Kiranga
Platinum Member
- Jan 29, 2009
- 71,282
- 105,486
Hapana.Sasa tatizo kwanza si hayo majibu ila tatizo ni wewe,kwa sababu jibu la swali unalouliza ushapewa kwa kuelezwa kusudio la mungu kuruhusu au kuweka maovu na mema. Sasa unachokifanya wewe unahoji kwanini kafanya hivyo na asifanye tofauti na hivyo kisa anao uwezo wa kufanya tofauti na hivyo?
Ndiyo nini sasa?
Tatizo majibu hayapo logically consistent.
Mtu anaweza ku solve
(x^2 + 2x + 1)/x + 2 = x
Kwa kusema x = 2
Lakini jibu hilo halina mantiki kwa sababu ukilitumia kwenye equation linakuwa la uongo.
Jibu la 2 halipo logically consistent kwa sababu ukilitumia katika equation utapata 2.25 = 2.
This is a clear contradiction.
Majibu niliyopewa yana contradiction.
Swali ni, kwa nini Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote kaumba ulimwengu ambao mabaya yanawezekana wakati alikuwa na uwezo wa kuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezekani.
Swali hili halijajibiwa katika njia iliyo logically consistent bado.