Mikael Aweda
JF-Expert Member
- Dec 17, 2010
- 2,973
- 3,901
Wakuu,
Jumatatu niliweka uzi hapa kuhusu nini hasa kinachoweza kuwa nyuma ya pazia la vifo vyenye utata ktk mikutano ya Chadema. Mtumishi wa idara muhimu ya serikali alniambia kuwa kuna mkakati wa kujaribu kudhoofisha chama chenu serikalini.
Kwamba mkakati wa serikali ni kutunga sheria ya kuthibiti vyama vya upinzani hususani Chadema mbele ya safari.
Kwamba hofu yao ni kama sheria hiyo itakukubalika kwa wananchi na wahisani. Na kwamba kuna maofisa wanaodhani kuwa sheria hiyo italeta vurugu.
Na hoja yake ni kwamba inawezekana vifo hivyo vimepangwa ili kuwalainisha wahisani, na kuwaandaa wananchi kuikubali sheria husika pamoja na kuwapa hoja wakubwa serikalini wanaoipigia chapuo sheria hiyo. Pili, sheria ikikwama basi mbinu za kuwachafua zinaweza kutumika. Utunzi wa sheria hii ulishadokezwa hadharani Bungeni na Mwanasheria mkuu.
Leo naomba nitoe hoja 2 zinazoonesha kwamba mtonyaji wangu kutoka serikalini alikuwa mkweli na yuko sahihi.
Mosi, kuvuja kwa siri ya Askari kutolewa nje ya Mkoa wa Iringa kinyemela kama lilivyonukuliwa na gazeti la mwananchi hapa chini
Chanzo hicho kilisema kwamba awali, hawakuwa wakifahamu kama baadhi ya wenzao walichukuliwa na kupelekwa Iringa. "Tulikuja kuona kwenye gazeti picha na tulipofuatilia tukaelezwa kuwa ni kweli Dodoma ilitoa askari kwenda Iringa."
Askari mwingine aliyekuwa katika operesheni hiyo ambaye jina lake tunalihifadhi kwa sababu za kitaaluma, alikiri kuwa hadi jana baadhi yao walikuwa bado wako Iringa na kwamba walikwenda kwa agizo la wakubwa wake wa kazi.
"Sisi ni Watanzania, lakini tumelazimika kuyafanya hayo kwa sababu ya mkate (malipo). Kwa kweli haikuwa haki, kuwatoa askari na silaha kutoka mikoa mitatu kana kwamba wanakwenda kupigana vita!"
Alidokeza kwamba, askari wote waliotoka Dodoma walikuwa njiani kurudi mkoani humo, jana lakini gari la maji ya kuwasha liliendelea kubaki huko Iringa likiwa na dereva wake na askari mmoja mwenye cheo cha inspekta. Askari huyo alisema kwamba gari hilo lililazimika kubaki kutokana na hitilafu.
"Wengine wamerudi lakini, kuna wengine wenye gari la kuwasha bado walikuwa Iringa, gari lao limepata hitilafu kidogo," kilisema chanzo hicho kutoka mjini Dodoma.
Mmoja wa askari hao alidaiwa kwamba hiyo inaweza kuwa moja ya sababu ya askari hao kumshambulia marehemu Mwangosi wakati mwenzao anayemfahamu akijaribu kuwazuia. "Hii inaonyesha kuwa askari hao waliompiga walikuwa hawamjui na huyu aliyekuwa akiwazuia, alimjua."
Alipoulizwa kuhusu taarifa hizo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Zelothe Stephen hakukubali wala kukanusha na badala yake alisema: "Mambo yote hayo yanatakiwa kujibiwa na Kamanda wa Iringa."
Aidha, alisema sakata la kifo cha mwandishi huyo kwa sasa liko katika vyombo vya uchunguzi hivyo asingekuwa tayari kulizungumzia.
"Siwezi kusema kama askari wangu walikwenda huko au hawakwenda, isipokuwa ninachoweza kusema ni kwamba suala hilo lipo katika vyombo husika hivyo waachiwe wao au Kamanda wa Iringa ndiye mwenye majibu."
Alipotajiwa jina la mmoja wa askari aliyeonekana katika picha za video na magazeti za tukio hilo kwamba anatokea katika moja ya vituo vyake, kamanda huyo alisema: "Mimi yakitokea Dodoma nitazungumza wala siyo mtu mwingine kwa hiyo, mambo ya Iringa siwezi kuyazungumza na kama tutaanza kila Kamanda kuzungumza jambo hilo hamuoni kuwa itakuwa ni kama vurugu?"
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Athuman Diwani alikanusha pia kuwapeleka askari wake Iringa akisema: "Hizo taarifa siyo za kweli. Hakuna askari yeyote aliyekwenda Iringa wakati wa vurugu zile."
Maswali ya kujiuliza
Kwa nini askari waliochukuliwa kwa siri hata bila wenzao kujua?
Kwanini makamanda wa mikoa walipoulizwa na mwananchi kuhusu sakata hili wamekuwa waoga kusema ndio au hapana kama ni utaratibu wa kawaida kupeleka askari wa ziada Iringa. Na je, mbona haikutangazwa? Kwani siri? Kwa nini Kamanda wa Mkoa wa Mbeya alidanganya kwa kusema hapana wakati jibu ni kweli askari wake walienda Iringa? Je, askari kutoka Mbeya walitoroka? Nini malengo yao.
Sasa mimi nikihitimisha kwamba askari hawa walikuwa na lengo maalum, ninakosea?
NB; Ifahamike kuwa askari hao wanaletwa Iringa wakati Chadema walishakubali kuendelea na mikutano ya ndani kupisha sensa badala hadhara na hakukuwa na mvutano mkubwa baina yao uliohitaji nguvu kubwa kiasi hicho.
Hoja ya pili ni kauli za viongozi hasa J. Tendwa na Waziri Nchimbi.
Msajili wa vyama John Tendwa na Waziri Nchimbi kwa nyakati tofauti wanatoa hoja za kuilaumu zaidi Chadema, huku Tendwa akitishia kufuta Chadema. Wote hawa, wanajua kwamba ktk vifo vyote hivyo, hakuna kosa la dhahiri lililofanywa na viongozi au wanachama wa kawaida. Badala yake wao wamekuja kudhihirisha kile ambacho mtonyaji wangu aliniambia kuwa lengo ni kupunguza nguvu ya Chadema kwa kuitungia sheria mbovu, kuichafua, kuwatisha wananchi ili wasusie chama hicho na ikiwezekana waifute, japo ktk kuifuta hawakoserious.
NB;Wakati huo huo, usisahau kwamba mrithi wa Shehe Yahaya Nape Nnauye alitabiri kifo cha Ali Zona pale alipowatahadharisha wananchi wa Morogoro redioni siku mmoja kabla kuwa wasiende ktk mikutano ya Chadema Morogoro kwa sababu vurugu zitatokea. Mtabiri Nnauye alipatia na mtu akafa. Je, yeye ni mtabiri mzuri au alijua kitakachokea? alijuaje?
Mwisho ni je, jitihada zao zimefika mwisho? Muda utatuambia. tafakari.
Jumatatu niliweka uzi hapa kuhusu nini hasa kinachoweza kuwa nyuma ya pazia la vifo vyenye utata ktk mikutano ya Chadema. Mtumishi wa idara muhimu ya serikali alniambia kuwa kuna mkakati wa kujaribu kudhoofisha chama chenu serikalini.
Kwamba mkakati wa serikali ni kutunga sheria ya kuthibiti vyama vya upinzani hususani Chadema mbele ya safari.
Kwamba hofu yao ni kama sheria hiyo itakukubalika kwa wananchi na wahisani. Na kwamba kuna maofisa wanaodhani kuwa sheria hiyo italeta vurugu.
Na hoja yake ni kwamba inawezekana vifo hivyo vimepangwa ili kuwalainisha wahisani, na kuwaandaa wananchi kuikubali sheria husika pamoja na kuwapa hoja wakubwa serikalini wanaoipigia chapuo sheria hiyo. Pili, sheria ikikwama basi mbinu za kuwachafua zinaweza kutumika. Utunzi wa sheria hii ulishadokezwa hadharani Bungeni na Mwanasheria mkuu.
Leo naomba nitoe hoja 2 zinazoonesha kwamba mtonyaji wangu kutoka serikalini alikuwa mkweli na yuko sahihi.
Mosi, kuvuja kwa siri ya Askari kutolewa nje ya Mkoa wa Iringa kinyemela kama lilivyonukuliwa na gazeti la mwananchi hapa chini
Chanzo hicho kilisema kwamba awali, hawakuwa wakifahamu kama baadhi ya wenzao walichukuliwa na kupelekwa Iringa. "Tulikuja kuona kwenye gazeti picha na tulipofuatilia tukaelezwa kuwa ni kweli Dodoma ilitoa askari kwenda Iringa."
Askari mwingine aliyekuwa katika operesheni hiyo ambaye jina lake tunalihifadhi kwa sababu za kitaaluma, alikiri kuwa hadi jana baadhi yao walikuwa bado wako Iringa na kwamba walikwenda kwa agizo la wakubwa wake wa kazi.
"Sisi ni Watanzania, lakini tumelazimika kuyafanya hayo kwa sababu ya mkate (malipo). Kwa kweli haikuwa haki, kuwatoa askari na silaha kutoka mikoa mitatu kana kwamba wanakwenda kupigana vita!"
Alidokeza kwamba, askari wote waliotoka Dodoma walikuwa njiani kurudi mkoani humo, jana lakini gari la maji ya kuwasha liliendelea kubaki huko Iringa likiwa na dereva wake na askari mmoja mwenye cheo cha inspekta. Askari huyo alisema kwamba gari hilo lililazimika kubaki kutokana na hitilafu.
"Wengine wamerudi lakini, kuna wengine wenye gari la kuwasha bado walikuwa Iringa, gari lao limepata hitilafu kidogo," kilisema chanzo hicho kutoka mjini Dodoma.
Mmoja wa askari hao alidaiwa kwamba hiyo inaweza kuwa moja ya sababu ya askari hao kumshambulia marehemu Mwangosi wakati mwenzao anayemfahamu akijaribu kuwazuia. "Hii inaonyesha kuwa askari hao waliompiga walikuwa hawamjui na huyu aliyekuwa akiwazuia, alimjua."
Alipoulizwa kuhusu taarifa hizo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Zelothe Stephen hakukubali wala kukanusha na badala yake alisema: "Mambo yote hayo yanatakiwa kujibiwa na Kamanda wa Iringa."
Aidha, alisema sakata la kifo cha mwandishi huyo kwa sasa liko katika vyombo vya uchunguzi hivyo asingekuwa tayari kulizungumzia.
"Siwezi kusema kama askari wangu walikwenda huko au hawakwenda, isipokuwa ninachoweza kusema ni kwamba suala hilo lipo katika vyombo husika hivyo waachiwe wao au Kamanda wa Iringa ndiye mwenye majibu."
Alipotajiwa jina la mmoja wa askari aliyeonekana katika picha za video na magazeti za tukio hilo kwamba anatokea katika moja ya vituo vyake, kamanda huyo alisema: "Mimi yakitokea Dodoma nitazungumza wala siyo mtu mwingine kwa hiyo, mambo ya Iringa siwezi kuyazungumza na kama tutaanza kila Kamanda kuzungumza jambo hilo hamuoni kuwa itakuwa ni kama vurugu?"
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Athuman Diwani alikanusha pia kuwapeleka askari wake Iringa akisema: "Hizo taarifa siyo za kweli. Hakuna askari yeyote aliyekwenda Iringa wakati wa vurugu zile."
Maswali ya kujiuliza
Kwa nini askari waliochukuliwa kwa siri hata bila wenzao kujua?
Kwanini makamanda wa mikoa walipoulizwa na mwananchi kuhusu sakata hili wamekuwa waoga kusema ndio au hapana kama ni utaratibu wa kawaida kupeleka askari wa ziada Iringa. Na je, mbona haikutangazwa? Kwani siri? Kwa nini Kamanda wa Mkoa wa Mbeya alidanganya kwa kusema hapana wakati jibu ni kweli askari wake walienda Iringa? Je, askari kutoka Mbeya walitoroka? Nini malengo yao.
Sasa mimi nikihitimisha kwamba askari hawa walikuwa na lengo maalum, ninakosea?
NB; Ifahamike kuwa askari hao wanaletwa Iringa wakati Chadema walishakubali kuendelea na mikutano ya ndani kupisha sensa badala hadhara na hakukuwa na mvutano mkubwa baina yao uliohitaji nguvu kubwa kiasi hicho.
Hoja ya pili ni kauli za viongozi hasa J. Tendwa na Waziri Nchimbi.
Msajili wa vyama John Tendwa na Waziri Nchimbi kwa nyakati tofauti wanatoa hoja za kuilaumu zaidi Chadema, huku Tendwa akitishia kufuta Chadema. Wote hawa, wanajua kwamba ktk vifo vyote hivyo, hakuna kosa la dhahiri lililofanywa na viongozi au wanachama wa kawaida. Badala yake wao wamekuja kudhihirisha kile ambacho mtonyaji wangu aliniambia kuwa lengo ni kupunguza nguvu ya Chadema kwa kuitungia sheria mbovu, kuichafua, kuwatisha wananchi ili wasusie chama hicho na ikiwezekana waifute, japo ktk kuifuta hawakoserious.
Hii taarifa ya Molemo nayo inatisha.Mungu amewaumbua.Kilichoikoa CDM ni zile picha zilizopigwa na waandishi kuonyesha yule polisi katili alivyofumua utumbo wa mwandishi yule masikini.Kwani siku ile tayari Chagonja alishasema CDM ndiyo walirusha kitu kizito kumuua yule mwandishi,kumbe walishajipanga kupiga propaganda na tayari Tendwa alishaandaliwa kuongea ujinga kama wa leo ili kuhalalisha kufuta CDM.Mungu ni mwema waandishi wamemuumbua Tendwa na wenzie.
NB;Wakati huo huo, usisahau kwamba mrithi wa Shehe Yahaya Nape Nnauye alitabiri kifo cha Ali Zona pale alipowatahadharisha wananchi wa Morogoro redioni siku mmoja kabla kuwa wasiende ktk mikutano ya Chadema Morogoro kwa sababu vurugu zitatokea. Mtabiri Nnauye alipatia na mtu akafa. Je, yeye ni mtabiri mzuri au alijua kitakachokea? alijuaje?
Mwisho ni je, jitihada zao zimefika mwisho? Muda utatuambia. tafakari.