Kwanini Hayati Magufuli alitumia " State apparatus " kuunyamazisha Umma?

Sir John Roberts

JF-Expert Member
Mar 1, 2017
9,668
16,026
State apparatus ni vyombo vya ulinzi na usalama kwa wasioelewa kimombo. Marehemu John Pombe Joseph Magufuli katika style ya utawala wake aliunda serikali kwa kutumia "State Apparatus personell" kuanzia viongozi wa kisiasa mpaka maofisa waandamizi serikalini. Ilikuwa aidha ni major wa jeshi, brigadier mstaafu au kanali na wengine kutoka vyombo vya ulinzi na usalama: polisi, Usalama wa Taifa, TAKUKURU n.k.

Kiukweli ni Watanzania wachache walimuelewa mzee yule na style yake ya uongozi. Wengi tulilalamika utawala wa kimabavu usiojali uhuru kwa wananchi, demokrasia kwa vyama vya upinzani, uhuru wa vyombo vya habari, Bunge n.k. (Hapa Kazi tu).

Lakini miaka kadhaa baada ya kifo chake, nimeona tofauti kubwa kati ya utawala wa sasa na uliopita kwa namna serikali inavyoendeshwa. Na naweza kusema, Mh. Rais Samia, kwa aina hii ya utawala wako, ukubali na kubeba madhara yake (consequences) na uwe na kifua hasa cha kustahimili hayo yatokanayo.

Sikufundishi namna ya kuendesha nchi, ila tu nakutahadharisha Waswahili tuna msemo: "Ukicheza sana na mbwa utaingia nalo msikitini."

Watakaokuja kuchangia, tafadhali tuchangie kwa ustaarabu. Siyo mlete kejeli na mambo ya siyo na mbele wala nyuma (Watanzania tunapenda porojo).
 
Unataka Samia ateke na kuua watu?

Naona wameanza kutishia kuua mawakili pengine wameshaanza kufuata ushauri wako.

Halafu mleta mada huna maana, unataka Samia aanze kuteka, kupoteza na kuua watu halafu unataka tuchangie mada yako kistaarabu.

Ina maana unataka Samia afanye yale ya Ben Saa nane, Azory Gwanda, Simon Kanguye, Elias Michael, na maiti za kwenye viroba?.

Inasikitisha sana.
 
Unataka Samia ateke na kuua watu?

Naona wameanza kutishia kuua mawakili pengine wameshaanza kufuata ushauri wako.

Halafu mleta mada huna maana, unataka Samia aanze kuteka, kupoteza na kuua watu halafu unataka tuchangie mada yako kistaarabu.

Ina maana unataka Samia afanye yale ya Ben Saa nane, Azory Gwanda, Simon Kanguye, Elias Michael, na maiti za kwenye viroba?.

Inasikitisha sana.
Hapana sina maana hiyo utakuwa umenielewa vibaya. Nilikua mpinzani mkubwa aina ile ya utawala ingawa nimeona tofauti kubwa kati ya wakati ule na sasa nimemuelewa kwanini Magufuli aliamua kufanya vile. Nimemshauri tu Mh. Rais wa sasa awe na kifua cha kustahamili consequences za uhuru.
 
Awamu hii wataua watu wengi sana tangia tupate uhuru.

Maana mambo wanayofanya ni mwendawazimu pekee anaweza kuyavumilia.
Hatutaki kurudi tulipotoka. Ninamshauri tu huyu Rais wa sasa awe na kifua cha kustahamili consequences za uhuru alioamua kuuachia.
 
kama marehemu ambaye alikuwa ni mbabe kwelikweli na kulindwa isivyo kawaida alitumia dola ila mwishowe yakamshinda, unadhani hawa ambao wamepewa tuhuma kali za ufisadi wakitumia dola ndiyo watakuwa salama ?

Ndiyo mabavu yanaweza kutumika na watu wakaumizwa, lakini tatizo kubwa ni kwamba hili linaloendela limegeuzwa swala la kidini na kikanda. Ingekuwa rahisi kwa dola kama hizi vurugu ni za kisiasa, bahati mbaya sana nyuma yake kuna suala la dini, ubaguzi wa rangi na ukanda.

Mabavu yakitumika watu wanaweza kutafasiri kwamba walengwa ni wa dini fulani jambo ambalo litaigawanya zaidi nchi. Kumaliza changamoto kama hizi busara ya hali ya juu inabidi itumike. Ethiopia miaka yote matatizo yake yalikuwa ni kisiasa tu, ila lilipokuja suala la ukanda wamejikuta wamefika walipofika leo huku wakishindwa kutoka.
 
kama marehemu ambaye alikuwa ni mbabe kwelikweli na kulindwa isivyo kawaida alitumia dola ila mwishowe yakamshinda, unadhani hawa ambao wamepewa tuhuma kali za ufisadi wakitumia dola ndiyo watakuwa salama ?

Ndiyo mabavu yanaweza kutumika na watu wakaumizwa, lakini tatizo kubwa ni kwamba hili linaloendela limegeuzwa swala la kidini na kikanda. Ingekuwa rahisi kwa dola kama hizi vurugu ni za kisiasa, bahati mbaya sana nyuma yake kuna suala la dini, ubaguzi wa rangi na ukanda.

Mabavu yakitumika watu wanaweza kutafasiri kwamba walengwa ni wa dini fulani jambo ambalo litaigawanya zaidi nchi. Kumaliza changamoto kama hizi busara ya hali ya juu inabidi itumike.
Wanaoligeuza kuwa suala la udini na ukanda watakua wameshiwa hoja. Hapa nazungumzia madhara ya kuachia uhuru wa habari, bunge na taasisi za kiraia na nimempa ushauri rais kuwa na kifua cha uvumilivu . Kwa upande wa Rais ukisema mwishowe yakamshinda nashindwa kukuelewa maana alikufa tu kama watu wengine wanavyokufa ( otherwise utueleze alikufa kufaje) hakuna lililomshinda.
 
Wananchi wakiwa na maswali yao ni vyema wajibiwe, hizo state apparatus hazina maana, na wala haziwezi kuwafunga watu midomo, tangu enzi za Dr. Ulimboka kwenye mgomo wa madaktari.
Sijui kama umesoma ukanielewa. Tafadhali rudia kusoma nilichoandika.

Watanzania tunapenda porojo
 
Wanaoligeuza kuwa suala la udini na ukanda watakua wameshiwa hoja. Hapa nazungumzia madhara ya kuachia uhuru wa habari, bunge na taasisi za kiraia na nimempa ushauri rais kuwa na kifua cha uvumilivu . Kwa upande wa Rais ukisema mwishowe yakamshinda nashindwa kukuelewa maana alikufa tu kama watu wengine wanavyokufa ( otherwise utueleze alikufa kufaje) hakuna lililomshinda.
Sawa.
 
State Apparatus ni vyombo vya ulinzi na usalama kwa wasioelewa kimombo. Marehemu Joseph Pombe Magufuli katika style ya utawala wake aliunda serikali kwa kutumia" State Apparatus personell " kuanzia viongozi wa kisiasa mpaka maofisa waandamizi serikalini ilikua Aidha ni major wa jeshi, brigadier mstaafu au kanali na wengine kutoka vyombo vya ulinzi na usalama polisi , Usalama wa Taifa , TAKUKURU n.k
Kiukweli ni watanzania wachache walimuelewa mzee yule na style yake ya uongozi wengi tulilalamika utawala wa kimabavu usiojali uhuru kwa wananchi , demokrasia kwa vyama vya upinzani , uhuru wa vyombo vya habari , Bunge n.k ( Hapa Kazi tu)

Lakini miaka kadhaa baada ya kifo chake nimeona tofauti kubwa kati ya utawala wa wa sasa na uliopita kwa namna serikali inavoendeshwa na naweza kusema Mh. Rais Samia kwa aina hii ya utawala wako ukubali na kubeba madhara yake ( consequences) na uwe na kifua hasa cha kustaahimili hayo yatokanayo.

Sikufundishi namna ya kuendesha nchi ila tu nakutahadharisha waswahili tuna msemo ukicheza sana na mbwa utaingia nalo msikitini .

Watakaokuja kuchangia tafadhali tuchangie kwa ustaarabu siyo mlete kejeli na mambo ya siyo na mbele wala nyuma ( watanzania tunapenda porojo.
Alikuwa ni MWOGA sana kinyume na wafuasi wake wanavyomwita Shujaa. Alikuwa hana uwezo wa kujenga hoja na kuvumilia kukosolewa.

Ndani zaidi alikuwa Fisadi, mwizi, mwongo na mbinafsi. Aendelee kuungua na moto wa jehanam huko aliko
 
Hakuwapa uongozi Takukuru coz ni watu Fulani wanaojielewa tofauti na vyombo vingine wao black ni black,white ni white maisha yanasonga
 
Back
Top Bottom