Uwezo Tunao
JF-Expert Member
- Nov 14, 2010
- 6,942
- 1,190
Mpango wa serikali kuvipa vyama vya siasa RUZUKU ni sawa kabisa kwa kuwa ni vyama vyetu sisi wenyewe. Lakini, maswali yote yatakua yamejibiwa juu ya zoezi hili ipasavyo??
Labda nanze kwa kuuliza kwamba je, hizi fedha za RUZUKU KWA VYAMA VYA SIASA zitatolewa na Serikali gani ukizingatia ukweli kwamba WIZARA YA FEDHA si swala la Muungano. Hebu tuwekane sawa hapa.
Naona CUF ina wabunge wengi Visiwani, chini ya Serikali ya Zanzibar ambayo ina Wizara yake ya Fedha, kuliko hali halisi ilivyo huku bara. Nayo CCM ina Wabunge wengi zaidi Bara, ambako nako kuna Wizara yake ya Fedha, kuliko hali halisi ilivyo kule visiwani. Sasa ulipaji wa ruzuku hizi zitakuekoje hapo??
HOJA YANGU:
Wenye habari zaidi tujuzeni kama Mkaguzi Mkuu wa Fedha na Matumizi ya Serikali Tanzania, Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Msajili wa Vyama Mzee John Tendwa na wenyeviti wenyewe wa Vyama Tanzania wamekwishaliona UTATA huu.
Kusije kukatokea vyama fulani KULA DABO Bara na Visiwani au Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kuubeba mzigo wote wa kulipa vyama vya siasa ruzuku kwa kujumuisha na wabunge wa Bara ambao hawana faida kwao visiwani.
Labda nanze kwa kuuliza kwamba je, hizi fedha za RUZUKU KWA VYAMA VYA SIASA zitatolewa na Serikali gani ukizingatia ukweli kwamba WIZARA YA FEDHA si swala la Muungano. Hebu tuwekane sawa hapa.
Naona CUF ina wabunge wengi Visiwani, chini ya Serikali ya Zanzibar ambayo ina Wizara yake ya Fedha, kuliko hali halisi ilivyo huku bara. Nayo CCM ina Wabunge wengi zaidi Bara, ambako nako kuna Wizara yake ya Fedha, kuliko hali halisi ilivyo kule visiwani. Sasa ulipaji wa ruzuku hizi zitakuekoje hapo??
HOJA YANGU:
Wenye habari zaidi tujuzeni kama Mkaguzi Mkuu wa Fedha na Matumizi ya Serikali Tanzania, Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Msajili wa Vyama Mzee John Tendwa na wenyeviti wenyewe wa Vyama Tanzania wamekwishaliona UTATA huu.
Kusije kukatokea vyama fulani KULA DABO Bara na Visiwani au Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kuubeba mzigo wote wa kulipa vyama vya siasa ruzuku kwa kujumuisha na wabunge wa Bara ambao hawana faida kwao visiwani.