Kuteuwa Wakurugenzi nje ya Utumishi wa Umma hakupaswi kufumbiwa Macho

Kuna kitu hukijui au unakisahau.
Siyo kila kiongozi wa CCM hajapitia utumishi wa umma kabla ya kupewa uongozi CCM.
Sasa siku akirudishwa serikalini huwezi kusema hana uzoefu kwenye utumishi wa umma.
Mfano kuna katibu wa CCM mkoa fulani wa kaskazini alikuwa mwalimu serikalini kwa miaka mingi.
Mtoa hoja amesema sifa ya mkurugenzi anatakiwa atoke kwenye manegarial position yaani awe aliwahi kuwa mkuu wa idara fulani, kama ni elimu basi awe amekuwa mkuu wa moja ya idara za elimu na sifa nyingine hatakiwi kuwa mwanachama wa chama cha siasa. Rejea wakurugenzi walioteuliwa kipindi cha utawala wa rais Kikwete uliona mkurugenzi mwana ccm? Magufuli alikuwa anakiuka sheria na taratibu za utumishi wa umma na Samia naye anaendeleza yale yale, matokeo yake ukurugenzi wa halmashauri, wilaya na mikoa wamekuwa wakiteuliwa kwa misingi ya uchama na sio kama taratibu za utumishi wa umma zinavyotaka. Mtu anayeshabikia ccm na uongozi wake na hana akili timamu.
 
Mtoa hoja amesema sifa ya mkurugenzi anatakiwa atoke kwenye manegarial position yaani awe aliwahi kuwa mkuu wa idara fulani, kama ni elimu basi awe amekuwa mkuu wa moja ya idara za elimu na sifa nyingine hatakiwi kuwa mwanachama wa chama cha siasa. Rejea wakurugenzi walioteuliwa kipindi cha utawala wa rais Kikwete uliona mkurugenzi mwana ccm? Magufuli alikuwa anakiuka sheria na taratibu za utumishi wa umma na Samia naye anaendeleza yale yale, matokeo yake ukurugenzi wa halmashauri, wilaya na mikoa wamekuwa wakiteuliwa kwa misingi ya uchama na sio kama taratibu za utumishi wa umma zinavyotaka. Mtu anayeshabikia ccm na uongozi wake na hana akili timamu.
Sikatai kwamba kuna walio teliuwa ambao hawakufikia vigezo alivyo sema lakini tusijumuishe kila mteuliwa aliyetokea CCM hana hizo sifa.
Kwa mfano huwezi kuniambia mwalimu wa amejiendeleza kielimu na yupo kazini miaka kadhaa atashindwa hiyo kazi.
Huwezi kuniambia mtu msomi yupo CCM lakini amewahi kuajiriwa na kushika uongozi kwenye taasisi binafsi zenye operation nyingi na department nyingi, mbunifu, mchapa kazi, muadilifu na mwenye busara atashindwa kuwa mkurugenzi mzuri. Sababu pia kuna idara zenye viongozi chini yake ambao ndiyo wasaidizi na watekelezaji wa kazi za kila siku.

Hakuna maajabu kwenye hiyo nafasi sema hapa ni wivu na kuona wanapewa outsiders ulaji,
The keyword here is SELFISHNESS.
Pia watu wako conservative sana wanaogopa mabadiliko ya kuachana na ukiritimba, ubadhirifu na rushwa.

Magufuli alikuwa anataka kuleta watu wapya ambao hawajakuzwa kikazi serikalini katika mazingira niliyo kutajia hapo juu. Lengo kubadili mazoea ya tabia mbaya.
 
Sikatai kwamba kuna walio teliuwa ambao hawakufikia vigezo alivyo sema lakini tusijumuishe kila mteuliwa aliyetokea CCM hana hizo sifa.
Kwa mfano huwezi kuniambia mwalimu wa amejiendeleza kielimu na yupo kazini miaka kadhaa atashindwa hiyo kazi.
Huwezi kuniambia mtu msomi yupo CCM lakini amewahi kuajiriwa na kushika uongozi kwenye taasisi binafsi zenye operation nyingi na department nyingi, mbunifu, mchapa kazi, muadilifu na mwenye busara atashindwa kuwa mkurugenzi mzuri. Sababu pia kuna idara zenye viongozi chini yake ambao ndiyo wasaidizi na watekelezaji wa kazi za kila siku.

Hakuna maajabu kwenye hiyo nafasi sema hapa ni wivu na kuona wanapewa outsiders ulaji,
The keyword here is SELFISHNESS.
Pia watu wako conservative sana wanaogopa madiliko ya kuachana na ukiritimba, ubadhirifu na rushwa.

Magufuli alikuwa anataka kuleta watu wapya ambao hawajakuzwa kikazi serikalini katika mazingira niliyo kutajia hapo juu. Lengo kubadili mazoea ya tabia mbaya.
Kwa ufupi nafasi za ukurugenzi ni kwa waajiriwa walioko serikali na wenye sifa zinazokidhi vigezo vya utumishi wa umma. Ukurugenzi ni kama nafasi ya kupanda daraja sio ajira mpya na ndio maana muundo wa utumishi ukaweka masharti ya mtu kuwa mkurugenzi lakini ccm wamedharau taratibu za kiutumishi wameamua kugeuza vyeo vya ukurugenzi kuwa ajira za machawa wao ambao si waajiriwa wa serikalini.
 
Kimsingi, hakuna teuzi yeyote anayofanya Rais isiyokuwa na masharti. Wakurugenzi ni watumishi wa umma ambao ni permanent and pensionable. Wanatambulika kwenye muundo wa utumishi wa umma. Na sifa za kuwa mkurugenzi ni kuwa angalau umetumikia managerial position ya ukuu wa Idara kwa miaka mitano.

Makosa ya kuteua watendaji nje ya utumishi wa umma alianza nayo Magufuli, naona mama nae anaendeleza. Hii ni dhambi, inapaswa tuikemee kama ambavyo tulikemea DPW.

Mkurugenzi wa Tanesco alitoka nje ya utumishi wa umma. Tanesco imemshinda. Sasa wanamhamishia TTCL, si kwa sababu anaweza, bali hamna pa kumpeleka kwa sababu tayari kawa mtumishi wa umma wa ajira ya kudumu. Na mshahara wake hautashuka hata kama watampa kazi ya kufagia ofisi.

Huko halmashauri ni yale yale. Rais anateua mwenyekiti wa CCM kuwa mkurugenzi wa halmashauri. Kweli? Anajuwa kazi? Ana vigezo kwa mujibu wa utumishi wa umma na scheme of service? Kwa kawaida mkurugenzi anapaswa kuwa kawahi kuwa mkuu wa idara kwenye local government au hata kwenye madhirika ya umma. Sasa unaleta mtu kutoka nje. Inamaanisha watu waliopo ndani ya utumishi wa umma hawafai? Hii ni kuwadharau seniors walioko kwenye utumishi wa umma. Na kumbuka kwenye utumishi wa umma kuna succession plan. Mkurugenzi lazima aandae mtu ambae anaweza kushika nafasi yake kwa kuwa anamkaimisha na. Ndivyo utumishi wa umma unafanya kazi.
Sasa huyu wa kufundishwa kazi anawezaje andaa viongozi wengine? Remember, namna utumishi wa umma unafanya kazi ni tofauti kabisa na uongozi ktk siasa ama private sector.

Fikiria akaja Rais mwingine na akaona mkurugenzi huyu hafai, anamtengua. Atafanya kazi gani? Magufuli alikuwa anawatengua, anakaa kimya. Wanakaa kula mshahara bila kazi. Wakienda kuomba msamaha anawapa kazi nyingine kama ukatibu tawala. Ndo maana wage bill ilikuwa kubwa sana.

Jambo jingine, Mkurugenzi kupewa jukumu la kusimamia uchaguzi ni kwa sababu kikatiba mkurugenzi hapaswi kuwa kada wa chama chochote cha siasa. Sasa unamuweka kada, anawezaje kutenda haki?

Tukemee kwa nguvu zetu zote
Huu ujinga aliuanzisha marehemu.umeleta hasara kubwa mnooooo.
Pitia report ya CAG,utafahamu hasara hizo.
 
Back
Top Bottom