Chaimaharage
JF-Expert Member
- Apr 3, 2012
- 211
- 78
Jana nimekuona Martin Shigella kwenye taarifa ya habari ya saa 2 usiku TBC1 ukitoa comments zako kuhusu kitendo cha aliye kuwa mwenyekiti wa UVCCM A-town Ndg.James Millya kujiondoa Magamba. Kauli uliyotoa ya kwamba falsafa ya kujivua gamba inaendelea ukieleza kuwa Millya alikuwa gamba kwa hiyo amepima na kujiondoa mwenyewe. Sasa nashindwa kuelewa kama kweli alikuwa gamba au la. Kauli yako inatofautiana na ya Mh.Mbowe ambapo yeye ameonyesha kuwa Bwana Millya wanamfahamu kwa muda mrefu na hana historia chafu kama mnavyotaka kutuaminisha.
Kwa mtizamo huu ni wazi kuwa kwa tafsiri yenu mtu ni gamba iwapo ataonekana kuwa mshauri wa kukitaka chama kufuata misingi bora na ya haki katika utendaji wake na mengine mema yanayo fanana na hilo. Na ambao siyo magamba ni wale mafisadi walio kubuhu na kuonekana kupingwa na umma kwa ujumla wake. Watu hawa mmekuwa nao kwa muda mrefu pasipo kuwachukulia hatua yoyote.Hakika CDM hawawezi kutamka maneno yale iwapo mtu husika ni gamba halisia tofauti na tafsiri yenu. Nadhani time will tell ku justify kama kweli tuhuma zako juu ya Millya kuwa ni gamba ni za kweli. Sina wasi wasi kuwa aibu itakushikeni mbele ya safari.
Na mimi pia napenda kutoa wito wangu kwa watu walio magamba ambao wanajiona safi na kukerwa na uchafu ulio kithiri humo tokeni. Tunawajua wamo wengi tu! ila hofu tu ndiyo inawaogofya kuchukua maamuzi. Ila najua muda utafika watatoka.Lakini katika hili napenda kutoa angalizo; wale wote wenye nia halisi ya kutaka mabadiliko ya kisiasa na kiuchumi katika nchi hii ili kufikia ukombozi wa kweli wafanye sasa. Watakapo taka kujiondoa huko waliko kipindi cha chaguzi ndogo na mkuu tutakuwa na mashaka dhidi ya dhamira yao. watakapo enguana katika chaguzi za ndani kisha kukimbia hao siyo wana mageuzi halisia bali ni wachumia tumbo wenye njaa kali na maslahi binafsi.
Kwa kumalizia napenda kusema hivi; MARTIN SHIGELLA, BENNO MALISA NA WENZIO KAMA VILE NAPE NI MAGAMBA HALISIA, HATA MKIJIVUA GAMBA HAMTO POKELEWA CDM KAMA MWENZENU. Iwapo mtapokelewa basi mtakaa kama miaka 10 mnasafishwa uozo ulio ndani yenu sababu sidhani kama fikra na mioyo yenu viko sawa na ni aibu kwa vijana kama ninyi kuwa na hivyo mlivyo na kutenda hayo mnayo tenda. Your future is vague. No light at the end of the tunnel.
Masahihisho katika thread yangu;
Jana fundi mitambo TBC1 alionyesha jina la aliye kuwa akihojiwa ni Beno Malisa lakini ki ukweli alikuwa ni Martin Shigella na siyo yeye. Lakini pamoja na yote fikra na mawazo yao ni sawa. Nawashukuru walio nisahihisha. Cha msingi ni kwamba concept ya ujumbe imefika. Gamba mmoja ni sawa na yote hata ukikosea kumtaja comment utakazo toa juu yao zinawagusa wote.
Kwa mtizamo huu ni wazi kuwa kwa tafsiri yenu mtu ni gamba iwapo ataonekana kuwa mshauri wa kukitaka chama kufuata misingi bora na ya haki katika utendaji wake na mengine mema yanayo fanana na hilo. Na ambao siyo magamba ni wale mafisadi walio kubuhu na kuonekana kupingwa na umma kwa ujumla wake. Watu hawa mmekuwa nao kwa muda mrefu pasipo kuwachukulia hatua yoyote.Hakika CDM hawawezi kutamka maneno yale iwapo mtu husika ni gamba halisia tofauti na tafsiri yenu. Nadhani time will tell ku justify kama kweli tuhuma zako juu ya Millya kuwa ni gamba ni za kweli. Sina wasi wasi kuwa aibu itakushikeni mbele ya safari.
Na mimi pia napenda kutoa wito wangu kwa watu walio magamba ambao wanajiona safi na kukerwa na uchafu ulio kithiri humo tokeni. Tunawajua wamo wengi tu! ila hofu tu ndiyo inawaogofya kuchukua maamuzi. Ila najua muda utafika watatoka.Lakini katika hili napenda kutoa angalizo; wale wote wenye nia halisi ya kutaka mabadiliko ya kisiasa na kiuchumi katika nchi hii ili kufikia ukombozi wa kweli wafanye sasa. Watakapo taka kujiondoa huko waliko kipindi cha chaguzi ndogo na mkuu tutakuwa na mashaka dhidi ya dhamira yao. watakapo enguana katika chaguzi za ndani kisha kukimbia hao siyo wana mageuzi halisia bali ni wachumia tumbo wenye njaa kali na maslahi binafsi.
Kwa kumalizia napenda kusema hivi; MARTIN SHIGELLA, BENNO MALISA NA WENZIO KAMA VILE NAPE NI MAGAMBA HALISIA, HATA MKIJIVUA GAMBA HAMTO POKELEWA CDM KAMA MWENZENU. Iwapo mtapokelewa basi mtakaa kama miaka 10 mnasafishwa uozo ulio ndani yenu sababu sidhani kama fikra na mioyo yenu viko sawa na ni aibu kwa vijana kama ninyi kuwa na hivyo mlivyo na kutenda hayo mnayo tenda. Your future is vague. No light at the end of the tunnel.
Masahihisho katika thread yangu;
Jana fundi mitambo TBC1 alionyesha jina la aliye kuwa akihojiwa ni Beno Malisa lakini ki ukweli alikuwa ni Martin Shigella na siyo yeye. Lakini pamoja na yote fikra na mawazo yao ni sawa. Nawashukuru walio nisahihisha. Cha msingi ni kwamba concept ya ujumbe imefika. Gamba mmoja ni sawa na yote hata ukikosea kumtaja comment utakazo toa juu yao zinawagusa wote.