OKW BOBAN SUNZU
Platinum Member
- Aug 24, 2011
- 49,301
- 104,171
Baada ya sare ya bao 1-1 dhidi ya Medeama, uongozi wa klabu ya Yanga umeliandikia barua Shirikisho la Soka barani Afrika (CAF) KULALAMIKA uamuzi mbaya ulioonyeshwa na mwamuzi aliyechezesha mchezo wao huo
.
Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano ya Yanga, Rodgers Gumbo alikiri kuandika barua ya MALALAMIKO kwa CAF “Ni kweli tumepeleka barua ya malalamiko kwa CAF kutokana na kuwa na ushahidi wa matukio ambayo ni wazi hatukutendewa haki ambayo ni pamoja na rafu ambayo mchezaji wetu Nickson Kibabage alichezewa na mchezaji wa Medeama ambaye alistahili kuonyeshwa kadi nyekundu lakini refa hakufanya hivyo.
.
“Lakini pia kuna tukio la bao letu halali ambalo Kibabage alifunga lakini refa akalikataa akiwaaminisha watazamaji na wachezaji kuwa waliotea hivyo sio bao sahihi lakini baada ya kulitazama kwenye video tumebaini uonevu; Tumewaandikia ili wajue nini cha kufanya kwa sababu matukio kama yale yananyima timu haki ya kupata ushindi na kuipa nyingine matokeo ambayo haijastahili,” alisema Gumbo
My Take
Utopolo at work
.
Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano ya Yanga, Rodgers Gumbo alikiri kuandika barua ya MALALAMIKO kwa CAF “Ni kweli tumepeleka barua ya malalamiko kwa CAF kutokana na kuwa na ushahidi wa matukio ambayo ni wazi hatukutendewa haki ambayo ni pamoja na rafu ambayo mchezaji wetu Nickson Kibabage alichezewa na mchezaji wa Medeama ambaye alistahili kuonyeshwa kadi nyekundu lakini refa hakufanya hivyo.
.
“Lakini pia kuna tukio la bao letu halali ambalo Kibabage alifunga lakini refa akalikataa akiwaaminisha watazamaji na wachezaji kuwa waliotea hivyo sio bao sahihi lakini baada ya kulitazama kwenye video tumebaini uonevu; Tumewaandikia ili wajue nini cha kufanya kwa sababu matukio kama yale yananyima timu haki ya kupata ushindi na kuipa nyingine matokeo ambayo haijastahili,” alisema Gumbo
My Take
Utopolo at work