fikirikwanza
JF-Expert Member
- Jan 25, 2012
- 7,452
- 3,065
Inasikitisha sana kuona mtanzania hana fursa nzuri ya kujenga makazi bora kutokana na dhana mbaya ya serikali ya kuggeuza ardhi kuwa mtaji mkubwa wa mapato ya kuendesha nchi, yaani haki mojawapo ya makazi kati ya nne za maji, chakula, makazi, mavazi inagandamizwa kwa kasi kubwa.
Hebu tujiulize kwanini bei ya kiwanja iwe kubwa kuliko kipato cha mfanyakazi wa kima cha chini kwa mwaka mzima??? kweli sera za CCM zinaakili??? yuko wapi Filikunjombe, yuko wapi Makamba January, yuko wapi Mama Anne Kilango, yuko wapi Sitta yuko wapi Mwakyembe, yuko wapi Waziri anayehusika na Makazi, Yuko wapi waziri wa Ardhi, Yuko wapi waziri wa maendeleo ya jamii, yuko wapi Waziri MKUU, yuko wapi RAIS???????
Zaidi yote yuko wapi Mbunge, ambaye tunamlalamikia kila siku kuhusu bei ghali ya viwanja, aliyeahidi kwenda kuongea matatizo yetu bungeni yuko wapi???
Je hata ardhi ambayo mungu katupatia bure nayo inashindikana kuigawa kwa watanzania ili wajenga makazi bora, inakuwa suala la tajiri hata na hili? kulala sehemu nzuri imekuwa luxury????
Ushauri wangu kila mtu apewe kiwanja kwa bei ya laki 1-5 tu, serikali ivunje mtandao wa ulanguzi wa viwanja; ardhi sio biashara, iweje mtu anachukua viwanja 50 ili auze kwa bei ghali, udhaifu wa serikali ukome sasa. Mbaya zaidi wakati wa magufuli alidai hata naibu wake RM alikwa na viwanja vingi vingi amejilimbikizia.
Unyonge wetu ututoke kwanza ndo tusitahili haki. TUUNGANE KUPAMBANIA HAKI YA MAKAZI BORA
Hebu tujiulize kwanini bei ya kiwanja iwe kubwa kuliko kipato cha mfanyakazi wa kima cha chini kwa mwaka mzima??? kweli sera za CCM zinaakili??? yuko wapi Filikunjombe, yuko wapi Makamba January, yuko wapi Mama Anne Kilango, yuko wapi Sitta yuko wapi Mwakyembe, yuko wapi Waziri anayehusika na Makazi, Yuko wapi waziri wa Ardhi, Yuko wapi waziri wa maendeleo ya jamii, yuko wapi Waziri MKUU, yuko wapi RAIS???????
Zaidi yote yuko wapi Mbunge, ambaye tunamlalamikia kila siku kuhusu bei ghali ya viwanja, aliyeahidi kwenda kuongea matatizo yetu bungeni yuko wapi???
Je hata ardhi ambayo mungu katupatia bure nayo inashindikana kuigawa kwa watanzania ili wajenga makazi bora, inakuwa suala la tajiri hata na hili? kulala sehemu nzuri imekuwa luxury????
Ushauri wangu kila mtu apewe kiwanja kwa bei ya laki 1-5 tu, serikali ivunje mtandao wa ulanguzi wa viwanja; ardhi sio biashara, iweje mtu anachukua viwanja 50 ili auze kwa bei ghali, udhaifu wa serikali ukome sasa. Mbaya zaidi wakati wa magufuli alidai hata naibu wake RM alikwa na viwanja vingi vingi amejilimbikizia.
Unyonge wetu ututoke kwanza ndo tusitahili haki. TUUNGANE KUPAMBANIA HAKI YA MAKAZI BORA