Lord denning
JF-Expert Member
- Jun 3, 2015
- 13,226
- 26,048
Kipimo cha uwezo wa mwanadamu kama anafikiri sawasawa ni namna anavyofanya mambo yake kulingana na wakati husika.
Dar es Salaam ndo Jiji Kuu la Biashara la Tanzania. Sio hivyo tu, ndo Jiji lenye watu wengi zaidi Tanzania na kadri siku zinavyozidi kwenda idadi ya watu inazidi kuongezeka.
Kwa binadamu ansyefikiri sawasawa, sikutegemea kama katika karne hii ya 21 tena mwaka 2023 kwenye Jiji hili barabara kuu zingeendelea kujengwa kwa njia 4.
Nipo Dar es Salaam na nimesikitishwa sana maana imejengwa barabara mpya kabisa kutoka mbagala hadi posta ila bado imejengwa kwa njia 4( mbili kwenda na mbili kurudi na katikati mwendokasi). Nimetembea pia njia ya kutoka Posta hadi Uwanja wa ndege nimeona ujenzi unaendelea na hali ni hiyo hiyo.
Swali langu kwenu Viongozi wa Tanzania. Je uwezo wenu wa kufikiri ndo umeishia hapo?
Kwa namna Jiji hili lilivyo na linavyotakiwa kuwa yaaani kama Jiji bora na la mfano Afrika Mashariki na Kati, nilitegemea barabara hizi kujengwa kwa Njia 6 hadi 8 pamoja na mwendokasi.
Kiufupi barabara zote kubwa za Dar zinazoingia Posta kuelekea Kibaha, Pugu, Mbagala, Bunju na inayotoka Morroco hadi Keko bila kusahau ya Mwenge- Ubungo hadi Bandarini zinatakiwa kuwa za njia 3 mpaka 4 kila upande na njia ya mwendokasi/ treni ya umeme katikati.
Ifike wakati nchi hii watu tufikiri kama tunaishi katika dunia wanayoishi wenzetu warabu na nchi za ulaya. Inasikitisha sana kuwa na mipango ya mwaka 1950/ 60 katika karne hii ya 21.
Naomba Viongozi wa Tanzania mbadilike kwa kweli.
Dar es Salaam ndo Jiji Kuu la Biashara la Tanzania. Sio hivyo tu, ndo Jiji lenye watu wengi zaidi Tanzania na kadri siku zinavyozidi kwenda idadi ya watu inazidi kuongezeka.
Kwa binadamu ansyefikiri sawasawa, sikutegemea kama katika karne hii ya 21 tena mwaka 2023 kwenye Jiji hili barabara kuu zingeendelea kujengwa kwa njia 4.
Nipo Dar es Salaam na nimesikitishwa sana maana imejengwa barabara mpya kabisa kutoka mbagala hadi posta ila bado imejengwa kwa njia 4( mbili kwenda na mbili kurudi na katikati mwendokasi). Nimetembea pia njia ya kutoka Posta hadi Uwanja wa ndege nimeona ujenzi unaendelea na hali ni hiyo hiyo.
Swali langu kwenu Viongozi wa Tanzania. Je uwezo wenu wa kufikiri ndo umeishia hapo?
Kwa namna Jiji hili lilivyo na linavyotakiwa kuwa yaaani kama Jiji bora na la mfano Afrika Mashariki na Kati, nilitegemea barabara hizi kujengwa kwa Njia 6 hadi 8 pamoja na mwendokasi.
Kiufupi barabara zote kubwa za Dar zinazoingia Posta kuelekea Kibaha, Pugu, Mbagala, Bunju na inayotoka Morroco hadi Keko bila kusahau ya Mwenge- Ubungo hadi Bandarini zinatakiwa kuwa za njia 3 mpaka 4 kila upande na njia ya mwendokasi/ treni ya umeme katikati.
Ifike wakati nchi hii watu tufikiri kama tunaishi katika dunia wanayoishi wenzetu warabu na nchi za ulaya. Inasikitisha sana kuwa na mipango ya mwaka 1950/ 60 katika karne hii ya 21.
Naomba Viongozi wa Tanzania mbadilike kwa kweli.