Kwa Wanasiasa: Kwanini tunauziwa viwanja bei ghali 2-8mil kwa bei ya serkali?

Je Mh. Halima Mdee na Uwaziri kivuli wa Ardhi, Nyumba na Makazi; Juu ya hili unasemaje kwa wananchi wa Tanzania???
 
hapa serikali inatakiwa iangalie kwa makini
Miji yetu inavurugika kwa fikra potofu za waliopewa dhamana. hivi ukiangalia jiji kama dar es salaam inasikitisha. nenda maeneo kama buguruni kwa ndani nyumba zinasikitisha, nenda magomeni nyumba za ajabu mikocheni ukipita barabara kuu unadhani ni jiji ukiingia ndani karibu na shule ya mikocheni A unashangaa hivi hapa ni mikocheni au, ukitoka viunga vya mji ndio kila mtu anajenga anavyopenda. bara bara hakuna, kupeleka huduma za jamii kama maji shida, wanasema serikali inaanzisha anwani za makazi sijui kwa maeneo yote au.

hivi waziri muhusika amekuja na kasi ya kupima viwanja huoni jiji na miji mingine imekwisha haribika vibaya. wekeni mkakati wa kupima viwanja kwa wingi simamisha ujezi holela wote na ikiwezekana weka sheria ndogo serikali za mitaa kila mwananchi anatakiwa kujenga katika kiwanja chenye ukubwa usiopungua kiasi fulani na kila kiwanja kiwe na barabara. ikiwezekana tumia serikali za mitaa vijana wapangalie tu maeneo kwa ujira mdogo mkiwaongoza kwa kuwaambia hapa acha ardhi kwa ajli ya shule, nakadhalika.

sasa hivi viwanja vinapimwa mbali watu wanajenga nyumba za kisasa mbali sana najiuliza humu katikati nani atajenga? wekeni mikakati ya kunusuru miji yetu ikiwezekana ondoa kodi kwenye vifaa vya ujenzi, pima viwanja kwa wingi na tunga sheria za maeneo fulani lazima nyumba iwe na hadhi fulani na wakazi wanaoweza kujenga wajenge wasioweza wauze kwa gharama nafuu wasogee nje ya mji.

hasara inayotupata kwa kutopangilia miji yetu ni kubwa mbali sana ukilinganisha na mapato kiduchu wanayopata kwa kufanya biashara ya viwanja.

waziri muhusika ajue hatutamsifu kwa kuanza kupima viwanja bali tutamkumbuka kwa kunusuru miji yetu na hapa atafakari achukue hatua. hapa kunahitajika uamuzi mgumu ila taifa baadae litakushukuru
 
Bila mpango mzuri kuhusu upatikanaji wa viwanja vya makazi, makazi bora ni wishful thinking, wizara inatusaidiaje kuja na sera ambayo inamwezesa kila raia kupata kiwanja iwapo atahitaji??? sera inayouzuia ardhi au viwanja kufanywa biashara???
 
Gvt plots are the cheapest though not affordable. Plot price is the summation of land acquits ion cost, survey costs, title deed preparation costs plus a premium of less than 15% call it a profit but in actual sence it serves as a revolving fund for future projects. If you are to pay a fair compensation, there is no way plots are going to be cheap because the two are dependent but very much opposing each other.
my opinion, we need to change our perspective, let the Nhc, NSsf, ppf etc construct as many houses as possible and float in the market for lease- purchase (call it mortgage), tuachane na ufahari wa kujenga nyumba wenyewe, hii biashara ndo kwanza inachangia ufisadi kwa kiwango kikubwa. Tax very very heavily private property developers, I'm telling you mwisho wa siku stress za nyumba zitapungua, wanaostahili (matajiri) kujenga nyumba watajenga wenyewe Si wengine tutaendelea
 
Sijafanikiwa kusoma maelezo yote ya kwenye uzi wako na hiyo ni kutokana na malalamiko mengi yasiyo na tija na kubwa ni ujinga tu wa kutoelewa kuhusu viwango vya bei ya ardhi. Ni vyema siku nyingine ukawa unauliza kuliko kulalama.

kwa ufupi; ardhi ndio raslimali mama kati ya zote, na uthamani wa ardhi umetofautiana kutokana na eneo ilipo ardhi hiyo, na thamani yake pia uongezeka siku hadi siku, lakini pia hutokea mara nyingine kwa thamani ya ardhi kushuka (laws and policies, zoning ana planning regulations etc).

Kuhusu bei ya ardhi; bei ya ardhi kwa soko huria uamuliwa na nguvu ya mahitaji na utoaji (demand and supply factors), kwa soko huria kiwanja ambacho kimepimwa na kina hati (a plot), kwa mita za mraba sio chini ya Tshs 30,000. Sasa zidisha hicho kisa na ukubwa (kwa maana ya eneo) la kiwanja husika, hii ni kwa Dar es salaam na maeneo mengine ya nchi yenye hadhi ya miji na majiji. Kwa Masaki, Upanga and the like; kwa mita square moja hupati kiwanja chini ya Tshs. 1,500,000. Kwa hiyo soko huria ndivyo lilivyo.

Tuje kwa serikali; serikali ya Tanzania imekuwa ikiuza ardhi na kuitoza kodi ardhi kwa bei ya kutupa kabisa, mleta mada kama uamini, hilo eneo unalo lalamika, hemu jaribu kuuliza kwa soko huria kiwanja bei gani, kwenye eneo hilo hilo. Tuache milawama ya ajabu na muda mwingine tuisifu serikali hasa kwenye kuhakikisha raia wake wanapata makazi yao wenyewe.
 
Mfumo wa kibepali ndo unakuja kwa kasi ,ambapo njia kuu za uchumi au uzalishaji kama Ardhi zitakua zinamilikiwa na wachache

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Sijafanikiwa kusoma maelezo yote ya kwenye uzi wako na hiyo ni kutokana na malalamiko mengi yasiyo na tija na kubwa ni ujinga tu wa kutoelewa kuhusu viwango vya bei ya ardhi. Ni vyema siku nyingine ukawa unauliza kuliko kulalama.

kwa ufupi; ardhi ndio raslimali mama kati ya zote, na uthamani wa ardhi umetofautiana kutokana na eneo ilipo ardhi hiyo, na thamani yake pia uongezeka siku hadi siku, lakini pia hutokea mara nyingine kwa thamani ya ardhi kushuka (laws and policies, zoning ana planning regulations etc).

Kuhusu bei ya ardhi; bei ya ardhi kwa soko huria uamuliwa na nguvu ya mahitaji na utoaji (demand and supply factors), kwa soko huria kiwanja ambacho kimepimwa na kina hati (a plot), kwa mita za mraba sio chini ya Tshs 30,000. Sasa zidisha hicho kisa na ukubwa (kwa maana ya eneo) la kiwanja husika, hii ni kwa Dar es salaam na maeneo mengine ya nchi yenye hadhi ya miji na majiji. Kwa Masaki, Upanga and the like; kwa mita square moja hupati kiwanja chini ya Tshs. 1,500.000. Kwa hiyo soko huria ndivyo lilivyo.

Tuje kwa serikali; serikali ya Tanzania imekuwa ikiuza ardhi na kuitoza kodi ardhi kwa bei ya kutupa kabisa, mleta mada kama uamini, hilo eneo unalo lalamika, hemu jaribu kuuliza kwa soko huria kiwanja bei gani, kwenye eneo hilo hilo. Tuache milawama ya ajabu na muda mwingine tuisifu serikali hasa kwenye kuhakikisha raia wake wanapata makazi yao wenyewe.

This is absurd,
Swali ni Je who is your targeted customer? Mambo ya cost za survey kuwa juu nao ni upuuzi mwingine. Wafanyakaz wa mamlaka za ardhi wanalipwa kwa kazi gani?

Its very unfair ardhi kuwa ghali kiasi hiki,hasa kwa watanzania wenye kipato HALALI.

Nisingekua na haja ya kununua ardhi kama NHC nao wangeuza au kupangisha nyumba kwa fair cost..lakini huko nako ni vituko tu kwa watu wenye vipato HALALI.

Swali linabaki, Who FOR REAL is your targeted customer?
OTHERWISE WATU WOTE TUGEUKE WAJASIRIAMALI, full ujanja ujanja
 
Gvt plots are the cheapest though not affordable. Plot price is the summation of land acquits ion cost, survey costs, title deed preparation costs plus a premium of less than 15% call it a profit but in actual sence it serves as a revolving fund for future projects. If you are to pay a fair compensation, there is no way plots are going to be cheap because the two are dependent but very much opposing each other.
my opinion, we need to change our perspective, let the Nhc, NSsf, ppf etc construct as many houses as possible and float in the market for lease- purchase (call it mortgage), tuachane na ufahari wa kujenga nyumba wenyewe, hii biashara ndo kwanza inachangia ufisadi kwa kiwango kikubwa. Tax very very heavily private property developers, I'm telling you mwisho wa siku stress za nyumba zitapungua, wanaostahili (matajiri) kujenga nyumba watajenga wenyewe Si wengine tutaendelea

Kama ikifika wakati wa kupata huduma gharama zote anatwishwa mla huduma, je kodi yangu ya PAYEE miaka 15 sasa isiyopungua 1mil kila mwezi inanisaidia wapi??? basi kodi za VAT na zingine serikali isichukue ili huduma inapoombwa ilipiwe kikamilifu. Kodi zetu za magari, mafuta vipuri nk ndo zinatakiwa kumudu gharama kama hizo. Pesa za Madini zinaenda wapi kama tukitaka huduma toka serikali tunalipia kila kitu hapo hapo, naomba mfikirie sana kabla ya kusapoti ujingaaaaaaa
 
sasa hivi kila halmashauri inakimbilia kupima viwanja lakini wenye ardhi wanalipwa pesa ndogo sana gharama ya kupima kiwanja kimoja haizidi laki mbili hayo ni makisio ya juu sana lakini cha ajabu bei ya kiwanja kimoja nizaid ya milioni tatu wakati watanzania wengi kipato chao ni cha chini pia idadi ya fomu zinazotolewa ni zaidi ya idadi ya viwanja hizo pesa za ziada zinaenda kufanya nini
waziri wa ardhi kwa sababu yupo hapa tunaomba atoe ufafanuzi
 
kinachonisikitisha.ni mipango ya hio viwanja mipango miji hawapo ka.bisa hebu fikiria viwanja huwa wanapanga hapa makazi hapa biashara subiri miaka miwili ipite ndio utajua hakuna serikali...eneo la makazi pamejengwa petrol station au godown
 
walanguzi wameingia ubia na Halmashauri kutufanya walalahoi tusiwe na uwezo wa kununua viwanja,Tanzania viwanja kwa Matajiri tu!
 
Inasikitisha sana kuona mtanzania hana fursa nzuri ya kujenga makazi bora kutokana na dhana mbaya ya serikali ya kuggeuza ardhi kuwa mtaji mkubwa wa mapato ya kuendesha nchi, yaani haki mojawapo ya makazi kati ya nne za maji, chakula, makazi, mavazi inagandamizwa kwa kasi kubwa.

Hebu tujiulize kwanini bei ya kiwanja iwe kubwa kuliko kipato cha mfanyakazi wa kima cha chini kwa mwaka mzima??? kweli sera za CCM zinaakili??? yuko wapi Filiku
njombe, yuko wapi Makamba January, yuko wapi Mama Anne Kilango, yuko wapi Sitta yuko wapi Mwakyembe, yuko wapi Waziri anayehusika na Makazi, Yuko wapi waziri wa Ardhi, Yuko wapi waziri wa maendeleo ya jamii, yuko wapi Waziri MKUU, yuko wapi RAIS???????

Zaidi yote yuko wapi Mbunge, ambaye tunamlalamikia kila siku kuhusu bei ghali ya viwanja, aliyeahidi kwenda kuongea matatizo yetu bungeni yuko wapi???

Je hata ardhi ambayo mungu katupatia bure nayo inashindikana kuigawa kwa watanzania ili wajenga makazi bora, inakuwa suala la tajiri hata na hili? kulala sehemu nzuri imekuwa luxury????

Ushauri wangu kila mtu apewe kiwanja kwa bei ya laki 1-5 tu, serikali ivunje mtandao wa ulanguzi wa viwanja; ardhi sio biashara, iweje mtu anachukua viwanja 50 ili auze kwa bei ghali, udhaifu wa serikali ukome sasa. Mbaya zaidi wakati wa magufuli alidai hata naibu wake RM alikwa na viwanja vingi vingi amejilimbikizia.

Unyonge wetu ututoke kwanza ndo tusitahili haki. TUUNGANE KUPAMBANIA HAKI YA MAKAZI BORA

Mzee hamia Tandahimba , huko ardhi bwerere na siajabu ukichimba msingi waweza kupata gesi!
 
I like kuhamia Tandahimba, kama viwanja ni vya tajiri pekee, sie masikini chetu kipi? mbona ndo mali mungu katupa tukiwa uchi wa mnyama???
 
"Makuwadi Wa Soko Huria" watakwambia bei ya kiwanja Kisarawe kwa Chamgui au Mkuranga Bombani si kubwa hivyo na ukitaka kiwanja bei rahisi nenda Kisarawe. Na mjini kama bei ni kubwa sana, watu watashindwa kununua na bei zitashuka zenyewe.

Na kama zinaendelea kuwa hizo hizo, maana yake watu hawashindwi kununua.

Na kama watu hawashindwi kununua, basi bei si kubwa.

Watamnukuu mpaka Adam Smith na kusema "price is a function of demand and supply". Kama wewe una ubavu wa kununua Kisarawe ambako laki unapata kiwanja kizuri ukitaka kununua Oysterbay "laki si pesa, fungu la biskuti za mbwa" ambako viwanja/nyumba vinafika kwenye mamilioni ya dola utataka kujiumiza roho tu.

Kama hizi bei si sawa zitashuka tu kama a "real estate bubble" needing a correction.

Hao wabunge waambieni waondoe sheria za eminent domain wananchi wamiliki (as opposed to kukodi kulipo sasa) ardhi, mtaona makampuni makubwa ya real estate yanajenga nyumba utitiri na kufanya ushindani ushushe chini bei za nyumba na kuifanya process ya kununua ardhi iwe standardized, ikiwa ni pamoja na bei za viwanja, credit system and mortgages.

Leo hii makampuni makubwa hayawezi kuja kufanya biashara ya real estate kwa sababu yanaogopa clauses za kukodi ardhi kwa miaka 33, 66 na 99 zinazoipa serikali umiliki wa ardhi na wao kuwa wapangaji tu (bongo hakuna kumiliki ardhi, kuna kukodi tu kwa Kikwete mmiliki mwenyewe)

Badilisheni haya ya msingi kuondoa umangimeza mengine yatajitengeneza.

Na badilisheni kwa akili kuepuka serfdom kama Kenya.
 
Back
Top Bottom