Kutoka Ukumbi wa Chuo Kikuu Huria Musoma: Prof. Muhongo atangaza nia ya Kugombea Urais

Asante Mungu wengi wameanza kuona. Huitaji kwenda shule au kuwa Malaika kuona how potential Prof. Muhongo is. Huitaji kujifunza vitu vingi saaana ili ujue Tanzania kama nchi tumekuwa tukikosa nini kwa mda wote huu baada ya kumsikiliza Prof Muhongo.
Nilimpigia simu mwenzangu mmoja baada ya kuangalia utangazaji nia wake nikamwambia naomba umuangalie prof .
kusema kweli ni kama Mungu ametushushia hii zawadi na kutuambia tuone tulikuwa tumekosa nini kwa miaka yote na sasa ndo ameamua kutupa.
Nazidi kuomba tena watu watu wa television na redio mrudie tena kuonyesha hii event ya prof Muhongo akitangaza nia. Naomba tena hata mnao andaa iyo midahalo please fanyeni juu chini kwenyew hii midahalo prof Muhongo awepo ili watanzania waweze kuiona hii hazina na fanyeni juu chini iyo midahalo ionyeshwe na television nyingi sana hapa nchini na irushwe na redio nyingi sana ili watanzania wapate kuiona hii hazina.
Mungu ambariki na kumlinda prof Muhongo.

Nilisema, Nasema Na Namalizia Sasa Kusema Tena NIKISISITIZA Kuwa Our Next President Is Going To Be Professor Sospeter Muhongo.
 
Kwa hiyo nani kakuambia tunahitaji cv, ndefu tunahitaji utendaji na sio cv na vyeti, wenye vyeti na cv wako wengi, hatutaki watu wanaojisifu tz ilipofika inahitaji rais anaefanana na dictator awakimbize watanzania tufike kwenye malengo, sio kujisifu umesoma ges, yeye anaona ges tu, kuna kilimo, viwanda hambavyo havipo, tusubiri watangaza nia wote na waupinzani ndo tutajua rais ni nani bhana...
 
Video nzima ya 060615 MARUDIO YA HOTUBA YA PROF. SOSPETER MUHONGO ALIYOITOWA MUSOMA WAKATI AKITANGAZA NIA - URAIS
mqdefault.jpg


Source: Gonga link hii: Channel ten
: https://www.youtube.com/watch?v=PMjRV4E0SAg
 
June 5, 2015

Mambo Muhimu Ya Kuzingatia Unapokwenda Kutoa Hotuba

Ndugu zangu,
Mada kuhusu sanaa ya kuzungumza mbele ya hadhara imevuta wengi. Bila shaka, sababu kuu ni ukweli, wengi tunapata tabu sana kila tunapotakiwa kuongea hadharani.


Kwa vile hata waliozaliwa na vipaji vya kuongea hadharani na kuvuta watu wanahitaji kujifunza zaidi, basi, hata asiye na kipaji, anaweza kujifunza na akawa mzungumzaji mzuri mwenye kuvutia hadhira yake.


Leo nitazungumzia kile kilicho muhimu kabisa kwa mtu anayehutubia. Kinaitwa ' actio' kwa Kigiriki.Actio inahusu zaidi kinachoonekana kwa nje na hadhira ama wasikilizaji pale mzungumzaji anapokuwa akihutubia. Ni ile misogeo au mitikisiko mbalimbali ya mzungumzaji kimwili ikiwa ni pamoja na sauti na hata mawasiliano ya mboni za macho ya mzungumzaji na wasikilizaji wake.

Muhimu sana unavyozungumza. Jinsi unavyoitumia sauti yako vile unavyohama kutoka hali tofauti za sauti. Unavyobadilisha ukubwa ama ujazo wa sauti yako. Na ni kwa namna gani, wakati mwingine, kulingana na neno au sentesi unayotaka kuisema unavyobadilisha sauti yako. Mfano mzuri hapa ni Julius Nyerere, aliweza kucheza vizuri na sauti katika hali zote; " .. Ni watu wa ovyo ovyo tu...!" Hapo aliweza kuibana sauti ikasikika kwa namna ya kuvutia kuweka msisitizo wa anachotaka kusema.(P.T)


Ufundi Ni Upi Kwenye Kuhutubia?


Ili uweze kutoa hotuba ya nguvu ikaweza hata kuwaacha watu wasitamani umalize na kuondoka ni sharti mzungumzaji uwe na uwezo wa kumiliki vitu vitatu;
1. Mimic - inahusu taswira. Hapa ni jinsi unavyocheza na mdomo, macho, na hata kope za macho.
2. Prosodi- Ni neno la Kigiriki hili, ina maana ya namna unavyotumia sauti na hata unapoweka vituo kwenye hotuba.
3. Gestik- Hapa inahusu unavyotumia viungo vya mwili wako ukiwa jukwaani.Tujikite kwenye Mimic.Eneo hili ni muhimu sana maana ndipo hupelekea wasikilizaji ama wamuamini mzungumzaji au wasimwamini. Kama kinachoonekana kwenye mdomo na macho yako hakifanani na unachosema, kuna wataoguna mioyoni, kuwa unawadanganya. Ndipo hapa tena, Julius Nyerere alipata kusema; :" Mgombea akisema anakemea rushwa, basi, tukimuangalia usoni tuseme , naam, huyu kweli anakemea rushwa!"Mzungumzaji unaweza ukakochiwa namna ya kuwasiliana kwa mimic. Na tabasamu la kweli huonekana kwa wasikilizaji. Hutokea mzungumzaji akatabasamu lakini macho yamenuna. Hilo ni tabasamu la uongo. Tabasamu la kweli huonekana machoni. Hapa tena Julius Nyerere ni mfano wa wazungumzaji walioweza kuonyesha tabasamu na macho yakatabasamu pia. Tabasamu ni muhimu sana kwenye hotuba. Ni kama kiungo kwenye chakula. Tabasamu huashiria mzungumzaji ni mtu rafiki, anasogelekeka kwa mazungumzo. Mzungumzaji katika hili tafuta yale ambayo unajua hata wewe ukiyasema hadharani yatakufurahisha. Utatabasamu tu kiuasilia...
Source: Mambo Muhimu Ya Kuzingatia Unapokwenda Kutoa Hotuba..
Kwa mwenye kutaka ushauri wa bure wasiliana nami;
0754 678 252Maggid.Dar es Salaam.

Naona kwa watia nia ya Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzana kupitia CCM Prof. Sospeter Muhongo amepata alama za juu , je wana-JamiiForums
 
Mhn watu bwana we Muhongooo ,Lowasa n.k mmejiuzuru kwa mbnde (muhongo) miaka 9 takrban hujanithbtishia ubora wako na iko hv ata uwe mwema kama waliokuzunguka wahun na we utakuwa muhun tu. Mm nakumbuka Kikwete alivyoingia madarakan na spd na uhakika mwsho wa sku ndo tumeshuhudia serkal ya ajabu kabsa kupata kutokea dunian yan baraza la mawazr likikarbia/likibadlishwa mara mbl. Na zikivuma sifa za uchum kupanda tu kherkhal watu njaa kali (Muhongo apo ulkuwa wap?!). Na hakuna kaul mbiu iliyokuwa kali kama ya kpnd cha huyu Jamaa Kikwete ile ya 'HALI MPYA NGUVU MPYA NA KASI MPYA'. Enhe lakn sasa tuje nn klchofuata baada ya apo sasa . Kikwete aliingia saf lakn akakuta kuna uozo tisha ndan akawa mpole kla ktu mpoooole msndanganye nyie wakina Muhongo wahongo tu ka' majina yenu.
 
Kwa hiyo nani kakuambia tunahitaji cv, ndefu tunahitaji utendaji na sio cv na vyeti, wenye vyeti na cv wako wengi, hatutaki watu wanaojisifu tz ilipofika inahitaji rais anaefanana na dictator awakimbize watanzania tufike kwenye malengo, sio kujisifu umesoma ges, yeye anaona ges tu, kuna kilimo, viwanda hambavyo havipo, tusubiri watangaza nia wote na waupinzani ndo tutajua rais ni nani bhana...

Hivi mtu akitaja CV yake anajisifu?
 
Professor na Mwalimu wangu Muhongo.

Asalaam..

Mara upatapo barua hii sisi ni wazima hofu na mashaka ni kwako Wewe uliye Mbali na upeo wa macho yetu. Sisi Sote tunakusalimu na kukutakia Afya njema Kwenye masuala yanayoendelea huko mijini.

Dhumuni la barua hii kwanza ni salaam, pili kukupa mrejesho wa upepo wa kisiasa ulivyo huku bara, watu wamebadillika, hawaangalii UKAWA wala CCM, watu wanaangalia Mtu. Uchaguzi wa mwaka huu ni Taifa kwanza CHAMA Baadae, watu huku wanaangalia rekodi Za uchapakazi. Wanasema rekodi Za Kazi waliZo nazo Lowassa Na Slaa zinatisha. Hawa jamaa wanasifika Kwa Kazi sio MCHEZO .

Professor wangu, masihi Yesu kipindi flan watu walimuuliza Kwa habari ya kuwatambua waongofu miongoni mwa raia wa DUNIA. Basi masihi Yule akawaambia hamtaweza kuwatambua Kwa maneno matam, hotuba nzurinzuri, sura zao wala tembea Yao, Bali mtawatambua Kwa matunda Yao.

Kwa hiyo rekodi ya kazi alizofanya Mtu Kwa jamii ni Za Muhimu sana. Hiki hasa ndicho kinacho wafanya mamilioni ya Watanzania kuwahitaji watu hawa.

Mwisho professor wangu, tungependa kuziona KaZi zako. GST imefanya tafiti Za madini Kwa ufadhili wa Fedha Za nje. Na Baada ya tafiti watu Hawa wamezitumia tafiti hizo kufahamu rasilimali Za Nchi yetu. Tukisema utafiti Wenu umesababisha nchi yetu kuuzika nje tumekosea.!

Madigrii yako yote ya uprofessor umeshindwa HATA kutengeneza kinu kimoja tu Cha kuosha dhahabu au Shaba. Umeshindwa kuthaminisha madini yetu Kwenye soko la nje. Umeshindwa kuwawezesha wajasiriamali wa Madini wa ndani Na kuwatengenezea wigo mpana nje ya Nchi. Embu jiulize zaidi ya kula hela Za wafadhili Kwenye tafiti Ni kitu gani Elimu yako imefanya Kwa wananchi ?

Kazi Za Mtu .. KaZi Za Mtu professor..
 
Kunawatu akili zao wamezivalia kwenye soksi huyu mleta mada ni miongoni mwao.
 
Prof Muhongo ndy raisi mwenye kuteletea mafanikio siyo matumaini.Dhana ya matumaini ipo kwa wa Tanzania wanaokaribia kufa.
 
Hivi chama cha mapinduzi mwaka 1975 kilikuwepo? huu ni usanii wa hali ya juu. Kadi ina muhuri wa chama cha mapinduzi wakati chama chenyewe hakikuwepo.
 
TUJIKUMBUSHE ILIANZIA WAPI SAFARI YA PROF. S. MUHONGO KUTIA NIA URAIS KWA TIKETI YA CCM

APRIL 7, 2015

Prof. Muhongo: Nitazungumzia urais muda ukifika

Wakati makundi mbalimbali yakipigana vikumbo kumshawishi aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo agombee urais, mwenyewe amesema muda bado, ukifika atasema. Baadhi ya makundi yaliyojitokeza na kumtaka agombee ni Chama cha Watu wenye ulemavu mkoani Mwanza na wanafunzi wa vyuo vikuu vya Jomo Kenyatta, IAA, Semmco na Makumira.

Akiwa bungeni mjini Dodoma, Profesa Muhongo amekuwa akitajwa mara kwa mara na wabunge wenzake kama rais mtarajiwa na yeye amekuwa akifurahia kuitwa hivyo. Lakini alipoulizwa na gazeti hili kuhusu suala hilo, alijibu "Ya kwangu nitayasema muda ukifika."

Alisema kama kuna watu wanamuunga mkono hawezi kuwazuia, ila wasiandamane kumfuata kwa nia ya kumshawishi kwani kufanya hivyo ni kinyume na taratibu.

Machi 22 mwaka huu, kupitia mwenyekiti wao, Charles Ngereza wanafunzi hao waliwaambia waandishi wa habari jijini Arusha kuwa watazunguka kwenye vyuo na taasisi zote za elimu ya juu nchini kuwashawishi wenzao kuungana nao.

"Sababu kuu ya kumuunga mkono ni rekodi ya utendaji wake. Kwa kipindi kifupi alichoongoza Wizara ya Nishati na Madini amefanya mapinduzi makubwa yaliyowashinda watangulizi wake ikiwamo kushusha bei ya kuunganisha umeme kufikia kati ya Sh27,000 hadi Sh177,000 vijijini," alisema Ngereza.

Alisema kasi ya utekelezaji wa mradi wa umeme vijijini, licha ya kuwapatia wananchi huduma ya nishati, pia imechangamsha uchumi kwa kuongeza shughuli za uzalishaji zinazotegemea nishati ya umeme.

Muhongo: Ni mapema mno

Profesa Muhongo alisema kuwa ni mapema sana kuzungumza kama atawania urais au la.

"Hawajaja (wanafunzi) kuniona kama wanataka (kunishawishi) waendelee huko huko si kuja kwangu," alisema.

Aliongeza, "Taratibu zimewekwa mbona mnakuwa na wasiwasi, ya kwangu nataka nikiyaongea muda uwe umefika."

Katika hoja zao wanafunzi hao, walisema hatua ya Profesa Muhongo kujiuzulu ilitokana na uwajibikaji kutokana na dhamana aliyokuwa nayo.


Walisema hiyo ni moja ya sifa za uongozi na kumtaja Rais mstaafu wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi aliyejiuzulu uwaziri wakati wa uongozi wa Mwalimu Julius Nyerere na baadaye kuukwaa urais.


Wanafunzi waliohudhuria mkutano huo na vyuo vyao kwenye mabano ni Rahma Sengela (Jomo Kenyatta), Daudi Shayo (IAA), Sarah Aminarabi (Arusha), Nelson Machumu (Semmco) na Hobeshi Juvenary kutoka Makumira.

Source: Prof. Muhongo: Nitazungumzia urais - Kitaifa
 
Hakujiuzulu ila alipigwa chini ushahidi wa kimazingira ulionyesha hivyo. Haiwezekani ndani ya lisaa moj kama sio mawili kabla Rais hajataja baraza lake la mawaziri yeye ajiuzulu wakati aligoma Mwanzo na ndani ya muda huo Rais awe amempata mtu wa kumweka kwenye wizara nyeti na ngumu kama hiyo wenye akili tunajua alipigwa chini uwaziri kama Milioni kumi kwa mboga
 
Muhongo anaongoza kwa kua na uhakika na mambo yanayotekelezeka huyu jamaa ndio atatuvusha hawa wengine chai tu
Kamanda safi safi kwa hii hoja yako,wengine badala ya kufanya utafiti wanafitinishwa na TV na Magazeti kuwa jamaa hafai,Jamaa anajiamini,anaongea kile kinachowezekana,na anaona mbele,kuna watu wamezoea kudandia na ushabiki,hawawezi kueleza ubaya wa huyu jamaa zaidi ya kusikia kwenye magazeti na TV.
BIG UP PROF MUHONGO...BILA KUPEPESA MACHO
 
nimetafakari kwa kina, nimemfanyia tathmini iliyotukuka na kumlinganisha na watangaza nia wenzake wote 22 mpaka leo ukiachia mbali wale wa kesho sasa ni rasmi na nasadiki kusema kuwa iwe isiwe kwa mujibu wa mathematician gentamycine 100% rais mpya ajaye wa tanzania ni profesa sospeter muhongo.

sifa zake ni nyingi na zilizotukuka na sijaona anayefanana nae kiakili na kimaono kati ya wote waliokwisha na watakaomalizia kutangaza nia. profesa muhongo ndiyo jibu la watanzania na nina imani na wana ccm wote kuwa mtampitisha huyu genius wa kitanzania ili atutawale.

profesa muhongo popote ulipo tafadhali hebu tutafutane ili niweze kukupa mikakati mingine ya kuelekea ikulu mwezi october 2015 na sasa natangaza rasmi kukuunga mkono wewe na nipo tayari kukupigia chapuo kokote kule nchini tanzania ili uweze kuwa rais wetu na nina imani kabisa kuwa utapita.

Ninachokuomba tu ni kwamba ukishafanikiwa kuwa rais usisahau kuwapa vyeo watu hawa ili kudhoofisha makundi yao. Kwa mfano ningependekeza ukiwa rais wetu wizara ya mambo ya nchi za nje au ubalozi wa tanzania nchini ujerumani mpe mzee lowassa ili imrahisishie kwenda ulaya au kupata tiba kama pakiwa na hilo hitaji lakini wizara ya afrika mashariki mteue mzee benard membe au kama vipi utampa ubalozi wa tanzania nchini libya au burundi lakini nakuomba makamu wako wa rais ( running mate ) awe jaji augustino ramadhan na iwe isiwe nakuomba waziri mkuu wako mpe mzee john pombe magufuli na hao wagombea wengine waliotangaza nia utaamua tu kuwatupa huku na kule ili wasinyong'onyee na kukuletea jicho la husuda.

Namalizia tena kwa kusema tena nikiwa na uhakika wa maono yangu yaliyotukuka kwamba ewe mheshimiwa profesa sospeter muhongo ndiyo utakuwa rais wetu na zingatia hayo yote niliyokuelekeza hapo juu na kwa mengi zaidi wewe mwenyewe au kupitia kamati yako hakikisha au hakikisheni mnanitafuta ili niwape strategies zingine zilizotukuka pamoja na mambo ya kiitifaki ambayo siwezi kuyaanika yote hapa ila ukini pm mwenyewe nitawasiliana na wewe tuweze kukutana na kufanya kazi ila ikulu kaa ukijua kuwa ni yako.

Najua wengine mtanuna na mtanuna sana na mno mwaka huu ila profesa muhongo ndiyo next prezidaa wetu na tambueni mathematician gentamycine akipenda kitu basi hata mwenyezi mungu na malaika wake wamekikubali na wamekithibitisha.

Nawatakieni maandalizi mema watanzania wenzangu wote ya kumpokea rais mpya na ajaye tanzania mheshimiwa profesa sospeter muhongo na maneno yangu haya ya leo nayasadiki kwenu.

Akhsanteni.
chukua tena "like" mkuu umemaliza kila kitu,huyu ni mzee wa facts bila kupepesa macho..
 
Back
Top Bottom