Gangongine
JF-Expert Member
- Dec 31, 2015
- 3,854
- 1,776
Nawasihi sana Vijana mlio na matarajio ya kile mnachokiita UKAWA kwamba mtachukua Nchi kwa siku za karibuni mfute kabisa mawazo hayo kwa
ni itawachukua muda mrefu kufikia ndoto hizo kwa sababu zifuatazo:-
(a) Hakuna Kiongozi wa Upinzani mwenye nia ya dhati wala mipango ya kwenda IKULU. CDM walikuwa wanakaribia kwenda IKULU kama siyo tama yao ya kutoandaa Mgombea anayekijua Chama chao na mwenye uzoefu wa kutosha katika Siasa za Upinzani. Ndio maana walikosa kujiamini na kuitupa LULU yao dakika za majeruhi.
(b) Hakuna mikakati ya Kisiasa itakayowashawishi wananchi wavipe ridhaa Vyama hivyo kwa kuwa badala ya kunadi Sera wanapoteza muda kunadi makosa ya CCM ambayo hata wao wakiingia madarakani watayafanya tu.
(c) Mtandao wa Upinzani kwenye ngazi ya Vijiji, Kitongoji na Mtaa bado ni dhaifu tofauti na CCM ambayo ina balozi wa nyumba kumi. Kura za Lowassa hazikutokana na Wananchi kuipenda UKAWA bali chuki zao baada ya mtu waliyeamini ni Mgombea bora na aliyekuwa amewekeza kwa muda mrefu kukatwa dakika za majeruhi. Sasa CCM kumetulia na kura za namna hiyo hazitapatikana tena 2010. Natabiri hata kura milioni 2 Wapinzani hawatapata 2020.
(d) Kujichanganya kwa Wapinzani kuhusu Sera wanazosimamia. Angalau wakati wa Dr. Slaa wananchi walijua alichokuwa akikisimamia na wananchi walianza kumuamini. Kwa sasa hata Katibu Mkuu sijui anaitwa nani hata Wananchi hawamjui kabisa na sijui anafanya kazi gani. Ushauri mzuri kwa Vijana ni kwamba msipoteze nguvu zenu mahali ambapo hamtavuna chochote.Rejeeni CCM maana ndio Chama kilichoaminiwa, kinachoaminiwa na kitakachoendelea kuaminiwa kwa muda mrefu mbeleni.
UKWELI NI KWAMBA HAKUNA UPINZANI WA KWELI TANZANIA NDIO MAANA HATA BUNGENI BADALA YA KUJIBU AU KUPAMBANA NA HOJA ZA CCM WABUNGE WENU WANAKIMBIA NA KUSUSA MAANA HAWANA CHA KUONGEA. WANAPIGANIA HOJA ZA OVYO KAMA BUNGE KUONESHWA "LIVE" BADALA YA KUIBANA SERIKALI IPELEKE MAJI, BARABARA, UMEME, HUDUMA ZA AFYA, ELIMU N.K .
AMKAENI VIJANA MSIKUBALI KKUDANGANYWA KUANDAMANA NA KUPAMBANA NA DOLA MAANA HAMTOFANIKIWA ZAIDI YA KUPATA MADHARA NA VIONGOZI WENU HAWATAWASAIDIA KAMWE!!
ni itawachukua muda mrefu kufikia ndoto hizo kwa sababu zifuatazo:-
(a) Hakuna Kiongozi wa Upinzani mwenye nia ya dhati wala mipango ya kwenda IKULU. CDM walikuwa wanakaribia kwenda IKULU kama siyo tama yao ya kutoandaa Mgombea anayekijua Chama chao na mwenye uzoefu wa kutosha katika Siasa za Upinzani. Ndio maana walikosa kujiamini na kuitupa LULU yao dakika za majeruhi.
(b) Hakuna mikakati ya Kisiasa itakayowashawishi wananchi wavipe ridhaa Vyama hivyo kwa kuwa badala ya kunadi Sera wanapoteza muda kunadi makosa ya CCM ambayo hata wao wakiingia madarakani watayafanya tu.
(c) Mtandao wa Upinzani kwenye ngazi ya Vijiji, Kitongoji na Mtaa bado ni dhaifu tofauti na CCM ambayo ina balozi wa nyumba kumi. Kura za Lowassa hazikutokana na Wananchi kuipenda UKAWA bali chuki zao baada ya mtu waliyeamini ni Mgombea bora na aliyekuwa amewekeza kwa muda mrefu kukatwa dakika za majeruhi. Sasa CCM kumetulia na kura za namna hiyo hazitapatikana tena 2010. Natabiri hata kura milioni 2 Wapinzani hawatapata 2020.
(d) Kujichanganya kwa Wapinzani kuhusu Sera wanazosimamia. Angalau wakati wa Dr. Slaa wananchi walijua alichokuwa akikisimamia na wananchi walianza kumuamini. Kwa sasa hata Katibu Mkuu sijui anaitwa nani hata Wananchi hawamjui kabisa na sijui anafanya kazi gani. Ushauri mzuri kwa Vijana ni kwamba msipoteze nguvu zenu mahali ambapo hamtavuna chochote.Rejeeni CCM maana ndio Chama kilichoaminiwa, kinachoaminiwa na kitakachoendelea kuaminiwa kwa muda mrefu mbeleni.
UKWELI NI KWAMBA HAKUNA UPINZANI WA KWELI TANZANIA NDIO MAANA HATA BUNGENI BADALA YA KUJIBU AU KUPAMBANA NA HOJA ZA CCM WABUNGE WENU WANAKIMBIA NA KUSUSA MAANA HAWANA CHA KUONGEA. WANAPIGANIA HOJA ZA OVYO KAMA BUNGE KUONESHWA "LIVE" BADALA YA KUIBANA SERIKALI IPELEKE MAJI, BARABARA, UMEME, HUDUMA ZA AFYA, ELIMU N.K .
AMKAENI VIJANA MSIKUBALI KKUDANGANYWA KUANDAMANA NA KUPAMBANA NA DOLA MAANA HAMTOFANIKIWA ZAIDI YA KUPATA MADHARA NA VIONGOZI WENU HAWATAWASAIDIA KAMWE!!