Kuna uraibu wa vyakula vya nazi? Chakula cha nazi ni bora sana tofauti na kisicho na nazi?

Si umesema huwezi toka bila Ile feni yako ya kininja, sasa nazi tunaweza nunua ambayo ipo tayar Kwa matumizi usibebe kibao beba feni🤣
Nazi ni lazima niikwangue mwenyewe. Maana ili iwe tamu inabidi wakati wa kukwangua niwe nakata mauno yale ya unyago. Tofauti na hapo haitakuwa tamu kwenye chakula.

Feni sibebi bhana… kwani kwako hamna AC?
 
Wenyeji wa Mikoa ya Bara hatukuwa familiar sana na msosi wa nazi

Binafsi nilizoea kula chakula kilichoungwa maziwa.

Yaani Wali wa Maziwa,

Mboga ya majani/maharage yameungwa maziwa n.k

Baada ya kuishi Pwani, nikaanza kuonja vyakula vya nazi

Kutokea hapo nimekuwa addicted na Vyakula vilivyoungwa Nazi.

Hivi mmewahi kula wali wa nazi, au dagaa zikaungwa nazi? Ama majani ya kunde yaliyoungwa Nazi je? 😋😋😋
 
Kuna Daktari mmoja aliniambia alihusika kwenye utafiti flani mkoa wa Pwani. Akasema waligundua Kuna idadi kubwa ya Watu matatizo ya presha. Hii inatokana na kula vyakula vya nazi kwa wingi.
 
Kwa mwenye uhitaji wa nazi tuwasiliane 0659445718, nazi zipo za kutosha, zikiisha unaweka oda kisha nakuletea.
 
umeuliza kitu ambacho kipo wazi sana. kwetu nazi ni kiungo cha heshima sana.

nikienda kumtembelea bi mkubwa, nikikaa siku 3 anaweza tumia nazi hata 10 kuanzia mboga mpaka wali wenyewe.

mambo hayo yanapatikana sana pwani especially Tanga.
Watu wa pwani wanapenda Kuna kipind zinafika moja 2000 ila mtu Bora apike mchele nusu na Nazi ya elf 2 kuliko kula wali wa mafuta hata migahawa midogo midogo ni wali Nazi
 
Wenyeji wa Mikoa ya Bara hatukuwa familiar sana na msosi wa nazi

Binafsi nilizoea kula chakula kilichoungwa maziwa.

Yaani Wali wa Maziwa,

Mboga ya majani/maharage yameungwa maziwa n.k

Baada ya kuishi Pwani, nikaanza kuonja vyakula vya nazi

Kutokea hapo nimekuwa addicted na Vyakula vilivyoungwa Nazi.

Hivi mmewahi kula wali wa nazi, au dagaa zikaungwa nazi? Ama majani ya kunde yaliyoungwa Nazi je? 😋😋😋
Hatari sana hapo kwenye majani ya kunde alafu ukute samaki kaungwa Nazi achilia maharage yaungwe Nazi alafu yalale😀😀
 
Back
Top Bottom