Kwa kasi ya Mchina na Electric Vehicles (EV), sio muda tutapishana nazo Dar

Ni kweli lakini gari una charge tu inakwenda hakuna cha kuweka mafuta hio huoni kimahesabu ni nafuu sana, halafu lifespan ya battery si kwamba kila mwaka unabadili, ukifanya mahesabu utagundua gari ya mafuta ina gharama kiuendeshaji.

Mfano mtu anayeendesha Fortuner au V8 vipi akitumia SUV ya umeme, ameokoa pesa kiasi gani..
Gari ya umeme ni expensive Kuliko gari ya mafuta, labda kama unazungumzia Bajaji na piki piki au gari inayozunguka posta na karikaoo pekee na Mwenge au Sinza
 
Hydrogen is one of the most abundant element and is the future of energy in transportation.
EV is just another scam like others..ukifuatilia ev vehicles Zina uharibifu zaidi wamazingira kwa kupima vyanzo vya betri zake, disposal na upatikanaji wa madini yanayotumika katika uundani wake na source ya umeme unaotumika.

Toyota hili wamelitambua mapema..
Wanaharibu Mazingira Africa wanatunza ya kwao... EV ni scam Fulani hivi ila Watu tunapenda vitu vya Kisasa
 
Issue Iko kwenye ku replace battery ikiisha hapo mziki ndio upo
Electric car battery replacement costs outside of warranty can range from $6,500 to $20,000
Hizo bei ni kwa genuine battery toka kiwandani, ngoja nikuulize unajua bei ya engine ya ist brand new toka kwa toyota wenyewe? Je bongo hii nani angeiweza? Lakini sasa hivi chini ya 2mill unabadili engine kwa mitumba na spea za kichina kibao mtaani. Juzi nlikuwa natafuta genuine engine block ya pikipiki yamaha 4gl ya cc90, za kichina 25,000 huku mitaani, ila original kwenye mtandao wa Katayama japan ni 500,000 bado usafiri, battery za hizi gari za hybrid hapo nairobi kuna jamaa wanauza cell moja laki moja ya tanzania, na gari nyingi hybrid wana cells hadi 30, na watu wanapima ipi cell iko weak na inakuwa replaced maisha yanasonga, sasa wafikir battery itakuwa ni tabu? Wait and see
 
Battey zake ni ghari kuliko gari lenyewe na zina lifespan
Battery ni ghali ila sio kuliko gari lenyewe. Tumeona mfano hapo juu kwenye Tesla Model 3.

Na pia lifespan ilikua magari ya umeme ya zamani mfano Nissan Leaf, ila Tesla battery yake tumetoa mfano apo inaweza kukaa miaka 22 na kuendelea.

Imagine.
 
Battery ni gari ila sio kuliko gari lenyewe. Tumeona mfano hapo juu kwenye Tesla Model 3.

Na pia lifespan ilikua magari ya umeme ya zamani mfano Nissan Leaf, ila Tesla battery yake tumetoa mfano apo inaweza kukaa miaka 22 na kuendelea.

Imagine.
Sasa kuliko kununua battery si bora ununue gari jipya?
 
Umeshawahi kuuliza gharama za betri, betri replacement inacost 150% ya original cost ya Tesla.

Vipi kuhusu moto, hisi gari zikiwaka moto hata uitumbukize baharini haizimiki inaendelea kuungua hadi iishe.

Do your research on after market issues.
 
Back
Top Bottom