Kwa hili, Rostam Aziz hutasameheka

WC,kwanza nashukuru kwa comments zako zote,ni very positive zenye lengo la kusaidia nchi..
Katika post yako hii labda nami nikuulize unadhani nchi yetu tatizo ni kukosekana kwa fedha?Unafikiri Bunge likiwa dogo ndio haya matatizo yatakwisha?unadhani hili ndio primary solution,nifafanulie and then tujadiliane kwa kina!
Regia,
Tatizo sio kukosekana kwa fedha. Ni jinsi tunavyozitumia bila kuwa na vipaumbele vyetu kama NCHI. Fedha nyingi sana zinaelekezwa kwenye siasa na wanasiasa kama wewe. Hapo nimetoa mfano wa ukubwa wa BUNGE letu la sasa na anasa zake ambazo wewe unazifahamu kwa sasa. Fikiria tuondoe viti maalum na kisha kila Halmashauri/ Manispaa/ mji uwe na Mbunge mmoja tu wa kuchaguliwa kama ilivyo Igunga. Tutakuwa tumeokoa kiasi gani cha fedha kwa mwaka? Pili ni ruzuku kwa vyama vya siasa. Kama makanisa, NGOs, misikiti na asasi nyingine zinajiendesha zenyewe kwa kutumia michango ya wanachama wao na njia zingine kwanini vyama vya SIASA vipewe kodi zetu hata tusio na vyama kujiendesha? Tutaokoa kiasi gani ruzuku hii isipolipwa kwa vyama hivi?
Sio hilo tu. Angalia na serikali yetu ilivyo pana na kubwa. Angalia vyeo vya kisiasa vinavyolipwa na gharama za kuviendesha. Tunavyoigharamia SIASA ndivyo huduma za kijamii zinavyodorora kwa kasi ya ajabu halafu unamtaka Rostam atumie utajiri wake kuijenga Igunga?
 
Yule jamaa jibaba aliye kodishwa kulia wakati rozitamu akitangaza kujivua Gamba mbona hatukumuona akishangilia ushindi au naye anaishi Mwanza.
 
Nimeamua kuandika habari hii baada ya kujishauri tangu nikiwa Igunga!

Rostam Aziz amekuwa Mbunge wa Igunga tangu mwaka 1994 ambapo mpaka sasa ni takribani miaka 17 chini ya uongozi wake. Nilikuwa sijawahi kufika Igunga kabla hivyo sikuifahamu ilivyo.Siku Rostam anajiuzulu alieleza mafanikio mengi aliyoyafanya Igunga nikadhani Igunga hali ni shwari na watu wanamaendeleo mazuri,nilivyofika sikuamini nilichokiona. Rostam alitudanganya. Katika tembea yangu yote hapa nchini sijawahi kuona Wananchi wanashida kama wa Igunga.

Mambo yafuatayo nimeyagundua katika jimbo la Igunga;

1. Wananchi wengi wa Jimbo la Igunga hawajui kusoma na kuandika mpaka vijana wadogo

2. Wananchi wengi wa Igunga wanatembea hadi Kilomita 13 kufuata maji kwenye Makomero tena maji yenyewe sio safi wala salama

3. Wananchi wengi wa Igunga wanatembea hadi Kilomita 10 kufuata shule,wengine wanaenda hadi 20

4. Kwenye kata nilizopita hawaelewi wala kuzijua shule za awali.

5. Wananchi wengi wanatembea umbalimrefu kufuata Zahanati na hayo majengo yenyewe ya Zahanati unaweza kulia.

6. Hakuna barabara za kuunganisha kijiji kimoja na kingine,njia zilizopo ni mapitio ya ng'ombe.

7. Wananchi wengi hawana vyoo wala hawana mpango wa Kujenga vyoo,wao wajenga mabafu tu yanayotumika kuogea na kujisadia haja ndogo,haja kubwa utajua mwenyewe.

8. Zipo Kata ambazo hazing mawasiliano ya simu

9. Lipo Kabila mpaka leo wanatembea uchi kama kwa King Muswati.

10. Wapo wanaotembea karibu Kilomita 13 kufuata TV waone taarifa ya habari na mambo mengine. Hii ni Kata anayotoka Dr. Kafumu

11. Na mengine mengi madogo madogo.

Rostam alikuwa na uwezo wa kupunguza hayo niliyoyataja kwasababu zifuatazo

1. Alikuwa ni Mbunge hivyo alikuwa na fursa ya kupiga kelele ndani na nje ya Bunge na akasililizwa.
2. Alikuwa Mbunge mwenye ushawishi ndani ya chama chake hivyo angeweza kushawishi Mawaziri ili miradi iende Jimboni kwake.
3. Alikuwa Mbunge tajiri sana,kama aliweza kuipa CCM,Mabilioni ya shillingi,Kama aliweza kuhonga watu mbalimbali mamilioni ya shilingi alishindwaje kusaidia Jimboni kwake? aliishia kuwanunulia tu simu Mabalozi wa Nyumba Kumi ili wamfanyie Kampeni.
4. Alikuwa anafahamiana na wafadhili wengi tu wa Maendeleo wa ndani na nje ya nchi alishindwaje kuwashawishi wawekeze kwake?

Rostam aliyaweza haya yote lakini hakujali kwakuwa hakuwa na lengo la kuwatumikia Wananchi wa Igunga. Kwasababu hizo basi nashawishika kusema kuwa Rostam ni zaidi ya DUBWANA ni mtu anayeongoza kwa roho mbaya hapa nchini. Hana huruma hata kidogo, anajali maslahi yake tu.. Bora ulivyojiuzulu, ungejiuzulu na utanzania kabisa, ukaombe uraia wa nchi nyingine huko ughaibuni sio Afrika!

Nawasilisha!
Duh!Nimeisoma hii nikapata goose bumps!Mbona hukugusia Kagoda,DOWANS etc?Kuna watu wana roho mbaya sijawahi kuona!Time is coming watakuwa held responsible.Sidhani kama wataachiwa hawa nchi ikipata uhuru wa kweli.Mtaji wa Taifa utapatikana kutoka kwa mafisadi wote.Wajiandae tu.
 
Mimi nawaombea hawa watu wapate pigo zaidi. Wana macho, hawaoni. Wana masikio, hawasikii. Wanamiguu lakini hawaendi.
Wale wote waliokuwa wanashinda kwenye mtandao sasa wanawacheka wanaigunga na kuwatimulia vumbi.
Nikiona watanzania wanavoumizwa kwa ujinga wao machozi hulenga lenga.[/QUOTE
Sio wote mkuu wapo watu wenye dhati ya kuikataa ccm lakini si umeona mizengwe ya uchaguzi ? kuna mtu alianzisha thread kuonyesha cdm ilivyokuwa na maadui wengi igunga mfano ccm, cuf, polisi, mkurugenzi, na wengine wengi ndio maana tunawajibika kuwapongeza wale wote waliochagua cdm mbali na vitisho ,ubaguzi wa kidini nk badala ya kuwalaumu mie nawaona kama mashujaa wataendelea kupata tabu lakini ni bora hawakuichagua ccm.

Umesahau NEC, Masheikh na waislamu. Kuna mama mmoja mfanyakazi wa NEC alikuwa anashangilia ushindi wa magamba kama hana akili nzuri.
 
Nasema mara nyingi humu tunaigharamia sana SIASA bila sababu. Kama mabilioni yaliyotajwa kwenye TD ya leo ni kweli mnashangaa nini Igunga kuwa katika hali hii? Eti dada Regia, CHADEMA peke yenu mmetumia milioni mianne (400,000,000/=) kutafuta ubunge wa Igunga pekee?

Hata kama mtu ni mjinga basi jaribu kuuficha mbele za watu usionekane. Hoja nyingine mtu unasema mengine. Kama Chadema imegharamia hizo pesa Igunga basi imarisha hoja yako ya kuwa tunagharamia sana siasa na utoe mifano ukiwamo huo wa Chadema ukianza kusema Chademe yenu, CCM yenu unakuwa unaharibu mjadala mzima, unatoka kwenye mada. Hapa linatafutwa suluhisho la nini kifanyike tutoke huku tulipo. Uwe Chadema uwe CCM ni dhahiri wote tunajua nchi nyetu ina hali mbaya sana katika nyanja muhimu za maisha zinazomfanya mtu aishi na kuusitiri utu wake. Uwe Chadema au CCM ukienda Igunga unatumia barabara ile ile. Ukiwa Chadema au CCM kama Igunga hakuna maji wote mnakosa maji. mgawo wa umeme tulio nao hauchagui Chadema wala CCM. Ajali za barabarani zinatuua kila siku hazichagu kama wewe ni CCM au Chadema. Tukitoa hoja kwa staha tutaheshimiana na tutajifunza kusikilizana na pengine kukubaliana katika mambo ya msingi kuhusu taifa letu. Taifa kwanza vyama baadae!
 
WC,unafikiri haya unayoyapendekeza yakifanyika,matatizo haya tunayoyapigia kelele yataondoka?kimsingi nakubaliana na hoja yako ila najaribu kutafakari kwa kina,kwamba leo nchi yetu ikiamua kupunguza ukubwa wa Bunge,Serikali n.k.Je hali tuliyonayo sasa ya umaskini itapungua kwa kiasi gani?


Regia,
Tatizo sio kukosekana kwa fedha. Ni jinsi tunavyozitumia bila kuwa na vipaumbele vyetu kama NCHI. Fedha nyingi sana zinaelekezwa kwenye siasa na wanasiasa kama wewe. Hapo nimetoa mfano wa ukubwa wa BUNGE letu la sasa na anasa zake ambazo wewe unazifahamu kwa sasa. Fikiria tuondoe viti maalum na kisha kila Halmashauri/ Manispaa/ mji uwe na Mbunge mmoja tu wa kuchaguliwa kama ilivyo Igunga. Tutakuwa tumeokoa kiasi gani cha fedha kwa mwaka? Pili ni ruzuku kwa vyama vya siasa. Kama makanisa, NGOs, misikiti na asasi nyingine zinajiendesha zenyewe kwa kutumia michango ya wanachama wao na njia zingine kwanini vyama vya SIASA vipewe kodi zetu hata tusio na vyama kujiendesha? Tutaokoa kiasi gani ruzuku hii isipolipwa kwa vyama hivi?
Sio hilo tu. Angalia na serikali yetu ilivyo pana na kubwa. Angalia vyeo vya kisiasa vinavyolipwa na gharama za kuviendesha. Tunavyoigharamia SIASA ndivyo huduma za kijamii zinavyodorora kwa kasi ya ajabu halafu unamtaka Rostam atumie utajiri wake kuijenga Igunga?
 
Hata kama mtu ni mjinga basi jaribu kuuficha mbele za watu usionekane. Hoja nyingine mtu unasema mengine. Kama Chadema imegharamia hizo pesa Igunga basi imarisha hoja yako ya kuwa tunagharamia sana siasa na utoe mifano ukiwamo huo wa Chadema ukianza kusema Chademe yenu, CCM yenu unakuwa unaharibu mjadala mzima, unatoka kwenye mada. Hapa linatafutwa suluhisho la nini kifanyike tutoke huku tulipo. Uwe Chadema uwe CCM ni dhahiri wote tunajua nchi nyetu ina hali mbaya sana katika nyanja muhimu za maisha zinazomfanya mtu aishi na kuusitiri utu wake. Uwe Chadema au CCM ukienda Igunga unatumia barabara ile ile. Ukiwa Chadema au CCM kama Igunga hakuna maji wote mnakosa maji. mgawo wa umeme tulio nao hauchagui Chadema wala CCM. Ajali za barabarani zinatuua kila siku hazichagu kama wewe ni CCM au Chadema. Tukitoa hoja kwa staha tutaheshimiana na tutajifunza kusikilizana na pengine kukubaliana katika mambo ya msingi kuhusu taifa letu. Taifa kwanza vyama baadae!
Siku zote wajinga kama mimi ndio huwa tunauliza maswali. Na hakuna ujinga mbaya kama kuuficha ujinga wenyewe. Kama unajua hauna haja ya kuuliza. TD ya leo inasema CCM wao wametumia zaidi ya 3bn! Haulioni hili kama linachangia hali ilivyo katika huduma za jamii kwa nchi yetu? Tusipovisema na kuvikemea vyama hivi tuendako sio kuzuri. Swali nililomuuliza Regia liko palepale.
 
Regia,
Tatizo sio kukosekana kwa fedha. Ni jinsi tunavyozitumia bila kuwa na vipaumbele vyetu kama NCHI. Fedha nyingi sana zinaelekezwa kwenye siasa na wanasiasa kama wewe. Hapo nimetoa mfano wa ukubwa wa BUNGE letu la sasa na anasa zake ambazo wewe unazifahamu kwa sasa. Fikiria tuondoe viti maalum na kisha kila Halmashauri/ Manispaa/ mji uwe na Mbunge mmoja tu wa kuchaguliwa kama ilivyo Igunga. Tutakuwa tumeokoa kiasi gani cha fedha kwa mwaka? Pili ni ruzuku kwa vyama vya siasa. Kama makanisa, NGOs, misikiti na asasi nyingine zinajiendesha zenyewe kwa kutumia michango ya wanachama wao na njia zingine kwanini vyama vya SIASA vipewe kodi zetu hata tusio na vyama kujiendesha? Tutaokoa kiasi gani ruzuku hii isipolipwa kwa vyama hivi?
Sio hilo tu. Angalia na serikali yetu ilivyo pana na kubwa. Angalia vyeo vya kisiasa vinavyolipwa na gharama za kuviendesha. Tunavyoigharamia SIASA ndivyo huduma za kijamii zinavyodorora kwa kasi ya ajabu halafu unamtaka Rostam atumie utajiri wake kuijenga Igunga?
Wild Card,most of times huwa unabwatuka mkuu.I mean ni kama unaongea kishabiki kufunika funika hoja za maana kwa kutumia upupu.Kwani CCM hawatozi ada za uanachama?Hawapati ruzuku tena kubwa kupindukia?Halafu bado michango ya mafisadi?Halafu bado panga la ufisadi ie EPA?Sasa ruzuku haiwatoshi?Ama michango ya ada za uanachama haiwatoshi?Michango ya wahindi nk je?Mkijiondolea ruzuku hilo gap mtaziba na kitu gani na nchi mmeshauza?Ama ulikuwa ukifikiria nini wakati unabandikia hii kitu?Unafananisha NGOs,makanisa na vyama vya siasa?Serikali iwe kubwa ama ndogo,kama ufisadi ndo sera unadhani kutakuwepo na mabadiliko?Kwani wanaofanya ufisadi ni wengi kihivyo?Unaweza kupunguza ukubwa wa serikali kwa kuwaondoa wale "kauzibe" ukabakiza mafisadi wote,whats the point?Ustuchanganye hapa.RA hasameheki kwa kweli.
 
Rostam Azizi, aliisha iteka nchi yote na aliiweka kwapani. Ndani ya chama alikuwa ni muweka hazina na alikaa sehemu nyeti ambayo kila kiongozi atakaye tawala nchi kwa tiketi ya CCM lazima atakuwa rafiki mkuu wa Rostam.

Kweli kabisa Rostam alikuwa nii mtu hatari sana katika nchi yetu. Kishajua kuwa 2015 kuna hatari Tanzania kuwa na serikali ya mseto au CCM kuanguka madarakani. South Africa wana neno liitwalo "KAULEZA". hivyo huyu jamaa anatengeze life long KAULEZA!
 
WC,unafikiri haya unayoyapendekeza yakifanyika,matatizo haya tunayoyapigia kelele yataondoka?kimsingi nakubaliana na hoja yako ila najaribu kutafakari kwa kina,kwamba leo nchi yetu ikiamua kupunguza ukubwa wa Bunge,Serikali n.k.Je hali tuliyonayo sasa ya umaskini itapungua kwa kiasi gani?
Amini usiamini Dada Regia mapesa haya yanayotafunwa kisiasa yakielekezwa kwenye huduma za jamii na yakasimamiwa vilivyo na BUNGE letu na CAG na taasisi nyingine za udhibiti na usimamizi impact utaiona tu. Ni mengi sana. Wanasiasa wanakula si mchezo. Kusimamia kumekuwa hakupo kabisa. Hili ndilo mama wa matatizo yote NCHI hii.
 
Siku zote wajinga kama mimi ndio huwa tunauliza maswali. Na hakuna ujinga mbaya kama kuuficha ujinga wenyewe. Kama unajua hauna haja ya kuuliza. TD ya leo inasema CCM wao wametumia zaidi ya 3bn! Haulioni hili kama linachangia hali ilivyo katika huduma za jamii kwa nchi yetu? Tusipovisema na kuvikemea vyama hivi tuendako sio kuzuri. Swali nililomuuliza Regia liko palepale.
Hiyo siyo solution.Wewe sasa ni regular card.There aint no wirldness in this.You lost the point.Kwani hizo 3bn wangezipelekea kwenye shughuli za kimaendeleo?Unajuwa zingekuwa wapi hizo pesa kama jimbo lisingekuwa wazi?Sidhani kabisa kama zingekwenda kwenye matumizi ya kuwasaidia wananchi,hiyo siyo culture yenu.Na tatizo haliko hapo.Kama ni matumizi ndo shida,mbona hukumshauri jamaa yako RA azitumie vyema kwa wananchi na wakati inajulikana kajilimbikizia kibao kwa migongo ya masikini?Think think think....Umeshaelezwa nguvu na ushawishi aliokuwa nao,pesa alizokuwa akizimwaga ccm haikuwa ni kwasababu anawapenda wananchi.
Dawa iliyobakini kuyaondoa tu haya matabaka ya mafisadi.Wana roho mbaya sana na wanaonekana hawatakaa wabadilike.Wangetaka wangeshabadilika.Hawatosheki na wana roho mbaya.
 
Kazi za mbunge zimegawanyika katika makundu matatu. Mbunge anawajibika jimboni kwake, bungeni na kwenye chama chake. Bungeni ana wajibu wa kushiriki kwenye debates, kupitisha sheria, n.k. Kwenye chama, anaunga mkono chama chake na kukisaidia katika nyanja mbali mbali kama ku advocate polices zake, msemaji wa chama, nk. Kwenye jimbo lake, mbunge ana jukumu la kushauri jinsi ya kutatua matatizo yanayowakabili wanajimbo hasa yale yanayotakiwa kutatuliwa na serikali, kuwakilisha concerns za wanajimbo bungeni na ku act as a figurehead wa jimbo lake.

Tatizo tulilonalo ni kuwa wabunge wetu wamejikita zaidi kwenye kusaidia vyama vyao kwa njia yoyote ile. Wabunge wengi tuu hawajishughulishi na majadiliano yanayokuwa yanaendelea bungeni. Wengine mpaka wanapigwa picha wakiwa wamelala wakati majadiliano makali yakiendelea. Kubwa zaidi wabunge wengi hawatekelezi majukumu yao kwenye majimbo yao.

Rostam Aziz ni mfano tuu. Sijawahi kumsikia Rostam amesimama bungeni akitetea jambo fulani linalohusu jimbo lake. Wengine walidhani hana haja ya kufanya hivyo kwa vile jimbo lake tayari lina maendeleo ya kutosha. Igunga ni mfano tuu. Kwa wale ambao wamebahatika kutembelea vijijini utalia na roho yako. Hali ni mbaya. Hawa watu wana wawakilishi lakini wanaishi Dar. Wakati Rostam anajiuzuli ilimbidi apande ndege aende Igunga kujiuzulu. Wengine wakijiuzulu watafanya hivyo hivyo.

Lakini the root cause ni sisi wenyewe Watanzania. Politicians use us for their own benefits because we Tanzania don't really bother anymore. Ili mradi tunaenda haja kubwa, that's what matter to us now. Our future generation tumeisahau kabisa. And we will be punished for this. Asha Dii alianzisha thread moja muhimu sana juu ya trend ya African Politics (https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...-politics-historia-itajirudia-tanzania-5.html) ambapo nilisema: We create problems, which in turn we use them to buy votes from voters. Whether wangeshinda Chadema, CUF au walivyoshinda CCM, by 2015 hali mbaya ya maendeleo jimbo la Igunga itaendelea kuwa vile vile. Trust me on this.

Our political game is based on manipulating the poor and illiterate. We create opportunities of dependency to the government and this way the poor always put the same leader, leadership style in power. We the people make our leaders whether new or old what they are. Our leaders in a large measure a reflection of the totality of our attitude to everything. Leadership is sustained by fellowship.
 
Wild Card,most of times huwa unabwatuka mkuu.I mean ni kama unaongea kishabiki kufunika funika hoja za maana kwa kutumia upupu.Kwani CCM hawatozi ada za uanachama?Hawapati ruzuku tena kubwa kupindukia?Halafu bado michango ya mafisadi?Halafu bado panga la ufisadi ie EPA?Sasa ruzuku haiwatoshi?Ama michango ya ada za uanachama haiwatoshi?Michango ya wahindi nk je?Mkijiondolea ruzuku hilo gap mtazipa na kitu gani na nchi mmeshauza?Ama ulikuwa ukifikiria nini wakati unabandikia hii kitu?Unafananisha NGOs,makanisa na vyama vya siasa?Serikali iwe kubwa ama ndogo,kama ufisadi ndo sera unadhani kutakuwepo na mabadiliko?Kwani wanaofanya ufisadi ni wengi ihivyo?Unaweza kupunguza ukubwa wa serikali ukabakiza mafisadi wote,whats the point?Ustuchanganye hapa.RA hasameheki kwa kweli.
Umenielewa kweli Mushi? Kwani mimi nimesema CCM iendelee kulipwa RUZUKU? Kwa kweli kama mnataka kuisambaratisha CCM hata leo hii ondoa ruzuku tu. Kwenye sanduku la kura na KATIBA hii mtaweza lakini baadae sana. Mimi sio mwanachama wa chama chochote nchi hii. Kwa nini kodi yangu ipelekwe CCM, CHADEMA au CUF ili wakodi helikopta?
Ninachokisema kingine ni ile hali ya kudhani kuwa mbunge wa nchi hii anaweza kwaletea maendeleo watu wa jimbo lake. Hili sio kweli sana.
 
Umenielewa kweli Mushi? Kwani mimi nimesema CCM iendelee kulipwa RUZUKU? Kwa kweli kama mnataka kuisambaratisha CCM hata leo hii ondoa ruzuku tu. Kwenye sanduku la kura na KATIBA hii mtaweza lakini baadae sana. Mimi sio mwanachama wa chama chochote nchi hii. Kwa nini kodi yangu ipelekwe CCM, CHADEMA au CUF ili wakodi helikopta?
Ninachokisema kingine ni ile hali ya kudhani kuwa mbunge wa nchi hii anaweza kwaletea maendeleo watu wa jimbo lake. Hili sio kweli sana.
Na wewe umenielewa kweli?Kuondoa ruzuku kutausambaratisha upinzani lakini siyo ccm,kwasababu wana mbinu za kuziba gap.Nilikuuliza mtaliziba vipi kwasababu mmeshauza nchi.Nadhani hamtashindwa maana punda bora afe,Igunga ni mfano.Mbona jamaa yako katajirika na huku jimbo umasikini ukizidi?Sasa unasema ni kwasababu hizo pesa alizisave kwenye akaunti yake badala ya kuzipeleka kwenye maendeleo na sasa waambiwe wasizitoe wakati wa kampeni bali waziache kwenye akaunti?Hapo nimekuelewa.
 
Nadhani hajji sahihi Mkuu. Kila mwaka Bunge hupitisha Bajeti ya Wizara mbalimbali kwaajili ya Miradi mbalimbali hapa nchini lakini swali la kujiuliza je miradi hii hukamilika yote?na je fedha zinazotengwa huenda wapi?na je kama tukipunguza ukubwa wa Bunge na Serikali je fedha hizi zitatumika vizuri?accountability ya fedha itabadilika?kupunguza- ukubwa wa Bunge na Serikali ni unafikiri ni suluhisho la awali?tatizo la nchi yetu sio uwajibikaji?

Amini usiamini Dada Regia mapesa haya yanayotafunwa kisiasa yakielekezwa kwenye huduma za jamii na yakasimamiwa vilivyo na BUNGE letu na CAG na taasisi nyingine za udhibiti na usimamizi impact utaiona tu. Ni mengi sana. Wanasiasa wanakula si mchezo. Kusimamia kumekuwa hakupo kabisa. Hili ndilo mama wa matatizo yote NCHI hii.
 
Kwani nani asiyejua kwamba huyu jamaa alikuwa CCM kwa maslahi yake binafsi na si wananchi?

Kwa utajiri alio nao na shughuli zake za biashara, huwezi kupata ht muda wa kupumzika km una manage shughuli zako zote, kwa nini yeye ajifiche nyuma ya kivuli cha chama na ubunge? Wapo matajiri wengi wakubwa km yeye ila hawapo kabisa ktk mambo haya kwani ht muda wa kusimamia biashara zao hawana, e.g. Bakhresa, Manji, Sabodo, Mengi, Mfuruki, etc.

Amemaliza shida zake na hapa anajianaadaa kutokomea!

Ukiona mfanyabiashara mwenye asili ya nani hii (maize) anakimbilia kwenye siasa, ujue biashara zake si halali, anataka kuvaa koti liitwalo 'mheshimiwa' hususan koti la kijani kama alilokavaa 'Rost azam' ili lifiche vitu vyake haramu, simple like that.
 
Hiyo siyo solution.Wewe sasa ni regular card.There aint no wirldness in this.You lost the point.Kwani hizo 3bn wangezipelekea kwenye shughuli za kimaendeleo?Unajuwa zingekuwa wapi hizo pesa kama jimbo lisingekuwa wazi?Sidhani kabisa kama zingekwenda kwenye matumizi ya kuwasaidia wananchi,hiyo siyo culture yenu.Na tatizo haliko hapo.Kama ni matumizi ndo shida,mbona hukumshauri jamaa yako RA azitumie vyema kwa wananchi na wakati inajulikana kajilimbikizia kibao kwa migongo ya masikini?Think think think....Umeshaelezwa nguvu na ushawishi aliokuwa nao,pesa alizokuwa akizimwaga ccm haikuwa ni kwasababu anawapenda wananchi.
Dawa iliyobakini kuyaondoa tu haya matabaka ya mafisadi.Wana roho mbaya sana na wanaonekana hawatakaa wabadilike.Wangetaka wangeshabadilika.Hawatosheki na wana roho mbaya.
Ninachosema ni kwa nini CCM na vyama vingine wapewe kodi zetu kama ruzuku huku wananchi wetu wakiendelea kutaabika namna hii? Ruzuku hii haiwezi kununua madawati? Haya Rostam hayupo. Tusubiri miujiza ya Kafumu kwa wanaIgunga?
 
Ninachosema ni kwa nini CCM na vyama vingine wapewe kodi zetu kama ruzuku huku wananchi wetu wakiendelea kutaabika namna hii? Ruzuku hii haiwezi kununua madawati? Haya Rostam hayupo. Tusubiri miujiza ya Kafumu kwa wanaIgunga?
Bana eeh,tunajuwa wabunge wanavyofanya kazi bana.Huo umasikini wa Igunga unaonyesha wazi kabisa kuwa haungetatuliwa na haya unayosema ya ruzuku.Hapa tatizo la msingi siyo hilo.Umeelewa mkuu?Kuna wabunge ambao hawakupata utajiri kama yeye na wamesaidia majimbo yao.Ni mapenzi ya mtu kwa taifa na wananchi na si eti mambo ya kuwanyima upinzani na ccm ruzuku.Kwanza nimeshakwambia kuwa ccm hawataathirika.Usizungushe mkuu,mbona husomi posti vyema?Hilo la kutokupewa ruzuku ni debatable lakini halina nafasi kwenye issue hii.Trust me,nionyeshe kivipi lingemsaidia RA kuwaletea maendeleo masikini wa Igunga aliotumia migongo yao na bado kuwaacha masikini wa kutupwa!Bila hata yale mahitaji muhimu ya kibinadamu?Aargh!
 
Ninachosema ni kwa nini CCM na vyama vingine wapewe kodi zetu kama ruzuku huku wananchi wetu wakiendelea kutaabika namna hii? Ruzuku hii haiwezi kununua madawati? Haya Rostam hayupo. Tusubiri miujiza ya Kafumu kwa wanaIgunga?

WC unafikiri fedha hizi zikiachwa kupelekwa kwenye vyama vya siasa ndio Maendeleo yatapatikana?hivi unadhani mtu aliyekuwa nakunywa pombe zamani then akaacha basi baada ya kuacha fedha zile alizokuwa ananunulia pombe zitaleta mabadiliko nyumbani kwake?
 
Back
Top Bottom