GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,656
- 109,056
Mganga mmoja maarufu anayetokea Mkoa mmoja wa Kanda ya Ziwa ( jina lake linahifadhiwa ) ameibuka na kusema kuwa hakuna Kismati / Bahati ambayo Mwanaume anaweza kuipata kama angalau akijiwekea utaratibu wa kila wiki angalau Kuvaa Chupi / Nguo ya ndani ya Mpenzi wake na kwenda nayo katika Shughuli zake.
Mganga huyo alienda mbele zaidi na kusema kwamba amekuwa akiwapa mbinu hii Wanaume wengi na imeweza sana kuwasaidia huku wengi wakimshukuru kwa kusema kuwa hapo nyuma maisha yao yalikuwa ni magumu ila mara baada ya kuanza utaratibu wa angalau Kuvaa Chupi za Wapenzi wao maisha yamebadilika kwani kuna vismati / bahati fulani sasa zinawapata.
Ni imani yangu kubwa sana kwamba baada ya kuwaleteeni hii taarifa sasa wale wenzangu na Mimi tunaobeti Ligi Kuu ya Uingereza, tunaofanya Kazi katika Machimbo ya Migodi, tunaofanya Biashara mbalimbali, wenye wadaiwa wetu Sugu na wale wengine wote wenye mahitaji mbalimbali ya Kimaisha kuanzia sasa mtajitahidi angalau hata ndani ya siku tatu za wiki mtakuwa mnavaa Chupi / Nguo za ndani za Wapenzi wenu na kuchanja nazo mbuga katika mihangaiko yenu.
Siku zote Mjumbe hauwawi na Shikamoo Mganga!
Nawasilisha.
Mganga huyo alienda mbele zaidi na kusema kwamba amekuwa akiwapa mbinu hii Wanaume wengi na imeweza sana kuwasaidia huku wengi wakimshukuru kwa kusema kuwa hapo nyuma maisha yao yalikuwa ni magumu ila mara baada ya kuanza utaratibu wa angalau Kuvaa Chupi za Wapenzi wao maisha yamebadilika kwani kuna vismati / bahati fulani sasa zinawapata.
Ni imani yangu kubwa sana kwamba baada ya kuwaleteeni hii taarifa sasa wale wenzangu na Mimi tunaobeti Ligi Kuu ya Uingereza, tunaofanya Kazi katika Machimbo ya Migodi, tunaofanya Biashara mbalimbali, wenye wadaiwa wetu Sugu na wale wengine wote wenye mahitaji mbalimbali ya Kimaisha kuanzia sasa mtajitahidi angalau hata ndani ya siku tatu za wiki mtakuwa mnavaa Chupi / Nguo za ndani za Wapenzi wenu na kuchanja nazo mbuga katika mihangaiko yenu.
Siku zote Mjumbe hauwawi na Shikamoo Mganga!
Nawasilisha.