Kwanini CCM Iko Matatani?

Ni kwasababu baadhi ya watanzania wamekuwa na uroho wa madaraka na wanatumia njama za hata kuihujumu serikali arimradi watinge ikulu.watu hawa hawako vyama vya kupinga tu hata ccm na ndani ya serikali wapo.wanatumia kila hila hata kuhatarisha maisha ya kila siku ya watanzania lakini watz tunaofikiri kwa mmbongo zetu tumekataa kuwachagua kwa zaidi ya 60% of votes.
 
Ile kauli ya Dr. Mwakyembe kwamba WATANZANIA SIO ....................................... On the face of that statement, its just one simple statement. Ila ni kauli ya mtu kuandikia paper na ikawa published na akawa promoted (if it involves that).........

Tutake tusitake information is power. Igunga na sehemu zingine kote Tanzania mwamko na vugu vugu la kisiasa etc sio lelemama..... That power lipo Tanzania nzima, haya mengine sasa ya ufahamu, uelewa, hiki kikoje yanafuatia............
 
ccm haipo matatani kwani ilikuwa hivyo zamani ila sasa CCM IPO MATEKENI..................kila mwenye uwezo wa kubatua anabatua atakavyo
 
CCM as an organization has grown too big and therefore hard to manage. The stakes and interests are to many and quite diverse. Unlike Nyerere's time, ccm for the last decades has been promoting the wrong values (corruption, majungu, fornication and outright stealing from the state ). As such, these are not values which would promote a sustainable organization, instead, ccm is wrotening from within which is soon going to lead to an ultimate death.
Sasa kuna majibu ya haraka na ya pupa. Na yapo majibu yanayohitaji kutafakari kidogo. Kwa haraka mtu anaweza kusema kuwa CCM iko matatani kwa sababu CDM wanapandikiza mbegu ya chuki kwa wananchi. Mwingine (katika haraka yake) anaweza kuja na kusema CCM iko matatani kwa sababu wameshindwa kujivua "gamba". Mwingine naye katika kujaribu kuelezea kwanini CCM iko matatani anaweza kuja na kusema kwa sababu ndani yake kuna "migongano".

Naomba kupendekeza kwamba kuna jawabu la kina zaidi. Naamini vyote hivi tunavyoviona ni dalili tu ya tatizo (symptoms). Sasa kwa wale ambao mnaifahamu CCM labda tangu ikiwa TAA hadi leo hii mnaweza kutusaidia na kuwasaidia vijana wetu kuelewa kwanini CCM iko matatani leo hii? Kwanini inajitahidi kutumia nguvu sana kushinda uchaguzi wakati zamani ilikuwa rahisi sana. Kwanini kwa mfano mwaka 2005 ilifanya vizrui sana kuliko wakati mwingine wa vyama vingi na miaka mitano baadaye ikafanya vibaya kuliko wakati wowote wa historia yake?

Katika majibu yetu tujaribu kuleta yote bila kujali ukweli wake. Ieleweke siulizii majibu ya kisayansi; najaribu kufanya brain storming ambayo inaweza ikatuelewa kwanini hiki chama ambacho kiliwahi kuwa mashuhuri zaidi, kupendwa zaidi na hata kuhofiwa leo hii kinaonekana kigeni machoni pa watu?
 
Mchango wangu katika bangua bongo hii unaweza kuwatatiza wengi lakini nitasema ili nitimize wajibu wangu kwa JF na wananchi wa Tanzania. Asili ya CCM ni TANU ambayo pia ilirithi majukumu ya TAA ambacho hakikuwa chama cha siasa bali Asasi isiyokuwa ya kiserikali ambayo ilikuwa na makusudi ya kupigania haki na ustawi wa watu weusi na kuondoa ubaguzi na dhuluma za wakoloni dhidi ya wafanyakazi wa kiafrika. Makusudi yake ilikuwa kuwaunganisha waafrika ili wawe na sauti kubwa wakati wakilalamikia haki zao hasa wale wa mijini. TANU ilipokuja iliingiza harakati za ukombozi wa kisiasa na kumng'oa mkoloni. TANU ilijipambanua kama chama cha siasa ambacho kilikuwa na jukumu la kuwaunganisha Watanganyika kujitawala kwa kudai uhuru kutoka mikononi mwa wakoloni. Kilikuwa chama cha wanyonge kikiunganisha makundi makubwa ya kijamii kwa wakati ule ya wakulima na wafanyakazi. Hata hivyo katika kufikia malengo yake hakikufanya dhambi ya ukaburu kwa rangi bali kilijitenga na makundi ya kifisadi na yale ambayo yalikuwa na ubnafsi katika harakati za kujitafutia riziki. TANU haikuwahukumu lakini iliwatenga kisiasa hasa katika uongozi. Wafanyabiashara na wapinzani wa itikadi yake hawakupatiwa nafasi ya uongozi na waliwachuja mapema kwa wale waliodiriki kuomba.

CCM ilirithi mambo yote ya tanu na pengine iliyafafanua kitaalamu zaidi, hata hivyo muda ulivyozidi kupita CCM imekuwa ikionyesha uchovu wa kisiasa na kushindwa kuhimili ushindani wa hoja na hivyo kilichofanyika ilikuwa ni kufungulia kundi ambalo halikuasisi siasa za chama hicho kushika hatamu za uongozi (uliwahi kuona wapi fundi wa gari awe mtu ambaye hakusomea kutengeneza gari?). Wafanya biashara wakawa wafadhili wakubwa wa Chama, na kwa kupitia hii dhana ya ufadhili katika siasa wakapata nafasi adimu ya kuwa karibu na viongozi wa chama na serikali wakaanza kuwaonyesha viongozi wetu waliokuwa maskini wa mali lakini werevu utamu wa fedha. Walipozidi kunogewa wakawambia asali hii ya fedha ni tamu zaidi kama na nyinyi mtalibomoa azimio la Arusha na miiko ya uongozi nao bila uoga na kwa ujasiri usiozoeleka wakabomoa miiko hiyo ya uongozi.

Viongozi hawakujua kuwa kuwaingiza katika chama kundi ambalo halikuasisi siasa za chama walikuwa wakiwapigia kura ya kuondoka walalahoi wakitanzania ambao sasa walikosa mtetezi wa kisiasa na masilahi yao sasa yalikuwa hayana nafasi . Niliwahi kumsikia Rais Mkapa akisema katika moja ya hotuba yake ya mwisho wa mwezi akiwaambia watanzania waache wivu na badala yake wafanye bidii, sikujua kauli hii ya mkapa kama ilitoka kwa bahati mbaya au alitaka kujilinda na uhalifu wake wa kisiasa alipokuwa Ikulu. Watanzania hawakuwa wanalalamika kwa sababu za wivu walilalamika jinsi utaratibu wa uongozi ulivyokuwa umeanza kupinda na kuhatarisha maslahi ya wengi. Siasa za uchumi wa ubinafshaji si mbaya kama zitafanywa katika misingi ya uwazi na wenye kuzingatia masilahi ya umma na siasa za uchumi wa uwekezaji si hatari kama wawekezaji watawekewa misingi ya kuwajibika na kunufaisha watanzania. Wanachojivunia CCM leo kama mafanikio ni pale wanapohesabu idadi ya shughuli zilizofanya hasa katika miradi ya ubinafshaji na uwekezaji. Hawadiriki kabisa kujua uhalifu wa kiuchumi wanaofanya katika miradi hii kwa jamii ya watanzania, hawaulizio ajira je kwa mtanzania, kodi je? bei chee ya kuwauziia mashirika yetu na rasilimali asili zetu. Wanahesabu miradi ya uwekezaji katika madini na utalii hawadiriki kutwambia kile tunachonufaika nacho ni sehemu kidogo sana ya haki yetu ama hakuna kabisa.


Wametujengea shule, barabara, miradi ya maji, afya na mingineyo mingi lakini kwa gharama kubwa kiasi kuwa hakuna thamani ya hela tena na watanzania wa leo ni waelewa wanaona hapa wameibiwa. Wafanyabiashara/matajiri hawajui siasa, wengi hawana utu tulichoambulia kutoka kwao ni kuasisiwa kwa mfumo wa kura za kununua, kusitawi kwa rushwa katika siasa na mengine mengi machafu na viongozi kupakatwa na matajiri kiasi kuwa wakiingia madarakani wanajishughulisha na ulipaji fadhila ili waendelee kuwapo.

Sitegemei wa kufikiria CCM iliyoasi asili yake kwa kuasisiwa na kundi lisilo asili iache kuwa na mgogoro na makundi yake asilia. Bahati mbaya sasa CCM ilipofikia haiwezi tena kukidhi haja ya makundi hasimu yaani makundi asilia na yale yaliyoibuka karibuni. Wanataka kura kutoka makundi yake asilia ili wawe madarakani vilevile wanataka fedha kutoka katika kundi jipya ili wamudu siasa za ushindani. CCM hawawezi kujua mvutano huu ndio uliowapotezea mvuto, hawezi kujua kuwa mvutano huu ndio unaowaweka matatani, kwao viongozi wetu, yote sawa na walipojaribu kujitambua na kutaka kuchukua hatua ya kujinasua nadhani wote mumeona na katika siasa zetu Igunga imeingia katika rekodi ya siasa kigeugeu.


kustawi kisiasa ni kutafuta udhaifu wa adui yako vyama shindani kisiasa na CCM vimeona upenyo huo na sasa vinajaribu kutupia makonde mazito hapohapo ili pavimbe papasuke na damu itoke kwa wingi mpaka CCM iwe dhaifu waiondoe kiulani madarakani, hilo mnaliona ingawa si kwa sipidi mnayotaka lakini CCM wenyewe wanatambua kuwa mzigo walionao umeanza kuwaelemea, wameanza kukodi wabebaji ambao nao nahisi watachoka haraka kuliko wanavyotegemea umma ukiendeleza nguvu zake kwao. Ni swali dogo tu kwa vyombo vya dola ambao sasa ndio wabebaji wakuu wa mzigo wa CCM "wangepanda kuona watanzania wangapi wanakufa ili CCM iendelee kuwa madarakani"

Mwanakijiji na wewe nae ni sehemu ya kilo ambazo zinafanya mzigo wa CCM kuwa hauwezi kubebeka endelea kazi nzuri sana ambayo italipa muda mfupi ujao

Aluta condinua, Our lost glory and stolen freedom will be with us soon
Well said mkuu! hakika u made my day kwa huu uchambuzi wako....yaani kama mi-ccm itapita kwenye post hii basi BP itawashika.
Na hapo kwenye bold na blue, si Mwanakijiji tu hata wewe kwa huu uchambuzi uliyotumwagia hapa'wewe pia ni mzigo mzito kwa ccm. Big up!
 
ccm IMEPOTEZA dira na mwelekeo, viongozi wanaangalia maslahi yao na familia zao. Watendaji wanateuliwa kwa kujuana na sio utaalamu matokeo yake ni mawazo rahisi kwa mambo magumu, no creativity, kila kitu wa cut na ku paste. Hakuna kauli moja ya viongozi(kila kiongozi ana kauli yake kwenye jambo moja) AHADI hazitekelezwi. (Bora ukae kimya ufanye kitu cha maana au usifanye kabisa kuliko uahidi usitekeleze).

Kutokusoma alama za nyakati na kwenda sawa na uelewa wa wananchi, kutokubali kukosolewa............
Umesomeka kakaa..na hayo tu hoja ya kuwa wananchi wa sasa sio wa zamani haina mashiko..hata CCM ya sasa haipo ka zzaamani hivyo hilo sio tatizo...!naongezea wanaojiuma kuonesha maendeleo ambayo ndio vitu vya kuongelea kwa wananchi wanafanyiwa zengwe.
 
Ni kutokana na kuingiza kundi la wafanyabiashara kama wadhamini wakuu wa chama, mfanya biashara anaweza kuwa mwansiasa, lakini ni lazima kuwepo na misingi na kanuni zinazozuia kutumia utajiari wake kuinfluence power katika chama. Kwa sasa hivi makundi ndiyo jibu sahihi, lipo kundi la wanyonge ambalo linajiona limesahaulika kwa viongozi, lakini haliko radhi kuwaachia matajiri wachache wabaki na chama, hivyo wanakomaa nao humo humo, lipo kundi la matajiri ambalo linatumia ukwasi wao kuweka viongozi wa juu katika chama, na pia wanatarajia fadhira kutoka kwa hao viongozi. Hii inazaa upendeleo, kitu ambacho kinaleta minyukano ndani ya chama.
 
CCM ife tu hata leo na haina cha maana zaidi inatufanya watanzania kuwa maskini na kupoteza umoja wetu
 
Sasa kuna majibu ya haraka na ya pupa. Na yapo majibu yanayohitaji kutafakari kidogo. Kwa haraka mtu anaweza kusema kuwa CCM iko matatani kwa sababu CDM wanapandikiza mbegu ya chuki kwa wananchi. Mwingine (katika haraka yake) anaweza kuja na kusema CCM iko matatani kwa sababu wameshindwa kujivua "gamba". Mwingine naye katika kujaribu kuelezea kwanini CCM iko matatani anaweza kuja na kusema kwa sababu ndani yake kuna "migongano".

Naomba kupendekeza kwamba kuna jawabu la kina zaidi. Naamini vyote hivi tunavyoviona ni dalili tu ya tatizo (symptoms). Sasa kwa wale ambao mnaifahamu CCM labda tangu ikiwa TAA hadi leo hii mnaweza kutusaidia na kuwasaidia vijana wetu kuelewa kwanini CCM iko matatani leo hii? Kwanini inajitahidi kutumia nguvu sana kushinda uchaguzi wakati zamani ilikuwa rahisi sana. Kwanini kwa mfano mwaka 2005 ilifanya vizrui sana kuliko wakati mwingine wa vyama vingi na miaka mitano baadaye ikafanya vibaya kuliko wakati wowote wa historia yake?

Katika majibu yetu tujaribu kuleta yote bila kujali ukweli wake. Ieleweke siulizii majibu ya kisayansi; najaribu kufanya brain storming ambayo inaweza ikatuelewa kwanini hiki chama ambacho kiliwahi kuwa mashuhuri zaidi, kupendwa zaidi na hata kuhofiwa leo hii kinaonekana kigeni machoni pa watu?

CCM: Kutoka TAA mpaka kibatari.
 
Kwa wale tulioiona TANU, then ikaja CCM, watakubaliana nami kwamba huko nyuma mfumo wa utawala uliweza kuwadanya vizuri tu Watanzania kwamba ndio wamiliki wa nchi yao na hatima yao na watoto wao. Nadhani hii haikutokana na sera chama tu, bali haiba ya viongozi. Naamini hivyo kwa sababu mtu pekee alieyeweza kubuni mfumo na kuwapa wenzake wameze na kusimamia utekelezaji wa sera na maamuzi mbalil mbali (tena wakati mwingine watendaji hawakuelewa waliyotumwa) ni Nyerere. Ndiyo maana baada ya mzee huyo kustaafu kila kitu kikasambaratika.

Nadhani CMM hawawezi kulikwepa gharika. Hawakujenga mifumo ya utawala (governance institutions) na kwa sasa hawana tena muda wa kufanya hivyo.

Suala la kutafakari ni maandalizi ya maisha ya Watanzania bila CCM....Hata wakibebwa vipi...mbeleko zitachanika!
 
Wananch wanapoteza iman na ccm c kwa 7b inatenda mabaya la hasha ukichunguza kwa kna utagundua chadema kuna uozo zaid hata ya ccm..kwa kuwa watu hawakchunguz vzur na wanatekwa na propaganda na ahad zao zczo za kikwel pia cdm viongoz wake n opportunist..hvyo wamewapata watu weng sana wacopenda kujiulza haya n ya kwel au? Mf.dr slaa kudai wapunguziwe mishahara(wabunge)..masuala ya posho..wananch wanashdwa kuelewa kuwa cdm co wakomboz..na mwshowe wamewapata MAZUZU!..
 
ccm has sold its soul for buying its favourates! how now can liberate its people? watu walikipenda chama sabbu hapo mwanzo
chama kilikuwa ktk harakat za kupigania uhuru
2:hapo mwanzo chama kilikuwa ni cha wakulima na wafanyakazi leo ni pango la wafanya biashara wakubwa
3:ccm haikubaliki ni kutokana na wakati that is time bar watu wamechoka kuwa na hichi chama kutokana na kushndwa kutatua kero za wakati
3:upumbavu ujinga vinakata kamba mtazamo2
 
Wananch wanapoteza iman na ccm c kwa 7b inatenda mabaya la hasha ukichunguza kwa kna utagundua chadema kuna uozo zaid hata ya ccm..kwa kuwa watu hawakchunguz vzur na wanatekwa na propaganda na ahad zao zczo za kikwel pia cdm viongoz wake n opportunist..hvyo wamewapata watu weng sana wacopenda kujiulza haya n ya kwel au? Mf.dr slaa kudai wap
HATA DARASA LA TATU HAWEZ KUTOA WAZO KAMA HILI MAANA UMEFIKIRIA MPAKA MWISHO
 
CCM ilianza kupoteza mvuto kwa wananchi na wanachama wake kwenye miaka ya 80 wakati ilipoanza kukumbatia wafanyabiashara na kuwaacha wakulima na wafanyakazi ambao ndio walikuwa nguzo na msingi mkuu wa chama. Wafanyabiashara wakaanza kujiingiza polepole hadi kwenye uongozi mkuu kwa kisingizio cha ufadhili na kufanikiwa kuwageuza hata viongozi safi tuliokuwanao kuanza kupenda mali na anasa kitu ambacho kilikwa mwiko enzi za awamu ya kwanza hadi kupelea kuvunjwa kwa Azimio la Arusha.

Nguvu ya wafanyabiashara kwenye chama ndiyo inayokiyumbisha chama, leo CCM hakitegemei tena wananchi kupiga kura ili kishinde kinategemea nguvu ya pesa hakina imani hata kama ni wanachama wake lazima kiwanunue. Zamani asset kubwa ya chama ilikuwa wananchi hasa wa vijijini lakini leo asset kubwa ya chama ni wafanyabiashara, mwananchi/mwanakijiji amekuwa akitumiwa kama tool (jembe) kufanikisha mavuno (kura) baada ya mavuno anasahauliwa hadi msimu mwingine.

CCM ijue dunia inabadilika hata siasa zinabadilika kwa kung'ang'ania mifumo ileile ya enzi na viongozi walewale ni kukinyima chama nafasi ya kujitanua. Viongozi kama kina Msekwa,Sitta wapo kwenye chama tangu tukiwa chipukizi miaka ya 70 wakituahidi sisi ni viongozi wa kesho, kesho imefika lakini bado wao ni viongozi, vijana wakileta mawazo mapya wanakumbushwa ahadi ile ya zidumu fikira za m/kiti/viongozi. Mwisho wa siku unakuta vijana ambao wanataka kutoa mawazo yao wanajiona kama hawatakiwi (Nape) wana deflect wanaamua kutafuta sehemu nyingine (chama mbadala) kutolea mawazo yao.
 
Wananch wanapoteza iman na ccm c kwa 7b inatenda mabaya la hasha ukichunguza kwa kna utagundua chadema kuna uozo zaid hata ya ccm..kwa kuwa watu hawakchunguz vzur na wanatekwa na propaganda na ahad zao zczo za kikwel pia cdm viongoz wake n opportunist..hvyo wamewapata watu weng sana wacopenda kujiulza haya n ya kwel au? Mf.dr slaa kudai wap<br />
HATA DARASA LA TATU HAWEZ KUTOA WAZO KAMA HILI MAANA UMEFIKIRIA MPAKA MWISHO
<br />
<br />
naona kwa vile ushabakwa kmawazo na wanasiasa wa chadema unafk kla m2 pia kabakwa
 
Ni kwa sababu haijui majibu ya maswali makuu waliyo nayo Watanzania wa leo. Kwa mfano, Tanzania ina rasilimali nyingi kuliko nchi zote katika Afrika mashariki, laikini kimaendeleo iko nyuma kwa mbali ya Kenya. Ndiyo maana Rais Kikwete alikuwa Paris Ufaransa akaulizwa kwanini nchi yako ni maskini pamoja na kuwa na rasilimali nyingi akajibu kuwa hata yeye hakujua sababu ya umasikini wa Tanzania.


Sio hilo tu hata akija mtaalamu mshauri ambaye amefanya vema katika nchi nyingine zikafanikiwa ikifika kwenye utekelezaji kila kitu kinaharibikia hapo kwa sababu ya mtazamo finyu wa kutanguliza ubinafsi badala ya kusaidia nchi ifanikiwa ili mafanikio hayo yasambae kwa wengi. Ndiyo maana kwenye MKURABITA pamoja na ushauri mzuri wa gwiji wa uchumi duniani Prof. De Sotto mpaka leo hakuna mafanikio yoyote ya maana.
 
Back
Top Bottom