Mwakalinga Bujo
JF-Expert Member
- Oct 22, 2008
- 2,719
- 1,440
Inasikitisha kuwa zaidi ya miaka 50 ya uhuru moja ya muhimili wa dola Mahakama inatumia lugha ya wakoloni (kingereza) kama lugha ya mawasiliano(kuandika hukumu) .Inashangaza kuona hukumu zinaandikwa kwa kingereza kwa kigezo kuwa lugha ya kisheria ni ya kitaalamu mno hivyo kuitafsiri kiswahili ni vigumu.
Haitoshi, pale ambapo mtuhumiwa/msomewa hukumu haelewi kingereza basi Hakimu/Jaji anamwelewesha kwa kiswahili.Swali la kujiuliza Je, hayo maneno ya kumwelewesha msomewa hukumu kwa kiswahili yatoka wapi ? ama ni upotoshaji unatumika kwa makusudi kupindisha mambo?.Ama ni ufinyu wa bajeti !!?
Mambo/maswali ya msingi ya kutafakari kwenye muhimili huu muhimu wa dola kwa miaka zaidi ya 50
1.Mahakama zipo kuwahudumia kina nani?
2.Wanaohudumiwa wanajua lugha gani kwa ufasaha?
Napenda kujua zaidi ya kidogo nachojua ,hivyo naomba kueleweshwa kulingana na mada.
Nawasilisha
Haitoshi, pale ambapo mtuhumiwa/msomewa hukumu haelewi kingereza basi Hakimu/Jaji anamwelewesha kwa kiswahili.Swali la kujiuliza Je, hayo maneno ya kumwelewesha msomewa hukumu kwa kiswahili yatoka wapi ? ama ni upotoshaji unatumika kwa makusudi kupindisha mambo?.Ama ni ufinyu wa bajeti !!?
Mambo/maswali ya msingi ya kutafakari kwenye muhimili huu muhimu wa dola kwa miaka zaidi ya 50
1.Mahakama zipo kuwahudumia kina nani?
2.Wanaohudumiwa wanajua lugha gani kwa ufasaha?
Napenda kujua zaidi ya kidogo nachojua ,hivyo naomba kueleweshwa kulingana na mada.
Nawasilisha