Kushtakiwa kwa waziri mkuu Pinda mahakamani, ushauri wangu kwa LHRC na TLS

Mikael Aweda

JF-Expert Member
Dec 17, 2010
2,973
3,901
Nakubaliana na waziri mkuu Pinda kwamba nchi hii lazima iongozwe kwa sheria,kinyume chake kama sheria haifuatwi hasa na viongozi wenye dhamana kunaweza kukatokea machafuko makubwa. kwa hiyo, napendekeza tuangalie mazingira yaliyo sababisha waziri mkuu afikie hapo ndipo tuamue kumshtaki au tumsamehe. Hebu tuangalie mifano michache ambayo inawezekana ndo imemkera sana waziri mkuu mpaka akatoa kauli hiyo tata;

1)Serikali imeshasema na sote tunakubali kuwa madawa ya kulevya ni mabaya sana kwa vijana wetu. Madawa haya yanaua vijana wetu na kufifisha nguvu kazi ya Taifa letu. Lakini wapo watz tena wengine viongozi wakiwepo wabunge na mawaziri wanaohusika na biashara hiyo. Kama Pinda anataka wauza madawa ya kulevya wapigwe na polisi suing mkono hoja ya kushtakiwa nashauri tumsamehe, kwa awamu hii tu.



2)Wako watanzania wengi sana waliopoteza maisha yao ktk mikutano ya hadhara ya vyama ktk mazingira ya kutatanisha inayowahusisha vyombo vya dola yakiwepo mabomu ya Arusha. Kwa mujibu wa katiba, na katiba iko wazi, kukitokea kifo cho chote chenye utata Rais ataunda tume kimahamaka ya majaji kuchunguza tukio hilo. Na viko vyama vilivyoomba Tume ya kimahakama ya majaji iundwe kwa mujibu wa katiba. Bahati mbaya SANA Rais amekataa kuunda Tume hiyo na vifo hivyo viko vingi sana. Sasa, kama Pinda ana uchungu na vifo hivyo, na ameshindwa kumwambia bosi wake moja kwa moja, badala yake anataka polisi indo wampige bosi wake ili aunde tume husika ya kuchunguza vifo hivyo tata, nashauri tumsamehe Pinda.

3)Wako watu waliomteka Kibanda, wako waliomwua Mwangosi, na wapo waliomteka Dr Ulimboka akiwepo Ramadhani Ighondu, na wapo waliomwagia Kubenea na Mzee Tegambwage tindikali. Sasa haya mambo yamemkera sana Pinda, amesarika sana na ameghaflika. Inawezekana kabisa Pinda anataka Ramadhan Ighohundu na wengine waliohusika na mateso, utekaji wa namna hiyo wapigwe na polisi. Kama huu ndo mtazamo wa Pinda naomba tumsamehe.


4)Wiki hii kuna mabinti wawili wa secondary walivamiwa na kubakwa na watu wasiofahamika ktk ‘gheto' au chumba chao. Mmojawapo alishindwa kustahimili akajiua. Jambo hili limesababishwa na viongozi waliofisadi pesa zetu za kujenga mabweni mpaka watoto wote wa sekodnary nchi nzima wanapata madhila makubwa sana ukiwepo ubakaji. Kama Pinda anataka viongozi waliosababisha kutokuwepo kwa mabweni wakiwepo mawaziri wahusika na huyo mbakaji wa watoto wapigwe na polisi, naomba tumsamehe Pinda, walau mara moja tu.

5)Wako wanaotuhumiwa kuua tembo na kuiba nyara za serikali. Mbaya zaidi ripoti za serikali inasema tembo wetu wataisha ndani ya miaka 7 ijayo kama ujangili hautathibitiwa. Kati yao yupo katibu mkuu wa ccm Abdulrahamani Kinana. Sasa kama Polisi aliwalenga majangili hao akiwepo kinana tutafakari upya kabla hatujamshtaki.


6)Wiki hii mimi na baadhi ya madiwani kutoka Mbulu na Babati tunafuatilia sakata la Watz zaidi ya 90 kutoka Manyara na Arusha wengi wao wairaqw na Wamasai waliohamia Tanga na Morogoro ambao wamefukuzwa na viongozi wa serikali kama wezi. Mbaya zaidi mtu amekaa hapo zaidi ya miaka 10, anapewa masaa 24 yeye na watoto walioko shule na mifugo waondoke ktk muda huo. Wengi wakashindwa kufanya hivyo, wakaswekwa ndani. Sasa Pinda akiagiza viongozi wa namna hiyo wapigwe na Polisi napendekeza tumsamehe.


7)Wanafuzni wetu wa kidato cha nne wamefelishwa sana kwa maelfu,- sijasema wamefeli, mpaka kidato cha sita na vyuo kuna hatari ya kukosa wanafunzi mbeleni. Hii ina maana kwamba mabilioni ya fedha za kuwasomesha watoto waliofeli yamepotea kutokana na uzembe wa viongozi wakiwepo mawaziri wa Elimu Mulugo na Kawambwa. Kwa maoni yangu, kama Pinda aliwalenga viongozi wote na mawaziri hao tusimshtaki kwanza kwa sababu anawalilia wanafunzi waliojiua baada ya kufeli na ana uchungu na wazazi waliopoteza fedha zao kulipia ada na gharama nyingine. Kwa hiyo, kama Pinda anataka Kawambwa na Mulugo wapigwe, tusimshtaki kwanza, Tumsamehe.

8)Wiki iliyopita gazeti la Jamhuri liliibika na ufisadi wa Mabilioni ya shilingi yaliyoibwa na viongozi wa serikali wakati wa mkutano wa smart partnership uliofanyika mwezi uliopita jijini Dsm. Katibu mkuu Kiongozi aling'aka akakwama. Polisi badala ya kuwahoji mafisadi wakawahoji Deo Balile na Jacktona Manyerere. Sasa kama Pinda anataka viongozi walioiba fedha zetu wapigwe, nashauri tukae naye kwanza tujadiliane naye ili tumwelewe.

9)Wako Viongozi waliopanga kuwadhuru Viongozi wa Chadema na wapo waliotumia mitambo maalum kuingilia mawasiliano yao ili kuwabambikiza kesi, wako waliomwekea mmojawapo kifaa cha kunasa mawasiliano yake Dodoma. Wako waliotaka kuwaua baadhi ya viongozi wa chama hicho. Wapo wahuni waliowapiga wabunge wetu 2 kule mwanza na kuwaumiza sana. Kama Pinda analenga hawa wavunja amani ya nchi yetu, kwa kweli hatumtendei haki Pinda tukimshtaki bila kumsikiliza.

10)Wako watz magezezani waliobambikiwa kesi za uwongo na Polisi. Waziri Nchimbi amekri hivyo na Mbunge Lema alikutana nao huko gerezani akaleta na mifano hai ya hizo kesi na ushahidi wa ubambikaji wa kesi hizo. Hii ina maana kwamba kuna wajane na wagane mitaani kwa sababu wenzao wanatumiki vifungo feki. Watoto wao wamegeuka watoto wa mitaani. Sasa, kwa kweli kama Pinda anataka polisi wawapige hao watu na hasa polisi wanaobambika kesi wapigwe na polisi wenzao , basi tumfikirie kwanza Pinada kabla ya kumshtaki.


11) Wako mafisadi ambao Pinda alishasema hawashitakiki mahakamani kwa kuwa ukiwashtaki nchi itatikisika. Wako mafisadi wa EPA, Buzwagi, Richmond nk. Sasa kama Pinda ameona kuwa kwa kuwa hatuwezi kuwashtaki tuwaruhusu Polisi wawapige, napendekeza kabisa tumsamehe Pinda kwa sababu madhara ya matrilioni yaliyoibwa na hao watu ni makubwa sana kuliko kichapo watakachopewa na Polisi.



Hata hivyo, kwa kuwa Pinda ndo aliyeagiza wasiotii sheria wachapwe itakuwaje kama yeye mwenyewe akivunja sheria naye achapwe. Maana yeye pia aliwahi kudanganya Bunge kuhusu sakata mauaji ya Arusha la January 5, 2011 na amegoma kujizulu. Lema alipeleka ushahidi wa jinsi Pinda alivyolidanganya Bunge LAKINI Spika ameamua kumpotezea Lema. Au tuseme kwa kuwa yeye ndo aliyeagiza wavunja sheria wachapwe yeye asichapwe na polisi kwa kulidanganya Bunge?

Hata hivyo, kama Pinda anataka watazania wanaolalamikia na kuandamana kwa sababu nilizotaja hapo juu ndo wapigwe na Polisi naomba niwapongeze LHRC NA TLS kwa kazi nzuri ya kumfungulia kesi na Jumapili nitawaombea kwa Mungu wasitolewe Meno na kucha Bila ganzi ili Mungu awalinde.


Ni mawazo yangu tu, maana naipenda nchi yangu Tanzania, sina nyingine
 
Nilishaona kwenye luninga nchi nyingi raia wake wakidundwa virungu na vyombo vya usalama hususani polisi. Hata kule democrasia inakohubiriwa kama vile Uingereza, Ufaransa, Ujeremani na hata Marekani. Ukweli ni kwamba binadamu ni kiumbe hatari sana. Kuna msemo wa kwamba ukicheka na nyani utavuna mabua. Sote tunaelewa jinsi wananchi walivyosababisha madhara makubwa ya mali hata uhai wa wengine. mifano iko mingi tu hata ikitajwa haitaisha. Kule Meru Mbunge moja mstaafu alivamiwa shamba lake na nyumba na magari kuteketezwa. Huko Mtwara mbunge mwingine juzi juzi amechomewa nyumba, gari na trakta na kundi la wananchi. Maumivu waliyo nayo hao waliofanyiwa hayo ni makubwa kupita kiasi. Jiulize mwenyewe ingekuwa yalikutokea wewe ungejisikiaje? Mimi nadhani virungu na vipigo ni njia pekee ya kuleta nidhamu kwa wale ambao ni wakorofi. Nakubaliana kabisa kwamba si haki vitumike vinginevyo kwa lengo tu la polisi kuonyesha ubabe na kufanya hivyo ni dhambi hata kwa Mungu. Ndio maana najiuliza itakuaje sasa kwa sisi wazazi ambao tunasema RUKSA walimu kuchapa wanafunzi kwa kiwango fulani ili kuwashikisha nidhamu? Je LHRC itatufikisha mahakamani vilevile? Au pengine itawafikisha waziri wa elimu na mkurugenzi wa elimu?
 
Nilishaona kwenye luninga nchi nyingi raia wake wakidundwa virungu na vyombo vya usalama hususani polisi. Hata kule democrasia inakohubiriwa kama vile Uingereza, Ufaransa, Ujeremani na hata Marekani. Ukweli ni kwamba binadamu ni kiumbe hatari sana. Kuna msemo wa kwamba ukicheka na nyani utavuna mabua. Sote tunaelewa jinsi wananchi walivyosababisha madhara makubwa ya mali hata uhai wa wengine. mifano iko mingi tu hata ikitajwa haitaisha. Kule Meru Mbunge moja mstaafu alivamiwa shamba lake na nyumba na magari kuteketezwa. Huko Mtwara mbunge mwingine juzi juzi amechomewa nyumba, gari na trakta na kundi la wananchi. Maumivu waliyo nayo hao waliofanyiwa hayo ni makubwa kupita kiasi. Jiulize mwenyewe ingekuwa yalikutokea wewe ungejisikiaje? Mimi nadhani virungu na vipigo ni njia pekee ya kuleta nidhamu kwa wale ambao ni wakorofi. Nakubaliana kabisa kwamba si haki vitumike vinginevyo kwa lengo tu la polisi kuonyesha ubabe na kufanya hivyo ni dhambi hata kwa Mungu. Ndio maana najiuliza itakuaje sasa kwa sisi wazazi ambao tunasema RUKSA walimu kuchapa wanafunzi kwa kiwango fulani ili kuwashikisha nidhamu? Je LHRC itatufikisha mahakamani vilevile? Au pengine itawafikisha waziri wa elimu na mkurugenzi wa elimu?

Waweza thibitisha askari wa kwenye Nchi za kidemkrasia wakiwapiga raia virungu? hili la PINDA kwenda KORTINI limewashtua watawala, maana siku za hivi karibuni mahakama imekataa kuwa shuka la kulalia la watawala, chochote chaweza kutokea ndio maana mnahangaika sana, lazima sheria za Nchi zifatwe, sio pinda wala wewe mwenye mamlaka ya kupiga wenzie.
 
Kule China watu walichapwa viboko ndio maana wakaendelea.

Sisi huku kwetu mentality tofauti tusijifananishe na Europe sisi ni kama wachina tu lazima tupelekane kwa mijeledi kwanza halafu mbele tutakaa sawa.
 
Mkuu M.P.Aweda;
Nadhani mahakamani ndiko mahala pazuri pakuanzia mjadala unaoupendekeza maana Pinda atatupa majibu ya nini alikuwa anamaanisha .Usisahau kuwa kuna maneno mengine zaidi ''Tumechoka''
 
Kule China watu
walichapwa viboko ndio maana wakaendelea.

Sisi huku kwetu mentality tofauti tusijifananishe na Europe sisi ni kama
wachina tu lazima tupelekane kwa mijeledi kwanza halafu mbele tutakaa
sawa.

mkuu, kuna watu wanadhani kuwa kutoadhibu watu wakaidi ndo demokrasia ya kweli. sijui kama wanakumbuka lile tukio la polisi afrika ya kusini kufyatulia risasi wafanyakazi wa mgodi wa marikana ambapo watu zaidi ya 40 walikufa. raia anapokiuka sheria na akakaidi amri ya polisi kinachoendelea ni adhabu. ingawa polisi wetu wanafanya kazi kwa weledi mkubwa, naona kuna watu wanataka kulazimisha polisi wafanye kazi yao ya haki. watu kama akina aweda ambao kila kukicha wanawaza kuanzisha maandamano, wanaona kuwa tamko la pinda ni kikwazo cha uovu wao
 
[FONT=lucida
console]Mkuu M.P.Aweda;
Nadhani mahakamani ndiko mahala pazuri pakuanzia mjadala unaoupendekeza
maana Pinda atatupa majibu ya nini alikuwa anamaanisha .Usisahau kuwa
kuna maneno mengine zaidi ''Tumechoka''
[/FONT]

serikali ikichoka kuvumilia maandamano yasiyo na kibali kinachofuata ni kipigo. I support Pinda
 
Tabia ya watu kutotii sheria inasababishwa na kuchoshwa na mienendo ya serikali yao katika kuwaletea maendeleo.
Miaka hamsnini ya uhuru tunasherekea tukiwa tunategemea chakula cha msaada,kukosekana kwa madawa hospitalini,Umeme kwa watanzania wasiozidi asilimia kumi,mishahara duni kwa wafanyakazi wa umma,huduma dhaifu kama elimu duni,maji machafu ya kunywa,Kunyimwa uhuru wa habari, kupumbazwa na madawa ya kulevya tuwe mazezeta n.k huku wakishuhudia fursa nyingi zenye neema wakipewa wawekezaji na kundi la watanzania wenye nasaba na wenye mamlaka.
Ukijumlisha na Hatua ya juu ya ukosefu wa staha kwa majeshi yetu kwa raia wasio na hatia na ukandamizaji wa makusudi wa demokrasia kwa kizazi cha sasa ambacho kiko "assetive" unatarajia utazalisha wananchi wenye tabia ya aina gani?
Ni muda mzuri kwa Mh.Pinda kubadili kauli na kuwageuzia kibao wale wanaopelekea Watanzania kuwa katika hali walio nayo sasa.
Kwakuwa amekiri "serikali imechoka" kukabiliana na watu ambao wana nia njema na nchi yao,ni busara wakapisha ambao "hawajachoka" wapate fursa ya kupumzika na kutafakari mazuri waliyoyafanya na mabaya ili wakiwa wamepumzika vya kutosha waje tena ulingoni wajaribu bahati yao.
Nafikiri kwa kauli aliyoitoa anapaswa kufikishwa kwenye sheria ili haki ipate kutendeka iwe mfano kwa watumishi wa umma kutochoka wakiwa kazini,ni bora waombe kupumzika kuliko kuchoka huku ukiendelea kuwepo madarakani.
 
Nilishaona kwenye luninga nchi nyingi raia wake wakidundwa virungu na vyombo vya usalama hususani polisi. It is Reasonable force to control situation Hata kule democrasia inakohubiriwa kama vile Uingereza, Ufaransa, Ujeremani na hata Marekani.Police brutality inalalamikiwa sana na police wanashitakiwa na wengine wanafungwa if quilty. Ukweli ni kwamba binadamu ni kiumbe hatari sana. Kuna msemo wa kwamba ukicheka na nyani utavuna mabua. Mimi nadhani virungu na vipigo ni njia pekee ya kuleta nidhamu kwa wale ambao ni wakorofi? Mwanafunzi chuo kikuu kudai posho yake ni ukorofi? wazee wa east Africa kudai mafao yao ni ukorofi? watoto wa shule za msingi kuzuia magari kushinikiza serikali kuweka matuta au alama za punda milia baada ya wenzao kugongwa ni ukorofi? Madaktari na manesi kuandamana kuomba mazingira mazuri na salama kwa kazi zao ni ukorofi? walimu kuandamana kudai mishahara yao waliyokosa kwa zaidi ya miezi 3 ni ukorofi? Nakubaliana kabisa kwamba si haki vitumike vinginevyo kwa lengo tu la polisi kuonyesha ubabe na kufanya hivyo ni dhambi hata kwa Mungu. Maandamano ni njia muhafaka kwa mujibu wa katiba ya JMT, kudai haki yako kwa njia ya amani ni dhambi? Ndio maana najiuliza itakuaje sasa kwa sisi wazazi ambao tunasema RUKSA walimu kuchapa wanafunzi kwa kiwango fulani ili kuwashikisha nidhamu? to discipline mwanafunzi na kumkomoa mpaka kumjeruhi ni vitu viwili tofauti. Sitegemei kijana wangu kuvunjwa mkono na mwalimu Je LHRC itatufikisha mahakamani vilevile? kama wewe ni mwalimu unazungumza hivi, watoto wetu watafeli kila siku Au pengine itawafikisha waziri wa elimu na mkurugenzi wa elimu?
Naomba ujibu hoja zangu
 
Kule China watu walichapwa viboko ndio maana wakaendelea.

Sisi huku kwetu mentality tofauti tusijifananishe na Europe sisi ni kama wachina tu lazima tupelekane kwa mijeledi kwanza halafu mbele tutakaa sawa.

Ungemuelewa mleta mada husingeandika haya kama unataka tufanane na china leo hii Kinana angekuwa kanyongwa,yule mmiliki na wote waliosababisha kusambaza dawa feki za ARV wangekuwa wamenyongwa,Idd Azan hasingekuwa nje angekuwa ndani akisubiri uchunguzi pia kama tungekuwa kama china tusingekuwa kituo cha upokeaji na usambazaji wa madawa ya kulevya.
 
Sipati picha sasa Kaka Petero kavuliwa miwani eti analambishwa bakora!! alivyokuwa na machozi ya karibu mmmhh
Sheria msumeno ati
 
Ki ukweli wananchi wakiachiwa wafanye watakalo sidhani hata huu muda wa kuleta uzi himu na kujadili utakuwepo lazima tukubali ukweli kwamba inapotokea ujeuri uonevu kutoheshimiana bila sababu ni lazima panishment iwepo ni kama ndani ya familia baba ukajidai kila kitu mwacheni tu kesho utakuta nyumba imekuwa danguro wavuta bangi wa unga wauza miili yao wapo hapo
 
JK atakuwa rais wa kwanza kushitakiwa kwa kutumia madaraka yake vibaya.
 
Kwake yeye wahalifu ni CDM. Waziri mkuu wa kwanza nyambaf = stupid Tanzania. Proved by the court of law Dodoma.
 
Back
Top Bottom