Kwenu wanaJF.
Je ni sawa kuwepo kwa mdahalo kati ya CCM na vyama vingine vya upinzani???
Nimependa niweke mada hii kwa mambo mawili.. matatu yafuatayo:
- Kwanza:
Kuweka mdahalo kati ya chama tawala CCM kilichotawala kwa zaidi ya miaka 40 na vyama vya upinzani (Chadema, CUF, UDP, NCCR-Mageuzi,... nk) ambavyo havijawahi kutawala kabisa si sawa. Kuweka mdahalo huu ni sawa na kumpima mtoto aliyesoma darasa la kwanza na mwingine ambaye hakusoma kabisa kisha ukawapa mtihani mmoja, ni wazi kwamba yule ambaye hakusoma kabisa atakuwa na la kujitetea.
Hapa ni rahisi kuikosoa CCM kwa kuwa tayari imeshakaa madarakani na kutoukosoa upinzani ambao haujawahi kuongoza nchi.
Pili:
Kuweza kufikia maendeleo makubwa kama ilivyo kwa nchi za Ulaya na Marekani inahitaji muda wa kutosha ikichukuliwa kwamba jamii yetu (Tanzania) bado haijaelimika vya kutosha hivyo kuwezesha nchi kuwa na maendeleo hayo.
Lakini tujiulize ni mambo mangapi ambayo Serikali chini ya CCM imeyafanya na kuendelea kuyafanya ilihali watu wakiendelea kufaidika nayo??
Kwa upinzani/Chadema kuweza kujibu maswali yote katika mdahalo ni rahisi sana kwa kuwa wakati wote watajibu wataweza na wakati huohuo huwezi kuwasahihisha ama kuwakosoa kwa kuwa hawakuwahi kuongoza nchi, ambapo tungeweza kupima na kujua ni lipi walilitekeleza na lipi hawakulitekeleza.
Hivyo sioni tatizo kwa Makamba kuwataka wagombea wa CCM kutoshiriki midahalo.
Kupima ubora wa pande mbili ni lazima pande zote ziwe zimeshiriki katika jambo tena kwa muda ulio sawa.
Je ni sawa kuwepo kwa mdahalo kati ya CCM na vyama vingine vya upinzani???
Nimependa niweke mada hii kwa mambo mawili.. matatu yafuatayo:
- Kwanza:
Kuweka mdahalo kati ya chama tawala CCM kilichotawala kwa zaidi ya miaka 40 na vyama vya upinzani (Chadema, CUF, UDP, NCCR-Mageuzi,... nk) ambavyo havijawahi kutawala kabisa si sawa. Kuweka mdahalo huu ni sawa na kumpima mtoto aliyesoma darasa la kwanza na mwingine ambaye hakusoma kabisa kisha ukawapa mtihani mmoja, ni wazi kwamba yule ambaye hakusoma kabisa atakuwa na la kujitetea.
Hapa ni rahisi kuikosoa CCM kwa kuwa tayari imeshakaa madarakani na kutoukosoa upinzani ambao haujawahi kuongoza nchi.
Pili:
Kuweza kufikia maendeleo makubwa kama ilivyo kwa nchi za Ulaya na Marekani inahitaji muda wa kutosha ikichukuliwa kwamba jamii yetu (Tanzania) bado haijaelimika vya kutosha hivyo kuwezesha nchi kuwa na maendeleo hayo.
Lakini tujiulize ni mambo mangapi ambayo Serikali chini ya CCM imeyafanya na kuendelea kuyafanya ilihali watu wakiendelea kufaidika nayo??
Kwa upinzani/Chadema kuweza kujibu maswali yote katika mdahalo ni rahisi sana kwa kuwa wakati wote watajibu wataweza na wakati huohuo huwezi kuwasahihisha ama kuwakosoa kwa kuwa hawakuwahi kuongoza nchi, ambapo tungeweza kupima na kujua ni lipi walilitekeleza na lipi hawakulitekeleza.
Hivyo sioni tatizo kwa Makamba kuwataka wagombea wa CCM kutoshiriki midahalo.
Kupima ubora wa pande mbili ni lazima pande zote ziwe zimeshiriki katika jambo tena kwa muda ulio sawa.