Screenshot_20240329_122129_Biblia Takatifu.jpg
    501.5 KB · Views: 1
Swali langu bado liko pale pale.

Umesema hakuna mwanafunzi wa Yesu aliyewahi kumuona Yesu. Je Yesu alikuwa anawatumia Voice Notes?

Source ya taarifa kuwa Prof Saul ndiye aliyemuona Yesu iko na credibility kwa asilimia ngapi>?

Bila shaka chanzo iko hakina umri kuzidi maandiko ya biblia, kwanini tuamini waliyoyazungumza watu wa baadaye kabisa?
Maalim.

Tuseme historia vzr.

Yesu alikuja ktkt ya dola ya rumi ya kale. Moja ya viongozi wakuu wa dola hii ni mtoto wa mfanyabiashara mkubwa wa wakati huo ambae ni sauli.

Yesu alipoanza kupingana na utawala wa rumi, makuhani na wa kirumi wakamuona ni tishio.

Sauli akiongozana na wasiojulikama wakaanza kuwauwa wafuasi ya yesu kwa kuwafata misikitini (sinagogi) watoto hawa wa ukoo wa daudi.
Wakaanza kumfungulia kesi kama Lissu. Na mwisho wakamhukumu kifo.

Baada ya kutokea yaliyotokea. Na yesu kupaa, sauli atajiondokea zake kutoka Palestine hadi hadi syria.

Pale Palestine Jerusalem wakimpinga kwa kusema kwake yule yesu na kwa jinsi alivyonusurika kupata adhabu ya laana kwa wayahudi akasema huyu yesu ndie Mungu mwenyewe. Na wala hakutumwa na Mungu bali yeye ndie mungu.

Kwa ufupi adhabu ya kusulubiwa kwa warumi ilikuwa ni adhabu ya juu kwa mtu aliwapinga sheria za warumi na kwao waliita ni adhabu anayopewa aliyelaaniwa na Mungu wa warumi.

Na kwamba kikubwa tunachojifunza sasa. Na sisi tuwe tayari kusubiwa, kuwekwa ktk mifuko ya sandarusu kupinga utawala huu wa kibinadamu na kupigania sheria za Mungu zitawale hapa duniani.

Jukumu hilo kwasasa wanalo waislam pekee. Na wako tayari kufungwa kwa miaka kadhaa kwa kosa la LENYE adhabu kubwa kwasasa kwa ajili ya kundi hilo.

Kosa la ugaidi wanaoutengeneza wenyewe watawala.
 
Ni ngumu sana kwasababu hayo mambo kuweza kuandikwa na kutiwa ktk kumbukumbu ktk miaka hiyo ilihitaji Mungu aingilie kati na uweza wake kwa manufaa ya kizazi kijacho na cha baadaye.
Umesema kweli kabisa ndio maana akatokea Muhammad.

Najua unakuwa na kigugumizi kwa kuwa mafundisho ya Muhammad yanakinzana pakubwa na agano jipya ambalo ndilo msingi wa mafundisho ya ukristo wako.

Jiulize kwanini walau agano la kale inafanana na quran.

Jibu jepesi ni hili. Agano jipya ni disinformation tupu.

Ni uongo uliotengenezwa na kuratibiwa kwa ustadi mkubwa wa wanazuoni wabobezi. Ukiongozwa na sauli
 
Umeshindwa kuiamini biblia yako utamuamini nani? Umekatazwa kula nguruwe kwenye biblia na bado unakula sasa kuna kitu kingine utakiamini kweli?

“Nguruwe msimle; ana kwato zilizogawanyika lakini hacheui; kwenu ni najisi. Kwa sababu wanyama hao ni najisi msile nyama yao wala msiguse mizoga yao” (Walawi 11: 7 – 8).

Umeshindwa kuamini kitabu chako imani yako ina faida gani sasa.
 
Karibu saa tisa, Yesu akapaza sauti, akisema: “Eli, Eli, lama sabakthani?” yaani, “Mungu wangu, Mungu wangu, kwa nini umeniacha?”

Mathayo 27:46
Ni vigumu kwa wewe usiye trinitarian kuweza kufahamu Matayo 27:46

Kama vile sisi wakristo tunavyoshindwa kuielewa Sura ya 33.Al-Ah'zab Mstari wake wa 56.

Unaosema Mungu (Allah) na Wanamswalia Mtume.

Yaani Mungu (Allaha) na Malaika wanapiga magoti kumswalia Mtume? Aisee.

Ukiweza kufahamu huo mstari wenu basi Matayo 27:46 haitokupa shida.
 
Unamuamini vip yesu ambaye kaja baada ya Mussa, Daudi 😅😅😅

Ina maana waliokuwepo kabla ya yesu kuja hawakuwa na dini sio?
Unamaanisha hutakiwi kumuamini Nabii Issa kwa sababu amekuja baada ya Mtume Muhhamad?
 
Yesu sio mungu na hajawahi kuwa mungu
Hujajibu swali.

Zingatia uzi.

Hata mimi nataka sababu ya kwanini nikuamini wewe uliyezaliwa mwaka 1997 na sio wale walio pata kuishi nyakati za Yesu za karne ya kwanza/.
 
Back
Top Bottom