Mkuu hapo namba moja umenchekesha sana!.. Hakika waraka ukimfikia baba wa Taifa, atakufa kwa mara ya pili. Tehe tehe!
baba kuna mchungaji mstaafu ameibuka huko samunge,mawaziri wote wameenda kupiga kikombe!!huenda angeibuka miaka ile ya 99 hadi leo na wewe ungekuwepo unadunda!!!!Baba wamekueleza karibia yooote, ila wamesahau kukwambia kuwa, baadhi ya watuhumiwa wa EPA wamekula mvua tano. Wamesahau kabisa adhabu yako ya viboko 24, yaani 12 wakati anaingia ili wamsodome vizuri, na 12 wakati anatoka akamuonyeshe mkewe.
kwako marehemu baba wa taifa,natumaini umepunzika kwa amani hakika nataka kukujuza maajabu mengi yaliyotokea tz toka uaage dunia;
- Kepten john komba amekuwa mbunge lakini kazi yake ni kusinzia tu bungeni
- Lowasa alipata uwaziri mkuu
- CCM imekuwa kichaka cha mafisadi
- Chama Chako kimejaa magamba tu
- Raisi wa nchi hajui kwa nini watu wake ni maskini
- Madini ambayo uligoma yasichimbwe mpaka watu wako watakapokuwa na uwezo,leo yanachimbwa na wananchi wanauwawa kwa risasi wakipinga unyonyaji lakini serikali inawaita wavamizi.
- Magari ya ikulu yanachakachuliwa mafuta
- Mafisadi wanaitwa mashujaa
- Uongozi unapatikana kwa kuwa na pesa badala ya uwezo wa mtu
- Kilimo kimekuwa ni siasa tu watu wanakufa na njaa
- Kiongozi mkuu wa nchi (mkuu wa kaya) anahubiri udini
- Semina elekezi kwa mawaziri zakutosha pamoja ya kuwa wanakutana kwenye vikao vya baraza la mawaziri
- Yusuph makamba alishika nafasi ya katibu mkuu CCM
- UVCCM sio kisima cha fikra tena imegeuka kijiwe cha kahawa
Hakika baba wa taifa maajabu mengi yametokea,haya ni baadhi tu utayapata mengi leo hii, kwa sababu toka uondoke tz ya leo sio ile ambayo uliiacha au ile ulipenda iwe,tz ya leo pengo kati ya maskini na tajiri limekuwa kubwa mnno,mpaka sasa hakuna hatua zzte madhubuti za kupunguza umaskini wa watz zaidi ya usanii,upatapo walaka huu naomba utunusuru na hili ombwe la uongozi katika tz yetu yenye neema.Mungu ibariki tz na watu wake.
hahahha umenichekesha sana aiseee! nikikumbuka NAPE ni pic zake duuu!halafu kuna hii style ya kucheza inaita kiduku..CCM wanaicheza vizuri sana baba na wameshinda tuzo nyingi kwa hii style......
Viongozi 80% ccm ni wa dini moja.
29. Dr Slaa ndie atakayekuw rais 2015 baba
30. Baba ikulu wanataka kwenda watu walioiba wake za watu