Kwa kilichonikuta leo, nashauri kuwekwe vifaa vya kuhifadhia uchafu/takataka kila baada ya mita 100

Stephen Ngalya Chelu

JF-Expert Member
Oct 31, 2017
7,621
16,373
Habarini wana jamiifoorums

Leo mida ya saa 7 nilitoka gheto nikaelekea zangu mwenge vinyago kwenda kucheki ishu fulani hivi. Na wakati naondoka gheto nilipita dukani nikanunua maji. Nikafika mwenge maji yakiwa yamebaki kidogo nikafanya ishu yangu niliyokuwa nimefuata nikaanza na nikamalizia pia maji yaliyokuwa yamebaki kwa chupa.

Kimbembe kikaja ni wapi naitupa hiyo chupa, nilijaribu kuangalia sehemu ya kutupa lakini sikuona. Nikasema ngoja nitembee kutoka pale nilipokuwa kuelekea makumbusho kwa kutumia barabara ya bagamoyo huenda nikapata pa kuhifadhi ile chupa. Cha kushangaza nimetembea kutoka mwenge hadi makumbusho stand sijaona sehemu maalum ya kuhifadhi uchafu. Ikabidi niibinyebinye ile chupa niiweke kwenye mfuko wa suruali ili nikaiweke katika chombo cha takataka gheto. Sasa hivi nipo kwenye gari na chupa langi mfukoni kisa tu hakuna sehemu za umma za kuhifadhi uchafu. Na hii si mara ya kwanza, nimeshawahi kurudi na maganda ya machungwa, mifuko ya rambo, na uchafu mwingine kwa kuwa sikuona mahala pa kutupa.

Ushauri wangu: Mamlaka ya majiji na miji iangalie uwezekano wa kuweka trash bins (sijui ndo huitwa hivyo😀😀😀) kila baada ya mita 100 au 150 hasa pembezoni mwa barabara, hii itasaidia kupunguza tatizo la uchafu kutupwatupwa hovyo. Kuweka sheria bila kuweka miundombinu wezeshi ni bure kabisa.

Nakumbusha: niko na chupa la maji mfukoni hapa😀😀😀😀
 
Habarini wana jamiifoorums

Leo mida ya saa 7 nilitoka gheto nikaelekea zangu mwenge vinyago kwenda kucheki ishu fulani hivi. Na wakati naondoka gheto nilipita dukani nikanunua maji. Nikafika mwenge maji yakiwa yamebaki kidogo nikafanya ishu yangu niliyokuwa nimefuata nikaanza na nikamalizia pia maji yaliyokuwa yamebaki kwa chupa.

Kimbembe kikaja ni wapi naitupa hiyo chupa, nilijaribu kuangalia sehemu ya kutupa lakini sikuona. Nikasema ngoja nitembee kutoka pale nilipokuwa kuelekea makumbusho kwa kutumia barabara ya bagamoyo huenda nikapata pa kuhifadhi ile chupa. Cha kushangaza nimetembea kutoka mwenge hadi makumbusho stand sijaona sehemu maalum ya kuhifadhi uchafu. Ikabidi niibinyebinye ile chupa niiweke kwenye mfuko wa suruali ili nikaiweke katika chombo cha takataka gheto. Sasa hivi nipo kwenye gari na chupa langi mfukoni kisa tu hakuna sehemu za umma za kuhifadhi uchafu. Na hii si mara ya kwanza, nimeshawahi kurudi na maganda ya machungwa, mifuko ya rambo, na uchafu mwingine kwa kuwa sikuona mahala pa kutupa.

Ushauri wangu: Mamlaka ya majiji na miji iangalie uwezekano wa kuweka trash bins (sijui ndo huitwa hivyo) kila baada ya mita 100 au 150 hasa pembezoni mwa barabara, hii itasaidia kupunguza tatizo la uchafu kutupwatupwa hovyo. Kuweka sheria bila kuweka miundombinu wezeshi ni bure kabisa.

Nakumbusha: niko na chupa la maji mfukoni hapa
ROCK CITY amna ishu kama izo jiji la wasafiiii
tapatalk_1538727372046.jpeg
 
\Muulize makonda yuko busy anakagau mik*** badala ya kushughulikia mambo kama hayo
 
  • Thanks
Reactions: y-n
Kwanini usingewapatia waokota makopo?
Hilo ndo suluhisho la kudumu? Kwamba jiji kubwa kama hili tutegemee kutunza uchafu kwa waokota makopo? Na vipi uchafu mwingine usio chupa za plastiki kama magunzi ya mahindi, maganda ya matunda na mwingineo tuwape akina nani?

Panatakiwa suluhisho la kudumu hapa.
 
Inaboa..mi mwenyewe leo nmerudi na kakopo kangu..
Nafsi ishakataa kutupa hovyo.
 
Kwan ile kampeni ya bashite ya Dar yangu (sijui ndo aliita hivyo..?!) Au ndo kama kawaida yake anaanzisha kitu then kinaishia juujuu tu..!
 
Uko sahihi kaka.
Hata mimi nimeshafanya hili mara nyingi tu. Bora hata kama unapanda daladala utaweka kwenye dustibin ya ndani ila kwa watembea kwa miguu ni kero tu.
 
Usafi ni culcture, kuwa msafi ni jambo moja na kuishi mahala pasafi ni jambi jingine. Kuweka namna ya kutunza usafi ili mazingira unayoishi yame na yaonekane masafi ndo usafi wenyewe.

Sijui nimeongea nilichokuwa namaanisha au nimeongea kama ile misemo tuliyofundishwa na wakoloni enzi zile....

Betty Billy bought a bit of butter but a bit of butter was bitter. so Betty Billy bought a bit of better butter to make bitter butter better. Iseme hii sentinsi haraka haraka bila kukosea.
 
Inaboa..mi mwenyewe leo nmerudi na kakopo kangu..
Nafsi ishakataa kutupa hovyo.
kweli mkuu, nilikuwa naona machupa mitaroni lakini wengine ujasiri wa kufanya hivyo hatuna, mtu unatupa kopo barabarani na hujihisi vibaya. Tunatofautiana sana asee.
 
Karibu Moshi,hakuna huo ujinga,na nyie wanaume Wa dar mnakubali kukaguliwa m**** wkt sehem za kuhifadhi Hamna!?
Habarini wana jamiifoorums

Leo mida ya saa 7 nilitoka gheto nikaelekea zangu mwenge vinyago kwenda kucheki ishu fulani hivi. Na wakati naondoka gheto nilipita dukani nikanunua maji. Nikafika mwenge maji yakiwa yamebaki kidogo nikafanya ishu yangu niliyokuwa nimefuata nikaanza na nikamalizia pia maji yaliyokuwa yamebaki kwa chupa.

Kimbembe kikaja ni wapi naitupa hiyo chupa, nilijaribu kuangalia sehemu ya kutupa lakini sikuona. Nikasema ngoja nitembee kutoka pale nilipokuwa kuelekea makumbusho kwa kutumia barabara ya bagamoyo huenda nikapata pa kuhifadhi ile chupa. Cha kushangaza nimetembea kutoka mwenge hadi makumbusho stand sijaona sehemu maalum ya kuhifadhi uchafu. Ikabidi niibinyebinye ile chupa niiweke kwenye mfuko wa suruali ili nikaiweke katika chombo cha takataka gheto. Sasa hivi nipo kwenye gari na chupa langi mfukoni kisa tu hakuna sehemu za umma za kuhifadhi uchafu. Na hii si mara ya kwanza, nimeshawahi kurudi na maganda ya machungwa, mifuko ya rambo, na uchafu mwingine kwa kuwa sikuona mahala pa kutupa.

Ushauri wangu: Mamlaka ya majiji na miji iangalie uwezekano wa kuweka trash bins (sijui ndo huitwa hivyo) kila baada ya mita 100 au 150 hasa pembezoni mwa barabara, hii itasaidia kupunguza tatizo la uchafu kutupwatupwa hovyo. Kuweka sheria bila kuweka miundombinu wezeshi ni bure kabisa.

Nakumbusha: niko na chupa la maji mfukoni hapa
 
Back
Top Bottom