Kwa nini bei ya cement iko juu sana hapa Tanzania ??

Mu-Israeli

JF-Expert Member
Mar 21, 2012
2,454
975
Hi wana JF wote.
Najiuliza sana kwa nini bei ya cement iko juu sana hapa Tanzania.
Najiuliza hivyo kwa sababu naona kuna cement toka nje ya nchi inakuja na kuuzwa kwa bei nafuu kuliko cement inayozalishwa hapa Tanzania.
Hiyo cement inayotoka nje imezalishwa kama cement yetu hapa, imesafirishwa, imelipiwa kodi, imelipiwa bima ya usafirishaji, n.k. halafu bado ni nafuu kuliko cement yetu !!!???
Nimeangalia bei za cement za nchini Pakistan ambako ndio inatoka cement nyingi inayoletwa hapa Tanzania.
Bei ya tani moja ya cement ni dola za kimarekani (USD) 62.00 kwa tani (ukinunua huko). Pia bei pamoja na usafirishaji mpaka bandari ya Dar es Salaam au Mombasa ni USD 90.21 kwa tani.
Bei hizo ukizibadilisha kuwa shilingi ni kama ifuatavyo:-
USD 62.00 = Tzs 99,200 kwa tani, ambayo ni Tzs. 4,960 kwa mfuko wa kilo 50.(Ukinunua kule Pakistan bila kusafirisha)
USD 90.21 = Tzs 144,336 kwa tani, ambayo ni Tzs. 7,218 kwa mfuko wa kilo 50 (bei pamoja na usafiri toka Pakistan mpaka Dar es Salaam).
Swali:-
Kinachofanya bei za cement zinazozalishwa Tanzania kuwa juu sana (Tzs. 12,000 au zaidi kwa mfuko wa kilo 50) ni nini ??

Visit: http://www.alibaba.com/product-free/107472674/Cement_52_5_in_20_ft.html
 
Hi wana JF wote.
Najiuliza sana kwa nini bei ya cement iko juu sana hapa Tanzania.
Najiuliza hivyo kwa sababu naona kuna cement toka nje ya nchi inakuja na kuuzwa kwa bei nafuu kuliko cement inayozalishwa hapa Tanzania.
Hiyo cement inayotoka nje imezalishwa kama cement yetu hapa, imesafirishwa, imelipiwa kodi, imelipiwa bima ya usafirishaji, n.k. halafu bado ni nafuu kuliko cement yetu !!!???
Nimeangalia bei za cement za nchini Pakistan ambako ndio inatoka cement nyingi inayoletwa hapa Tanzania.
Bei ya tani moja ya cement ni dola za kimarekani (USD) 62.00 kwa tani (ukinunua huko). Pia bei pamoja na usafirishaji mpaka bandari ya Dar es Salaam au Mombasa ni USD 90.21 kwa tani.
Bei hizo ukizibadilisha kuwa shilingi ni kama ifuatavyo:-
USD 62.00 = Tzs 99,200 kwa tani, ambayo ni Tzs. 4,960 kwa mfuko wa kilo 50.(Ukinunua kule Pakistan bila kusafirisha)
USD 90.21 = Tzs 144,336 kwa tani, ambayo ni Tzs. 7,218 kwa mfuko wa kilo 50 (bei pamoja na usafiri toka Pakistan mpaka Dar es Salaam).
Swali:-
Kinachofanya bei za cement zinazozalishwa Tanzania kuwa juu sana (Tzs. 12,000 au zaidi kwa mfuko wa kilo 50) ni nini ??

Visit: http://www.alibaba.com/product-free/107472674/Cement_52_5_in_20_ft.html
...Mkuu kuna mikono michafu y watu....
Malawi na Zambia, bei ya diezel ni Tshs 750/= ni mafuta yaleyale yanayokatisha hapa Ubungo.
je, si zaidi sana Cement toka Afghanstan?
 
kwakweli inaudhi sana
ngoja waje wanaofahamu labda kuna sababu
 
Bei ni function ya vitu vingi sana mkuu, siyo transport peke yake! kuna kodi mbalimbali, mkono wa serikali, rushwa, purchasing power ya wateja wako n.k. Hivyo u-compare bei za nchi moja na nyingine utakuwa unakosea sana!
 
Soko huru!! We tazama bei za viwanja ama nyumba/banda watu wakiweka humu!! havina sheria kwamba maximum price kwa eneo hili ni hivi!! utakuta mtu anaweka kiwanja ama shamba kuuza kisha kwenye bei anabofya namba anayojisikia kobofya kisha anaweka kidole kwenye sifuri mpaka asikie sound ya compyuta kwamba sasa imegota!! hio ndio bei!!

Sasa mkuu huko kwenye cement panataka ufafanuzi wa ndani kwa wale wenye elimu hio wache watumwagie tu humu. cha ajabu cement inapatikana hapa tunazalisha wenyewe ila bei ni ya juu kuliko ile bei tunayowauzia huko nje kwa export!! tazama mfano tu wakati wa South Africa world cup cement ilivyopanda bei kwa wananchi hapa nchini na bei tuliyowauzia makaburu ukiambiwa unaweza kutapika. ngoja ntoke ntarudi
 
dollar kila siku inapanda dhidi ya shilingi yetu na mfumuko wa bei kila siku unapanda kwa sababu wanauchumi wetu waliacha vichwa chuo kikuu. wakamua kuvaa vichwa vingine vya kudanganya yaani siasa. hawazungumzii na kupanga mkakati namna ya kukusanya kodi kutoka kwa hao wanaokufuru badala yake wanawaachia TRA NA SERKALI ZA MITAA watusokote shingo sisi wanyonge. wakubwa wakillipa kodm,i maduka ya fedha za kigeni yakisimamiwa ipasavyo,, madini yetu yakilindwa,, biashara zetu zikilindwa cement badala ya kupanda bei iiashuka au kubaki pale kwa kipindi kirefu
 
Back
Top Bottom