Kura ya Maoni: Muundo upi wa Muungano unafaa?

Muundo upi wa Muungano unafaa?

  • Serikali 1

    Votes: 81 23.3%
  • Serikali 2

    Votes: 22 6.3%
  • Serikali 3

    Votes: 241 69.5%
  • Sijui

    Votes: 3 0.9%

  • Total voters
    347
  • Poll closed .
mkuu wa nchi kashatusua kwa waliofuatilia hotuba yake Bungeni wataelewa tu...
Hii nchi amani tu ndo inatulinda kwakweli vinginevyo ni balaaaaa ni kwereeeeeeee arifuuuuuu
 
Serikali tatu. Hii ndio itatoa haki kwa kila upande. Ona wazanzibar watajiamulia na Watanganyika watajiamulia mambo yao. Kuna upendeleo kwa wazanzibar kwa kuwabeba mgongoni kama vile watoto kwa gharama za watanganyika tumechoka.
 
Mwanzon nilikuwa nashabikia serikali 3, bila kujua kiundan ila JK kanifungua kwa nini tunataka serikali 2.
 
Serikali 3 naamini ni bora kuliko option nyingine. Wakubwa wajaribu kupotosha historia na kutaka tuamini kwamba Tanganyika haipo, haikupata kuwepo na haitakuwepo. Wakati huohuo wanakubali kuwa Zanzibar ni nchi, huu Muungano umetokana na nini? Ni muungano wa Tanzania Bara na Zanzibar? Kuweni wa kweli. Hofu ya kuvunjika muungano eti kwa sababu ya serikali tatu ni dangaya toto wanatetea maslahi yao. Kwani Zanzibar hawawezi kuuvunja kwa kuwa wao ni nchi na wana katiba yao inayowalinda. Au tutatumia mabavu kuwabana?
 
Pamoja na uwingi wa mataifa yanayoiunda USA hatujawahi kusikia migogoro kama tiliyo nayo sisi, hii ni kwa sababu walifikiria kuungana na kweli kwa nia moja yenye mawazo yakinifu wakaungana na kufanya dola moja lenye kiongozi mmoja. Sasa sisi naona tunaigiza kuungana, mara serikali tatu mara 2 sijui huu unakuwa ni muungano wa namna gani. Kama tumeamua kuungana basi tumaanishe na kama suala hili linatushinda basi lisisumbue akili kwa sababu litaendelea kutufanya kuwa wafikiriaji wadogo kudhani muungano ni serikali 3 toka lini muungano wa vitu viwili ukapelekea vitu vitatu....????? Huu ni upuuzi.
 
Warioba kachemka sana yaani angekuja na hoja ya serikali moja kweli tungejuwa amebaini matatizo, kutuletea serikali 3 huku akijua 2 zilikuwa na changamoto kibao huko ni kutaka kutuvuruga na kutugawa hakika.
 
Baada ya mipasho ya Mwenyekiti wa Chama( CCM) dhidi ya Rasimu ya Tume ya Katiba katika hotuba yake jana kwa Bunge Maalumu la Katiba kinachoweza kuwa imebaki
kuwa Plan B kwa wana- CCM na Mwenyekiti wao ni kutumia Karata ya Maridhiano ili kufikia maamuzi yaliyowashinda Miaka Nenda Rudi ya kufikia Malengo ya Waasisi wa JMT ya kuwa na Nchi Moja na Serikali Moja.

Je hoja hii itafanikiwa kwa mbinu zifuatazo?

Maridhiano katika ya ; CCM VS UKAWA au Zanzibar vs Tanganyika.

Yetu macho na masikio.

Wajumbe wa Bunge Maalumu nawaomba sana michezo hii muanze kuzilia mazoezi ilimusije potezana na kushindwa kuliona Goli husika/manuafaa na Mikwamo.
 
Hakuna katiba mpya tena pale. Ninachokiona mimi ni watu wenye nia njema na Tanzania watafunga virago na kuondoka Dodoma.
 
Rasimu ya katiba iliyowasilishwa na jaji warioba inapendekeza muundo wa muungano uwe wa serikali tatu,hivi wananchi waliotoa hayo maoni walikuwa na uelewa kuhusu serikali na muundo unaofaa?nimejaribu kuwauliza baadhi ya wananchi wa kawaida huku vijijini na sehemu kidogo mjini kama wanaelewa nini kuhusu muundo unaopendekezwa,ukweli hawaelewi,hivyo ninachowaza huu muundo ni mapendekezo ya wanasiasa na jina la wananchi linatumika tu kuihalalisha wakati hawaelewi chochote juu ya muundo wa serikali,JK kasema asilimia kubwa ya wananchi waliotoa maoni hawanyazungumzia muundo wa muungano kwa maana hiyo muungano sio kero kwao,ukweli ni kwamba hawajui chochote au wanajua kidogo tu,watazungumziaje jambo wasilolijua?Kuhusu serikali mbili nalo halifahamiki kwa wananchi wengi,pili wakati huu muundo unaanzishwa hakukuwa na elimu yeyote iliyotolewa wala upigaji kura wa muundo unaofaa.Hivyo kuna wananchi wengi jinsi serikali yetu na mahusiano yaliopo kati ya zenj na bara.Hivyo basi,ili muungano uwe valid kwa maana ya maoni ya wananchi,uandaliwe mchakato wa kura ya maoni kuhusu muungano unaofaa,elimu ya kina itolewe kuhusu miundi yote miwili,then kura zipigwe kumaliza utata,hali ilivyo kwa sasa,wanasiasa ndo wanapitisha agenda zao kwa jina la wananchi.
 
Hakuna katiba mpya tena pale. Ninachokiona mimi ni watu wenye nia njema na Tanzania watafunga virago na kuondoka Dodoma.

Kufunga virago kwa Wajumbe ndicho JK na Chama chake wanachokitaka na watafurahi kuona hilo linafanikiwa .

Na hii itakuwa dhambi kubwa kwa UKAWA na wengineo wote kwa kula pesa za walipa Kodi na mwisho kususia kazi waliyotumwa.

Nawashauri kusimamia kidete kufufuka kwa Tanganyika kupitia Muundo wa Nchi mbili Serikali Tatu .

Kinyume na hapo kuwe na Muaafaka wa Nchi moja Serikali Moja na Na hili linafaa kuafikiwa na Wajumbe wote kabla ya kuanza Kujadili Rasimu Nzima ,maana kiuhalisia hakuna mantiki ya kujadili Rasimu kama Muundo wa Serikali haufahamiki/unaleta mgogoro.
 
Acha utoto unaposema mipasho unamaanisha nini... utu uzima pia ni kuwa mstaarabu kwa kila neno unalotamka!
 
Historia siku zote ndiyo inayomuhukumu mtu nilimsikiliza rais wakati anatoa hotuba na kutanabaisha kuwa serikali tatu ni gharama kuliko mbili na viongozi waliouasisi muungano waliona mbili ndio suluhu swali linakuja kama kwale serikali mbili ndio suluhisho nini kwa nini matatizo mpaka leo hayajatatuliwa mpaka sasa mwaka wa 50 huu na kadri tunavyokwenda serikali mbili ipo kwenye deni kubwa ambalo halilipiki zaidi ya nchi wahisani kufanya chochote wanachotaka kutokana na deni wanalotudai.
Swali la pili kama kweli sio unafiki kusema tunawaenzi waasisi nakumbuka hotuba moja ya mwalimu julius nyerere aliwahi waasa viongozi na kuwaambia rasilimali tulizokuwa nazo mfano madini na vinginevyo haviozi kwa hiyo viachwe mpaka nchi yetu tanzania itakaposomesha vijana wake na kuwa na wataalamu wa kutosha kuweza kusimamia na kuzitumia rasilimali za nchi ipasavyo je kama kweli hamkimbii kivuli chenu kwa nini katika hili hamkumuenzi mwali mkaanza kujimilikisha rasilimali za nchi kama za kwenu ? Uko wapi uzalendo hapa mnaouzungumzia zaidi ya uhafidhina .
Na ikumbukumbukwe kwamba enzi ya chama kimoja ccm walikuwa hawataki kabisaa kusikia nchi imeingia kwenye mfumo wa vyama vingi mwalimu akaitisha kura ya maoni watu wengi wakakataa vyama vingi wachache wakakubali vyama vingi lakini kutokana na upeo na maarifa aliyokuwa nayo mwl nyerere na kuangalia wakati uliopo akayachukua maoni ya watu wachache na kukubali nchi kuingia katika mfumo wa vyama vingi huyo ndio kiongozi aliyetumia busara hekma na maono kuepusha shari ambayo ingewezatokea mabeleni kutoka na wakati uliopo.
Hoja inakuja kwamba serikali tatu kwa wakati huu tuliopo haiepukiki kama ni gharama hata hii tulionayo sasa kila kichwa cha mtanzania kilicho hai kinadaiwa laki tano anaekataa haya aje na hoja ni kwanini muundo wa serikali mbili bado umeliingiza taifa katika deni kubwa ambalo halilipiki na kama litalipwa mtuambie ni nani atakaezilipa ni heri kuishi na mchawi kuliko kuishi na mnafki .
 
Sidhani kama wataondoka, lakini hata wakiondoka haiwezi kuwa nzuri kwa CCM....

Hawawezi kuandika katiba wao wenyewe, hata kama wangependa kufanya hivyo, nadhani wangependa kufanya hivyo lakini kwa mwamvuli kwamba wengine nao wameshiriki...lakini hawawezi kuwa wajinga kufanya peke yao wazi wazi....

Ndio maana pamoja na wingi wao, mara nyingi wamekuwa wanalazimika kuridhiana na wapinzani katika issues mbali mbali tangu mchakato huu uanze.....

Umoja wa CDM, CUF na NCCR hauwezi kuwa ignored kirahisi.......


Kufunga virago kwa Wajumbe ndicho JK na Chama chake wanachokitaka na watafurahi kuona hilo linafanikiwa .

Na hii itakuwa dhambi kubwa kwa UKAWA na wengineo wote kwa kula pesa za walipa Kodi na mwisho kususia kazi waliyotumwa.

Nawashauri kusimamia kidete kufufuka kwa Tanganyika kupitia Muundo wa Nchi mbili Serikali Tatu .

Kinyume na hapo kuwe na Muaafaka wa Nchi moja Serikali Moja na Na hili linafaa kuafikiwa na Wajumbe wote kabla ya kuanza Kujadili Rasimu Nzima ,maana kiuhalisia hakuna mantiki ya kujadili Rasimu kama Muundo wa Serikali haufahamiki/unaleta mgogoro.
 
Historia siku zote ndiyo inayomuhukumu mtu nilimsikiliza rais wakati anatoa hotuba na kutanabaisha kuwa serikali tatu ni gharama kuliko mbili na viongozi waliouasisi muungano waliona mbili ndio suluhu swali linakuja kama kwale serikali mbili ndio suluhisho nini kwa nini matatizo mpaka leo hayajatatuliwa mpaka sasa mwaka wa 50 huu na kadri tunavyokwenda serikali mbili ipo kwenye deni kubwa ambalo halilipiki zaidi ya nchi wahisani kufanya chochote wanachotaka kutokana na deni wanalotudai.
Swali la pili kama kweli sio unafiki kusema tunawaenzi waasisi nakumbuka hotuba moja ya mwalimu julius nyerere aliwahi waasa viongozi na kuwaambia rasilimali tulizokuwa nazo mfano madini na vinginevyo haviozi kwa hiyo viachwe mpaka nchi yetu tanzania itakaposomesha vijana wake na kuwa na wataalamu wa kutosha kuweza kusimamia na kuzitumia rasilimali za nchi ipasavyo je kama kweli hamkimbii kivuli chenu kwa nini katika hili hamkumuenzi mwali mkaanza kujimilikisha rasilimali za nchi kama za kwenu ? Uko wapi uzalendo hapa mnaouzungumzia zaidi ya uhafidhina .
Na ikumbukumbukwe kwamba enzi ya chama kimoja ccm walikuwa hawataki kabisaa kusikia nchi imeingia kwenye mfumo wa vyama vingi mwalimu akaitisha kura ya maoni watu wengi wakakataa vyama vingi wachache wakakubali vyama vingi lakini kutokana na upeo na maarifa aliyokuwa nayo mwl nyerere na kuangalia wakati uliopo akayachukua maoni ya watu wachache na kukubali nchi kuingia katika mfumo wa vyama vingi huyo ndio kiongozi aliyetumia busara hekma na maono kuepusha shari ambayo ingewezatokea mabeleni kutoka na wakati uliopo.
Hoja inakuja kwamba serikali tatu kwa wakati huu tuliopo haiepukiki kama ni gharama hata hii tulionayo sasa kila kichwa cha mtanzania kilicho hai kinadaiwa laki tano anaekataa haya aje na hoja ni kwanini muundo wa serikali mbili bado umeliingiza taifa katika deni kubwa ambalo halilipiki na kama litalipwa mtuambie ni nani atakaezilipa ni heri kuishi na mchawi kuliko kuishi na mnafki .

Japokuwa namheshimu sana Nyerere na natambua mchango wake kwenye Taifa hili; Yeye ndiye katuachia confusion yote hii.

Mimi nadhani Nyerere pia hakua tayari kuingia vyma vingi bali kwakujua yatakayotokea mbele ya safari alitu pre-empt na kutuanzishia vyama vinavyo fanana na upinzani lakini si vya upinzani in their operation.

Sasa ndiyo tunatafuta vyama vya upinzani kweli na demokrasia ya vyama vingi.

Well angekuwepo angetupa sababu ya kutuingiza kwenye hii confusion pengine nia ilikuwa njema labda alitaka guided demokrasia.....Hii ni labda lakini kwa macho yangu yaliyojaa maruweruwe basi successors wake ama hawakumwelewa na hivyo kawaacha wahawajui vision yake au hawakuwa pamoja naye tangu mwanzo.


Kimoja tu ni kuwa we are in a deep confusion; shukrani kwa incubent president amekuwa accomodative!
 
Back
Top Bottom